Haziwezi kufika huko ila zitashuka zaidi utanikumbuka wakati ukifika.
Nitakukumbusha wakati huo, lakini usiingie mitini
Haziwezi kufika huko ila zitashuka zaidi utanikumbuka wakati ukifika.
Hapo kwenye BLUE hilo ni swali zuri sana kama lingeulizwa lakini kwa jinsi ilivyo hakuna sehemu ambayo hawa jamaa wanaruhusu maswali na nafikiri wanajua wazi kama wakiruhusu issue ya maswali Mgimwa hawezi kujibu na isitoshe shujaa atakayejitokeza kuuliza swali lolote gumu inawezekana kabisa ndio ukawa mwisho wake kwani kinara wa Ugaidi ndani ya siasa za Tanzania ndie anayeendesha kampeni kwa upande wa CCM.hata mimi nimemsikia akiyasema hayo, busara ya kawaida tu wamuulize kwa mshahara wake mzuri na maisha yake mazuri huko ulaya, nini amewahi kufanya kwa wana-kalenga?
Pia Chriss Lukos anaogopa kuja Tena Tanzania na hususani kwao Iringa kwa kuwa amekula fedha za lambilambi za Marehemu mwangosi.
Mtu ameishi muda mwingi ULAYA, umeyajua saa ngapi matatizo ya wanaKalenga?Umbea huu tafuteni hoja za maana za kushindana na mgimwa japo naamini hamtaweza kabisa dogo yuko vizuri sana.
Hata lisu naye alishasemaga alikuwa Ulaya na alikuwa analipwa Mshahara mzuri ulaya, Kwa Mgimwa leo imekuwa ni ajabu? Acheni kudanganya wananchi , watu wanataka maendeleo waacheni waamue wenyewe.