MGOGOHALISI
JF-Expert Member
- Apr 16, 2011
- 4,479
- 6,532
Hao jamaa wamegeuka kuwa chombo cha habari na propaganda za CCM...kwenye Tv yao ndani ya King`amuzi cha Azam huwa napita nikiwa nashuka chini kutazama Sentanta Tv yangu.
Nikakuta wameanzisha kitu wanaita Uzalendo Kwanza sijui nini niniiiii....jamaa anaongea nyuma background ni bendera ya Tanzania,anasema rangi ya blue ktk bendera ni bahari inayotuunganisha Tz Bara na Visiwani ili kuuimarisha Muungano.(Upotoshaji mkubwa,anasahau hiyo blue hata ziwa Rukwa inawakilishwa nayo)
Wanatumika kubeba hoja ya Serikali mbili,wanatumika kuua hoja ya serikali tatu na Mamlaka kamili ya Znz,wanapotosha watu juu ya kuidai Tanganyika itambulike.
Huyo PJ ni mzee fulani anayetumika bila kujijua....wasamehe bure,hata shule zao vichwani ni za mashaka,ni lazma wajipendekeze ili wabaki mjini
Waandae tu disco zao haya mambo ya siasa hawayawezi, wamwulize mwenzao yule wa kasha sasa hivi anahenyeka na ICC