Hapana shaka unasubiri kwa hamu watokeo ya uchaguzi wa marudio utakaofanyika kesho tarehe 16.06.2013. Uchaguzi huu ni ishara ya kutambua mwelekeo wa CCM na CHADEMA kuelekea uchaguzi wa 2014/2015. Si vibaya ukapata muda wa kupitia ufafanuzi huu juu ya Dr. Slaa na Hatma ya Taifa letu.
Wakati unasubiri kwa hamu matokeo, hapana shaka leo hii Dr.Slaa ni moja ya Wanasiasa maarufu nchini. Kukataa kukiri ukweli huu ni ukosefu wa ukomavu wa kisiasa au mgogoro wa nafsi juu ya umaarufu huu. Lakini vilevile ni jambo lisilo na ubishi kwamba umaarufu wa Dr.Slaa nchi nzima unadhihirishwa na:
- Umati unaohudhuruia mikutano yake
- Jinsi vyombo vya habari vinavyomfuatilia na
- Homa ya Dr.Slaa kwa viongozi na wanachama wa CCM juu ya hatma ya chama chao.
Baadhi ya mambo mahususi yanayomtafautisha Dr.Slaa na wanasiasa wa vyama vingine hasa Chama Cha Mapinduzi(CCM) ni kama ifutavyo:
- Wakati Wapinzani wake kisiasa wanapanga mbinu na mikakati ya kumchafua, Dr.Slaa anazidi kuimarika kisiasa nchi nzima.
- Wakati wanasiasa maarufu nchini wanatafuta fedha, kujipendekeza kwa viongozi wa madhehebu ya dini, asasi za kiraia na makundi mengine katika harakati za kujenga mtandao wa kusaka Uraisi, Dr.Slaa anaendelea kuelimisha umma na kuibua fikra chanya juu ya mustakabali wa kizazi cha leo na vijavyo.
Umakini, ujasiri na uthubutu wake kisiasa unamtafautisha sana na wanasiasa wengi ambao wameifanya tasnia ya siasa kuwa mradi wa kiuchumi na kusaka madaraka kwa gharama yoyote ile. Kwa mafisadi, umaarufu wa Dr.Slaa katika kutetea maslahi ya makundi mbalimbali katika jamii ni KIKWAZO.
Katika muongo mmoja, Dr.Slaa amechangia sana kuibua kashfa mbalimbali ambazo ni kikwazo kwa ustawi wa Taifa. Mfano:
- Ufujaji wa fedha ndani ya benki kuu kupitia mfuko wa madeni ya nje (EPA),
- Kashfa ya mkataba wa serikali na kampuni ya Alex Stewarts.
- Kashfa inayohusu Makampuni ya Mwananchi Gold na Deep Green,
- Kashfa ya Richmond iliyomwondoa Bwana Lowassa, Nazir Karamagi na Msabaha n.k.
Ni wanasiasa wachache sana nchi hii ambao wanafanya tafiti na wana-uthubutu wa kuibua ufisadi unaoathiri ustawi wa Taifa hili. Bila tafiti Dr.Slaa angeingia kwenye matatizo makubwa ya kisiasa.
Pamoja na mijadala inayoibuliwa ya kifamilia, kidini n.k, ambayo inatokana na hila na njama zinazosukwa na washindani wake kisiasa kuwafanya watu waamini kuwa hana maadili na Mbaguzi. Dr.Slaa anazidi kupendwa, kuheshimiwa na kuaminiwa na wananchi. Kama wahenga walivyosema "Dua ya Kuku halimpati Mwewe", vilevile njama hizi hazitafua dafu juu ya Mpango wa Mungu kwa Taifa hili.
Baada ya kupitia Maelezo haya ni ukweli usipingika (undeniable truth) kwamba Dr.Slaa ni Mwanasiasa bora wa Muongo (Decade) na nyota inayoongoza kwa kung'aa katika tasnia ya siasa nchini. Ni Wanasiasa mchanga tu kifikra au wafitini ambao wanamuona Dr.Slaa ni mtu mzushi na asiye na akili nzuri, bila kutambua wanafanya kazi ambayo hawaijui.
Nawakilisha.