Kuongoza taifa lililofanya makosa ya kuwa na majaribio ya uongozi wa nchi inahitaji karama, ujasiri, ushupavu, huruma hata ukatili ikibidi..awamu zilizopita ama kwa kujua au kutokujua ziliwafanya watanzania kuwa watu wa aina hii; wabinafsi, wapenda starehe, wavivu, wanafiki, wanapenda short cut, wanapenda vitu rahisi, hawataki kufikiri, WALALAMISHI, wasiopenda kujitoa(kusacrifice) kwa ajili ya manufaa siku za usoni, hawana uvumilivu..nk na hapa nina maana ya kuanzia awamu ya pili yaani uongozi baada ya Mwl. kuongoza watu wa aina hii ukitaka ufanikiwe ajenda ya maendeleo, na hasa ukiangalia kwa upeo wa mbali kdg ni vyema kutosikiliza lawama na kilio fake..Mtumishi wa Mungu Musa kama tunavyosoma kutoka maandiko matakatifu, alishindwa kuiona nchi ya ahadi kutokana na makwazo yaliyosababishwa na lawama nyingi na kukosa shukurani kwa anaowaongoza, akateleza akamkosea Mungu pakubwa! Ni jambo la msingi sana kumuombea Mh. Rais kwa kuwa anaongoza taifa lililoharibiwa kwa kiwango kikubwa ndani ya mioyo, akili na matarajio yao, hata kama kwa nje wanaonekana watu wenye ustawi na kusifia awamu zilizopita lakini uharibifu uliotokea kwa mtu wa ndani (kila binadamu ana mtu wa nje na wa ndani, mtu wa ndani ndiye anaelekeza mtu wa nje)kwa kila mmoja wa watanzania ni mkubwa sana!! wengi hawana maarifa haya ni ubishi tu unaoongozwa na uchoyo, tamaa na ubinafsi..wanaofahamu habari hii hawachoki kumuombea Rais kwa sababu ni wajibu ili taifa liendelee kuwepo na kustawi kama aliyeliumba anavyotaka. Kutopandisha mishahara hadharani hata kama ni kwa miaka yote kumi atakayokaa madarakani hakufanyi maisha yetu kukosa thamani na matumaini, wapo wengi na mifano ipo mingi mahali tofauti tofauti waliopitia hali za kutisha, magonjwa, vita, mauaji ya kimbari, maafa ya asili nk kwenye maisha yao kama nchi..lakin leo wanafaidi mema ya nchi zao! mambo ya mishahara ni madogo sana kwa kutimiza lengo la kuumbwa kwako!