Katiba Mpya: Clouds FM Wachochezi!

Katiba Mpya: Clouds FM Wachochezi!

Donyongijape

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2010
Posts
1,497
Reaction score
814
Habari za asubuhi wadau. Asubuhi ya Leo Nimesikia taarifa maalumu ya mtu anayeitwa PJ, wa Clouds FM, akiitoa kuhusu vikao vya bunge maalumu huko Dodoma. Taarifa ile ilikuwa ikiwaambia wananchi kile kinachoendelea huko na kuwapa taadhari kuwa kuna kikundi kimejiandaa kuvunja bunge hilo. Huku pia akisema kuwa kuna mjumbe mmoja ambaye ni kiongozi wa juu kabisa wa chama cha upinzani aliteuliwa kuingia kwenye kamati ya uongozi lakini kwa sababu 'anazozijua mwenyewe' akajitoa.

Tatizo langu hapa ni namna ya uwasilishaji wa taarifa hiyo. Haijafuata ueledi wa habari kwani haikuwa na FACTS kama taaluma ya habari inavyotaka. Ilikuwa haina vithibitisho vya hizo njama, au kuwapa wasikiliazi fursa ya kusikiliza kile kilichotokea katika bunge hilo.

Mimi naona huu ni UCHOCHEZI ambao ni hatari kwa taifa na unalenga kujenga chuki miongoni mwa jamii. Mamlaka inayohusika na vyombo vya habari inabidi kuingilia kati na kutoa adhabu stahiki kwa vyombo vya habari vya namna hii. La sivyo vitatufikisha katika hali mbaya na kuhatarisha amani ya nchi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
 
Watangazaji wa Clouds isia mbele kuliko maadili ya uandishi!kama jambo halipendi mtangazaji basi....anaweka chuki zake
 
Hao jamaa wamegeuka kuwa chombo cha habari na propaganda za CCM...kwenye Tv yao ndani ya King`amuzi cha Azam huwa napita nikiwa nashuka chini kutazama Sentanta Tv yangu.
Nikakuta wameanzisha kitu wanaita Uzalendo Kwanza sijui nini niniiiii....jamaa anaongea nyuma background ni bendera ya Tanzania,anasema rangi ya blue ktk bendera ni bahari inayotuunganisha Tz Bara na Visiwani ili kuuimarisha Muungano.(Upotoshaji mkubwa,anasahau hiyo blue hata ziwa Rukwa inawakilishwa nayo)
Wanatumika kubeba hoja ya Serikali mbili,wanatumika kuua hoja ya serikali tatu na Mamlaka kamili ya Znz,wanapotosha watu juu ya kuidai Tanganyika itambulike.
Huyo PJ ni mzee fulani anayetumika bila kujijua....wasamehe bure,hata shule zao vichwani ni za mashaka,ni lazma wajipendekeze ili wabaki mjini
 
Naamin kama TCRA wapo makin watawahoji,moja ya mistari ya PJ ile inayosema kuna njama za kuifanya tanzania isitawalike baada ya kuvuruga mchakato wa katiba,,,,kumepangwa kufanyika machafuko pande zote za nchi hii,binafsi nilishtuka
 
Huyo anawapamba ccm ili aendelee kula ofa za bia na nyama choma huko Dodoma.
Ni ombaomba tu huyo anaejipendekeza.
 
Safi sana Clouds fm, huo ndio ukweli kuna watu wana njama hizo bora Wajue sasa , na wanajulikana, ni chadema,Lipumba(amedanganywa),Mbatia, na Maalimu Seif.

Hawa ni hatari sana mkiwaona wapigwe tu.
 
Utu wa mtu ubebwa na mtu mwenyewe,na ukitaka kujua akili ya mtu mpe nafasi ya kusema au kutenda
 
Habari za asubuhi wadau. Asubuhi ya Leo Nimesikia taarifa maalumu ya mtu anayeitwa PJ, wa Clouds FM, akiitoa kuhusu vikao vya bunge maalumu huko Dodoma. Taarifa ile ilikuwa ikiwaambia wananchi kile kinachoendelea huko na kuwapa taadhari kuwa kuna kikundi kimejiandaa kuvunja bunge hilo. Huku pia akisema kuwa kuna mjumbe mmoja ambaye ni kiongozi wa juu kabisa wa chama cha upinzani aliteuliwa kuingia kwenye kamati ya uongozi lakini kwa sababu 'anazozijua mwenyewe' akajitoa.

Tatizo langu hapa ni namna ya uwasilishaji wa taarifa hiyo. Haijafuata uelewe wa habari kwani haikuwa na FACTS kama taaluma ya habari inavyotaka. Ilikuwa haina vithibitisho vya hizo njama, au kuwapa wasikiliazi fursa ya kusikiliza kile kilichotokea katika bunge hilo.

Mimi naona huu ni UCHOCHEZI ambao ni hatari kwa taifa na unalenga kujenga chuki miongoni mwa jamii. Mamlaka inayohusika na vyombo vya habari inabidi kuingilia kati na kutoa adhabu stahiki kwa vyombo vya habari vya namna hii. La sivyo vitatufikisha katika hali mbaya na kuhatarisha amani ya nchi.
God bless us
 
Kadri siku zinavyozidi kwenda mtaacha kusikiliza Redio na TV zote, anzisheni za kwenu muwe mnaangalia wenyewe.
 
Naamin kama TCRA wapo makin watawahoji,moja ya mistari ya PJ ile inayosema kuna njama za kuifanya tanzania isitawalike baada ya kuvuruga mchakato wa katiba,,,,kumepangwa kufanyika machafuko pande zote za nchi hii,binafsi nilishtuka

Hata mimi nataka nione mamlaka husika itafanya nini???maaana hiyo ya kusema kuna watu wamepanga kufanya machafuko nchi nzima,basi yeye atakuwa wa kwanza kusaidia...Haya majitu yanatumika vibaya sana,njaa inawapeleka kubaya sana....Wakati mwingine kuajiliwa kwa kujipendekeza bila Academic Merits ni utumwa!!!Hii ndio hali ya hawa vilaza wa Clouds
 
Back
Top Bottom