Stephano Mango
Member
- Mar 23, 2012
- 64
- 13
Na Stephano Mango, Songea
KATIBU wa Chama Cha Tanzania Labour party (TLP) jimbo la Songea mkoani Ruvuma Joseph Mkondora (72) ametangaza kujivua uwanachama wa chama hicho ambacho amedai kuwa kimepoteza mwelekeo na badala yake ameamua kujiunga na Chama Cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ambacho ndio chama pekee cha upinzani kinacho onyesha kwa dhati dira ya maendeleo kwa watanzania.
Akizungumza na waaandishi wa habari jana kwenye hoteli ya Majimaji mjini Songea Mkondora alisema kuwa kwa kauli yake yeye mwenyewe ameamua kujivua uwanachama wa chama hicho na kujiunga na CHADEMA kwa sababu mwenyekiti wa TLP Taifa Agustino Liyatonga Mrema tangu achaguliwe kuwa Mbuge wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro ameshindwa kabisa kuangalia hali halisi ya TLP inavyoendelea kudorola kwenye jimbo la Songea mjini na badala yake anaonekana kuwa ni wakala wa chama cha CCM.
Mkondora ameeleza zaidi kuwa chama cha TLP katika Jimbo la Songea mjini mpaka sasa siku hadi siku kinaendelea kupoteza mwelekeo kwani hali ya kisiasa sio nzuri kabisa licha ya kuwa taarifa ya hali hiyo alicha ipeleka makao makuu ya chama cha TLP lakini mpaka sasa hakuna majibu ya aina yeyote yaliyoletwa.
Alisema kuwa amekuwa akifanya mawasiliano ya mara kwa mara na TLP makao makuu kuelezea hali halisi ya mwenendo mzima wa chama lakini jambo la kushangaza uongozi wa chama hicho umekaa kimya kabisa
Ndugu zangu waandishi hali ya TLP jimbo la Songea mjini iko taabani kisiasa kwani hapo awali ilikuwa na wanachama zaidi ya elfu saba lakini hivi sasa chama hicho kimebakiwa na wanachama kumi na moja tu ndio maana kwa ukimya wa uongozi wa TLP makao makuu chini ya Mwenyekiti wa chama hicho Agustino Mrema unahofiwa kuwa umekuwa ni mawakala wa CCM ambao umekuwa ukitengeneza mazingira ya wanachama wake kujiondoa alisema Mkondora
Alifafanua zaidi kuwa kwa muda mrefu amekitumika chama hicho akiwa kiongozi kwa nafasi hiyo lakini tangu mwenyekiti wa TLP Taifa Mrema alipochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Vunjo ameonekana kuwa hakijali kabisa chama chake na badala yake anaonekana kuwa ni mpiga debe wa CCM kwenye jimbo hilo.
Mkondora amesema kuwa kutokana na hali hiyo iliyopo ndani ya TLP ameamua kwa dhati kukiama chama cha TLP na kujiunga na Chadema ambako amepokelewa kwa baraka zote na sasa hivi anatarajia kukabidhi mali za chama cha TLP ambazo alikuwa anazitunza ambapo alizitaja kuwa ni Kadi za chama hicho, Majarada ya ofisi , Vitabu mbalimbali vikiwemo vitabu vya katiba ya TLP, ikiwepo samani za ofisi pamoja na bendera moja ya TLP kwa mwenyekiti wa jimbo la Songea mjini Daudi Mpangala ambaye naye anasita kukabidhiwa mali hizo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama hicho jimbo la Songea mjini Daudi Mpangala alipoulizwa na kuhusiana na kujivua uwanachama Katibu wake Mkondora alisema kuwa ni vigumu yeye kuzungumzia kwa wazi kiasi hicho lakini anatarajia kuitisha kamati yake ya utendaji ili kupata ufafanuzi wakujivua uwanachama kiongozi huyo.
Hata hivyo Katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) jimbo la Songea mjini Masumbuko Paul Masumbuko alithibitisha kumpokea Joseph Mkondora ambaye alikuwa ni mmojawapo kati ya wanachama wapya 52 wakiwemo mabalozi toka CCM ambao waliojiunga na chama hicho wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya udiwani kata ya Lizaboni ambayo iliachwa wazi na Ali Manya aliyefariki dunia miezi sita iliyopita ambapo katika uchaguzi huo mgombea udiwani kupitia chadema Alanusa Mlongo aliibuka kuwa mshindi kwa kumwaga mgombea wa udiwani kupitia CCM George Odo Mbunda.
