Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
- Thread starter
- #21
You missing something somewhere my friend, I think you better get the concept first if what you are saying is the case then hata kina Bush na wao wanastahili kifo unajua wamekufa watu wangapi Vietnam, Iraq, Somalia, Afghanstan na kwingeneko? na mauaji hayo yamefanywa na kusimamiwa na Serikali ya Amerika! Ugaidi una maana pana unaweza ukawa Ugaidi wa Taifa moja kulikandamiza taifa jingine au wa kikundi kukandamiza watu fulani fulani. Ugaidi huo huo unaweza ukafanywa na utawala dhidi ya raia zake.
Ifike sehemu tuone kwa jicho la tatu kuwa OBL kuuliwa sio dawa ila dawa wanyonge wapewe haki zao wenye mafuta waachiwe mafuta yao na wenye almasi waachiwe almasi zao si mnajua ya Savimbi?
Asanteni sana.
Mimi nadhani tatizo hapa ni kwamba "ugaidi" -- kwa mtazamo wa nchi za magharibi na wa watu wengine (hata humu JF) ni mauaji yanayofanywa kwa njia za kishenzi na zana za kishenzi. Kwa mfano kujilipua au kwa kutega/kurusha bomu katikati ya watu huuwa watu wasio hatia.
Kwa mtazamo huu vita, kama ile ya Iraq au Afghanistan ambazo pia zinasababisha watu wasio hatia kufa unainishwa kwamba siyo "ugaidi". Wenye mtazamo huu wanaona kwamba njia inayotumika na zana zinazotumika ni za kistaarabu zaidi -- yaani makombora ya Cruise na Tomahawk, vifaru, ndege za kivita nk nk.
Hapa ndipo I see the whole nonsense kwani kufa ni kufa tu -- ukitumia njia zozote -- hata za kistaarabu ni kufa tu! Adui yako usimchagulia silaha -- yaani iwapo mimi nataka kupigana na wewe na sina zana za kisasa, basi niruhusu nitumie njia na zana zangu duni tupigane. Najua sote tutauwa watu wasio hatia lakini usinitangaze eti mie gaidi kwa kuwa nauwa wasio hatia. Na wewe pia gaidi vile vile.
Kwa upande mwingine ndugu zangu -- vita ni ugaidi vile vile ni vigumu kulipinga hili -- kwa sababu watu wasio hatia nao hufa.