The Genius
JF-Expert Member
- May 29, 2018
- 820
- 2,070
Sayansi haisemi uongo, Ila uongo unaweza kujitengenezea sayansi yake.
Uchunguzi wa kimahakama wa matukio ya uhalifu ni uchunguzi wa kisaynsi unaolenga kukusanya ushahidi usio na shaka na kisha kuwapata wahalifu. Taaluma hii ni ngumu, tofauti na inavyoonekana kwenye filamu na riwaya.
Kanuni moja mujimu ni kwamba, kila muhalifu anaacha alama; hii ni kanuni maarufu kutoka kwenye maandiko ya mtaalamu wa sayansi hii, Dr. Edmond Locard.
Kila muhalifu anaacha alama anapofanya uhalifu wake, alama ambayo itatumika kumkamata.
Anakamatwaje? Uwezo wa timu ya uchunguzi, fedha, muda, ari ya kufanya kazi, ushirikiano baina ya wanataaluma mbalimbali na zana za kufanyia kazi ya uchunguzi - ni mamno yanayoathiri mchakato wa uchunguzi wa kimahakama. Ikiwa mambo hayo yatafanywa kuwa bora, basi wahalifu halisi watakamatwa.
Ikiwa muhalifu naye anajua mbinu za uchunguzi, basi anaweza kupoteza ushahidi na kuwachanganya wachunguzi - lakini alama za uhalifu kamwe hazifutiki.
Mtu mmoja alimuua mwanamke mmoja na kumtupa porini. Muuaji alivaa kificha uso, na glavu, kisha baada ya mauaji aliketeza kila kitu alichovaa kwa moto. Lakini hakujua, wakati dada huyo alipokuwa akipambania maisha yake, alifanikiwa kumfinya yule muuaji usoni. Vipande vidogo vya seli ya ngozi vilivyokutwa kwenye kucha za marehemu vilipimwa DNA, na muuaji alipatikana.
Unaweza kukimbia, lakini huwezi kujificha dhidi ya sayansi; panapo muda wa kutosha, uwezo wa kitaalum, zana za kisasa, ari, siha, utashi na moyo wa kufanya kazi...muhalifu atapatikana.
Uchunguzi wa kimahakama wa matukio ya uhalifu ni uchunguzi wa kisaynsi unaolenga kukusanya ushahidi usio na shaka na kisha kuwapata wahalifu. Taaluma hii ni ngumu, tofauti na inavyoonekana kwenye filamu na riwaya.
Kanuni moja mujimu ni kwamba, kila muhalifu anaacha alama; hii ni kanuni maarufu kutoka kwenye maandiko ya mtaalamu wa sayansi hii, Dr. Edmond Locard.
Kila muhalifu anaacha alama anapofanya uhalifu wake, alama ambayo itatumika kumkamata.
Anakamatwaje? Uwezo wa timu ya uchunguzi, fedha, muda, ari ya kufanya kazi, ushirikiano baina ya wanataaluma mbalimbali na zana za kufanyia kazi ya uchunguzi - ni mamno yanayoathiri mchakato wa uchunguzi wa kimahakama. Ikiwa mambo hayo yatafanywa kuwa bora, basi wahalifu halisi watakamatwa.
Ikiwa muhalifu naye anajua mbinu za uchunguzi, basi anaweza kupoteza ushahidi na kuwachanganya wachunguzi - lakini alama za uhalifu kamwe hazifutiki.
Mtu mmoja alimuua mwanamke mmoja na kumtupa porini. Muuaji alivaa kificha uso, na glavu, kisha baada ya mauaji aliketeza kila kitu alichovaa kwa moto. Lakini hakujua, wakati dada huyo alipokuwa akipambania maisha yake, alifanikiwa kumfinya yule muuaji usoni. Vipande vidogo vya seli ya ngozi vilivyokutwa kwenye kucha za marehemu vilipimwa DNA, na muuaji alipatikana.
Unaweza kukimbia, lakini huwezi kujificha dhidi ya sayansi; panapo muda wa kutosha, uwezo wa kitaalum, zana za kisasa, ari, siha, utashi na moyo wa kufanya kazi...muhalifu atapatikana.