Mwisho.
KATIBU wa Chama Cha Tanzania Labour party (TLP) jimbo la Songea mkoani Ruvuma Joseph Mkondora (72) ametangaza kujivua uwanachama wa chama hicho ambacho amedai kuwa kimepoteza mwelekeo na badala yake ameamua kujiunga na Chama Cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) ambacho ndio chama pekee cha upinzani kinacho onyesha kwa dhati dira ya maendeleo kwa watanzania.
Akizungumza na waaandishi wa habari jana kwenye hoteli ya Majimaji mjini Songea Mkondora alisema kuwa kwa kauli yake yeye mwenyewe ameamua kujivua uwanachama wa chama hicho na kujiunga na CHADEMA kwa sababu mwenyekiti wa TLP Taifa Agustino Liyatonga Mrema tangu achaguliwe kuwa Mbuge wa jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro ameshindwa kabisa kuangalia hali halisi ya TLP inavyoendelea kudorola kwenye jimbo la Songea mjini na badala yake anaonekana kuwa ni wakala wa chama cha CCM.
Mkondora ameeleza zaidi kuwa chama cha TLP katika Jimbo la Songea mjini mpaka sasa siku hadi siku kinaendelea kupoteza mwelekeo kwani hali ya kisiasa sio nzuri kabisa licha ya kuwa taarifa ya hali hiyo alicha ipeleka makao makuu ya chama cha TLP lakini mpaka sasa hakuna majibu ya aina yeyote yaliyoletwa.
Alisema kuwa amekuwa akifanya mawasiliano ya mara kwa mara na TLP makao makuu kuelezea hali halisi ya mwenendo mzima wa chama lakini jambo la kushangaza uongozi wa chama hicho umekaa kimya kabisa
Ndugu zangu waandishi hali ya TLP jimbo la Songea mjini iko taabani kisiasa kwani hapo awali ilikuwa na wanachama zaidi ya elfu saba lakini hivi sasa chama hicho kimebakiwa na wanachama kumi na moja tu ndio maana kwa ukimya wa uongozi wa TLP makao makuu chini ya Mwenyekiti wa chama hicho Agustino Mrema unahofiwa kuwa umekuwa ni mawakala wa CCM ambao umekuwa ukitengeneza mazingira ya wanachama wake kujiondoa alisema Mkondora
Alifafanua zaidi kuwa kwa muda mrefu amekitumika chama hicho akiwa kiongozi kwa nafasi hiyo lakini tangu mwenyekiti wa TLP Taifa Mrema alipochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Vunjo ameonekana kuwa hakijali kabisa chama chake na badala yake anaonekana kuwa ni mpiga debe wa CCM kwenye jimbo hilo.
Mkondora amesema kuwa kutokana na hali hiyo iliyopo ndani ya TLP ameamua kwa dhati kukiama chama cha TLP na kujiunga na Chadema ambako amepokelewa kwa baraka zote na sasa hivi anatarajia kukabidhi mali za chama cha TLP ambazo alikuwa anazitunza ambapo alizitaja kuwa ni Kadi za chama hicho, Majarada ya ofisi , Vitabu mbalimbali vikiwemo vitabu vya katiba ya TLP, ikiwepo samani za ofisi pamoja na bendera moja ya TLP kwa mwenyekiti wa jimbo la Songea mjini Daudi Mpangala ambaye naye anasita kukabidhiwa mali hizo.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama hicho jimbo la Songea mjini Daudi Mpangala alipoulizwa na kuhusiana na kujivua uwanachama Katibu wake Mkondora alisema kuwa ni vigumu yeye kuzungumzia kwa wazi kiasi hicho lakini anatarajia kuitisha kamati yake ya utendaji ili kupata ufafanuzi wakujivua uwanachama kiongozi huyo.
Hata hivyo Katibu wa chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) jimbo la Songea mjini Masumbuko Paul Masumbuko alithibitisha kumpokea Joseph Mkondora ambaye alikuwa ni mmojawapo kati ya wanachama wapya 52 wakiwemo mabalozi toka CCM ambao waliojiunga na chama hicho wakati wa kampeni za uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi ya udiwani kata ya Lizaboni ambayo iliachwa wazi na Ali Manya aliyefariki dunia miezi sita iliyopita ambapo katika uchaguzi huo mgombea udiwani kupitia chadema Alanusa Mlongo aliibuka kuwa mshindi kwa kumwaga mgombea wa udiwani kupitia CCM George Odo Mbunda.
Mwisho.