Inategemea mnagombana kwa ajili ya kitu gani,kama kuna tishio la wanawake wengine kwake unataka aseme nini ili akuzime ili maisha yenu yaendelee?Kila tukiwa na mtafaruku na mama watoto wangu ananambia kauli hii "Nitawapisha wengine waje wajaribu, nina kwetu" Hivi mwanamke aliyeolewa, yuko ndani ya ndoa zaidi ya miaka 10 anaweza kuendeleaje kufikiria kurudi kwao badala ya kufikiria kujenga mji wake ambao unaweza kuwa kimbilio kwa jamaa zake wanaoweza kuwa na matatizo?
Akili au matope??????
KAULI HII INANIKERA SANA!
Inategemea mnagombana kwa ajili ya kitu gani,kama kuna tishio la wanawake wengine kwake unataka aseme nini ili akuzime ili maisha yenu yaendelee?
Mwanamke siku zote fimbo yake ni mdomo hivyo kama unakereka na kauli kama hizo basi mtendee yaliyo mema na yasiyomtishia ndoa yake.
Jaribu kuweka na kiini cha ugomvi, pengine wewe ukawa ndio chanzo cha kila kasheshe kiasi mwanamke kaona yanaelekea kumshinda.
Kila tukiwa na mtafaruku na mama watoto wangu ananambia kauli hii "Nitawapisha wengine waje wajaribu, nina kwetu" Hivi mwanamke aliyeolewa, yuko ndani ya ndoa zaidi ya miaka 10 anaweza kuendeleaje kufikiria kurudi kwao badala ya kufikiria kujenga mji wake ambao unaweza kuwa kimbilio kwa jamaa zake wanaoweza kuwa na matatizo?
Akili au matope??????
KAULI HII INANIKERA SANA!
Kuna mengi katika maisha ya ndoa zaidi ya watoto, haijalishi ni ndoa ya kanisani au msikitini,kama huna hawala ila mazingira yote yanayokuzunguka yanaonesha hivyo unategemea nini toka kwa mwenza wako?Kama yapi Jose?
Ameolewa kwa ndoa ya kanisani;
Tumejaliwa watoto tena kwa kuchanganya jinsia;
Anaishi kwake;
Sina hawala;
Nifanyeje ndugu yangu!
Kama hizi ndio lugha zako za kumwongela mkeo unategemea nini? Hivi kweli mke unayempenda kwa dhati hata akikosea unaweza kuwaambia watu kwamba akili zake ni matope! Kweli? Huna heshima kwa mke wako, labda una unao waheshimu ndio maana anataka kuwapisha wenye akili nzuri.
Jifanyie assessment ya jinsi gani ambavyo huwa unahandle huo mtafaruku, kamwombe samahani kwamba umemtukana kwenye mhadhara wa watu wa JF na kwingine kote utakakokuwa umewahi kuyatamka haya.
Kifupi: Jichunguze, umenikera kweli kweli! Hivi wanaume wa siku hizi tukoje? Inaonekana hata siri zake zingine unatangazaga wewe, ndio maana anaona unamdharau wazi wazi!
Akikosea mwabie, haya ulitakiwa umwambia yeye, sasa unatuambia sisi tukamwambie au?
Kuna mengi katika maisha ya ndoa zaidi ya watoto, haijalishi ni ndoa ya kanisani au msikitini,kama huna hawala ila mazingira yote yanayokuzunguka yanaonesha hivyo unategemea nini toka kwa mwenza wako?
Maisha ya ndoa ni magumu sana hasa kwa vile nyie mmekutana huku mkiwa mmelelewa katika mazingira tofauti hivyo kuoneshana tabia tofauti ni jambo la kawaida na yafaa ukawa mvumilivu kwa mwenzio,na kama unaona hukosei basi kaa nae chini na zungumza nae jambi hili na mtafikia muafaka maana kwangu mimi si rahisi mwanamke kukwambia ana kwao na kusiwe na sababu inayomfanya aseme maneno hayo.
Kwa wanandoa chokochoko za hapa na pale huwa hazikosi; huwa ni kuheshimiana tu ndo amani inakuwemo ndani.
inakera kweli, sasa huyu mwananke ana matatizo, kwanza yawezekana anasema hivo kukutisha unajua tena wanawake akili zao ndogo saana, pili yawezekana ni mambo ambayo aliyazoea kuyasema bila kumaanisha, au background ya familia yake wazazi walikua wanatishana mbele ya watoto mambo kama hayo, ila kama hana makosa makubwa ya kumwacha, mpende mtimizie ilyo haki yake, nadhani mtaelewana kwani kupishana kimawazao katika familia ya wawili mbona kawaida, mwanaume pia unakosea, ila maana na msingi kusaeheana wongo jombaaaaaa
Basi jaribu kukaa na huyo mwenzi wako akueleze nini haswa huwa kinamkera toka kwako....pengine huwa hamna wasaa wa kurekebishana pale mnapokoseana zaidi ya kutumia maneno ya hasira na kejeli...
ndugu yangu akili za wanawake wengi kama sio 98% walioolewa huwa ni kurudi nyumbani tu.....ukikuta wachache wanaojiweza huwa wanakaa na familia zao na wako confident hata wakiachika watakaa wenyewe bila kurudi nyumbani.....