Kauli tata Mei Mosi 2019

Kauli tata Mei Mosi 2019

Maskini walimu wanatia huruma
Asante, but si walimu tu. Huu ni msiba wa taifa. Utasema mwanao anasoma private na mtoto wa rafiki yako, shangazi yako, mjombako na majority ya watz wanasoma wap?
Huko hospitali kuko salama? Kuna watu wengine wanauawa na manesi pasipokujijua. Iko siri watu wanaharibika viungo kwa kuchomwa sindano vibaya au dawa isiyosahihi. Ukichunguza kwa makini utagundua kuwa baadhi ya matukio hayo ni hasira za waganga kutendewa vibaya. Madaktari wamekuwa wakitufanyisha biashara. Anakuandikia dawa kanunue duka fulani kumbe dawa zipo lakini anatafuta 10%.
Walimu wengi wako vijijini na ndo benki za wakulima pia. Low purchasing power iliyoko vijijini sasahivi inawafanya wakulima kuishi maisha magum zaidi. Wanauza mazao yao kwa bei ya kutupwa. Debe la mahindi sh 2000 na hakuna mteja?
Wazazi wanashindwa kupeleka watoto hata shule za kata.
Huwezi amini hizo hela za elimu bure anazosema kapeleka shuleni anazichukua na kuzitumia mwenyewe. Mfano, umitashumta kuanzia wilaya hadi taifa inategemea michango toka shuleni.
Eti walimu wanasikitika, soon tutagundua nini kinaendelea. Mradi wa umeme ni bomu linasubiri kulipuka. MANENO HAYA HAYAWEZI KUELEWEKA HADI HAPO LITAKAPOTOKEA.
 
Alipaswa aongeze mwaka huu , maana kwamujibu wa katiba yetu huu ndiyo mwaka wake wa mwisho kabla ya kuingia duru ya pili ya uchaguzi, saaa mbona ana kuwa kama anajuwa kwamba na kipindi cha pili atapita bila kupingwa? Hii ni hatari kwa usala na amani ya nchi , iweje kwenye nchi inayo ongozwa na mfummo wa vyama vingi alafu ukawa na uhakika wa wewe kumaliza vipindi vyote viwili hii inatia ukakasi.
 
Kumbe CWT wana Mali nzuri namna hiyo?Picha ya KWANZA 2nd from left aje nimpunguzie kamshahara
 
Huyu braza yaani hajui hata kama kuna mtu anaongea maana inaonekana mbele yake kuna mtu anaongea ila hamwelewi kabisa halafu ni kama hamuoni vizuri au haamini kama kweli ni yule aliyemuahidi kitu!!!
Screenshot_2019-05-02-09-54-17-276_com.android.browser.jpeg
 
Sio hivyo tu,hata kakwepa kuahidi kuwa ataongeza mishahara mwakani na ni wazi hana uhakika kuwa hali itaruhusu kuongeza mishahara akaishia kutoa kauli/tungo tata kuwa ataongeza kabla hajatoka madarakani na wala msitarajien kuna siku watakuja na min budget ya kuongeza mishahara.

Huyu bwana ameshafeli na bado mtaona mengi siku zijazo(kajitishwa mzigo asiouweza na sasa umeanza kumuelemea na kuna siku atautua kwa aibu).
Tulivyo wajinga tunapiga makofi kabisaa.......na tutamchagua tena.
Hata Mungu anashangaa ni kwa nn
 
Back
Top Bottom