mimi nadhani utoto wako na kutofuatilia mambo kweli utakuwa umechangia kufikiri kama unavyofikiri.kwani kenya ODINGA alipata kura ngapi na KIbaki alipata ngapi?ni upi ulikuwa msimamo wa tume ya uchaguzi ya kenya kuhusu matokeo?ni upi ulikuwa msimamo wa waangalizi wa kumataifa kuhusu matokeo yale?ni upi ulikuwa msimamo wa mashirika ya kimataifa na mataifa mbalimbali juu ya uchaguzi ule?je?unafahamu slaa alipata kura asilimia ngapi dhidi ya rais kipenzi cha watu Ndug.JAKAYA KIKWETE? JE?unafahamu nini ulikuwa msimamo wa tume ya uchaguzi tanzania na waangalizi mbalimbali wa uchaguzi?je?unadhani slaa alikuwa na haki ya kukataa matokeo;au kufanya hivyo ingekuwa ni kosa kisheria na madhara yote ambayo yangejitokeza ingekuwa ni matokeo ya kosa hilo?kama kufanya hivyo ingekuwa ni kosa;vipi umpongeze mtu kwa kutofanya kitu ambacho hata hivyo hakutakiwa akifanye?
Mkuu betlehem ni kheri kuwa na hofu ya Mungu kwani usingeweza tumia nguvu kubwa kupindisha ukweli. Thanx LORD wanajamvi hatudanganyiki. Nakuomba usome vipengele vifuatavyo kwa umakini otherwise hutanielewa;
1.Kwa maelezo yako unataka tuamini kuwa Kibaki alishinda ki-halali kwa njia ya kura zilizopigwa na wakenya au ni kutumia nguvu ya tume ya uchaguzi? Wakenya wanasema aliyeshinda ni Odinga we mtz hata ambaye huku hudhuria uchaguzi huo unasema hapana Kibaki ndo' aliyeshinda, je tumwamini nani?
2.Endapo uchaguzi wa kenya ulikuwa wa huru na haki kwa nini mwenyekiti wa tume ya uchaguzi alikimbilia ugaibuni?
3.Endapo uchaguzi wa kenya ulikuwa wa huru na haki kwa nini baadhi ya viongozi nchini kenya wakabiliwe na kesi ya kujibu ICC the Hegue?
4.Je unataka tuamini kuwa Jeikei alishinda kwa kura tulizopiga mwaka 2010 au alishinda kwa nguvu ya tume ya uchaguzi,usalama wa taifa na vyombo vingine vya dola?
5.Kama Jeikei alishinda kihalali,kwa nini hadi leo hii hawajaweka matokeo ya u-rais kwenye website ya NEC?.
6.Ukweli utabaki palepale Dr. Slaa alishinda kwa kishindo. Hakupinga matokeo kwa sababu katiba ya nchi hairuhusu,ila unapaswa kufahamu kilicho sababisha nchi hii kuendelea na utulivu tulionao ni busara za. Dr. Slaa, otherwise angekuwa ni mtu mwenye tamaa ya madaraka nchi hii ingewaka.
7. Dr. Slaa ni tishio ndo' maana mara tu baada ya uchaguzi mlianza kumuandama ili kumdhoofisha yeye mwenyewe na CHADEMA,lakini nachelea kusema magamba mmechemsha.
8.Inaonekana wewe ni mvivu wa kusoma, nakuomba ukasome report ya waangalizi wa ki-mataifa ilisemaje kuhusiana na uchaguzi wa 2010 nchini Tanzania.
9.Umejikita sana kwenye msimamo wa tume ya uchaguzi. Lakini inakupasa utambue ya kuwa maamuzi ya tume ya uchaguzi siyo maamuzi ya watanzania zaidi ya milioni arobaini, ndo' maana tunaomba tume huru na siyo kuteuliwa na mgombea.
10.Mkuu inabidi ukubali uwezo wako wa ku-analyse issues ni mdogo sana ndo' maana hata kijana wa kidato cha tatu amekufunika.
Wana janvi naomba kuwasilisha.