Kuna kitu sijasikia watu wakikijadili sana ambacho Rais alikisema jana, ambacho hata mimi mwenyewe sijakielewa. Kuhusu fao la kujitoa. Alisema, Serikali imeamua (kwa kuwathamini wafanyakazi wa Tanzania) kukiacha kikokotoo cha zamani (Ambacho kwa maelezo ya Rais hakitumiki popote duniani) kiendelee kutumika. Kwa kufanya hivyo, Serikali imeamua kuchukua mzigo mkubwa ili kuwasaidia wafanyakazi wa Tanzania. I was totally confused. Mimi ni mfanyakazi. Nachangia kila mwezi kwa miaka zaidi ya 40 kabla ya kustaafu. Ninapopewa mkupuo wa asilimia 50 ya mafao yangu ya uzeeni kuna mtu au chombo kingine kimenifanyia hisani au huruma hapo? Hebu wahenga tusaidianeni hapa.