Ntuzu
JF-Expert Member
- Aug 8, 2013
- 17,418
- 10,852
Naamini kama ni Media Kakobe kaanza muda sana, na kama kusikika kwenye media za Bongo ndio kujiona basi Kakobe angeliweza kujisifu sana.
Suala hapa Kakobe huwa hatafuti kujikomba komba kwa watawala, tangu nimeanza kumsikia askofu huyu misimamo ambayo amekuwa anaitoa ni misimamo ambayo inakung'uta serikali, ndio maana hawana hamu nae.
Aliwahi kupinga nguzo za umeme zisipite kwenye kanisa lake kutokana na msongo mkubwa wa umeme. Serikali hii ya JK kwa jeuri na dharau wakati huo waziri wa nishati akiwa Ngeleja walipitisha umeme huo. Ila akawaonya kwa kuwa wametumia ubavu umeme wao hautawaka.
Serikali tangu imalize kufunga nguzo na kuweka nyaya, hawajarudi tena kuwaeleza watanzania, mradi huo wa MAKUMBUSHO- UBUNGO unafanya kazi?? na utazinduliwa lini?
sasa na hili la kuisambaratisha CCM alilitoa baada ya serikali kutoa majibu ya dharau kuwa haikupokea majina ya wapentekoste. Kakobe aliudhika sana na ile kauli akaamua kuomba na kuuliza kwa Mungu; serikali hii itawadharau wapentekoste hv hata lini??
majibu yaliyotoka yamo kwenye waraka alioutoa. Kitu cha ajabu Tangu waraka ule utolewe Kakobe hajawazi kuuzungumzia, aliutoa hivyo basi. Na wamo watu humu ambao nao naona wamejaa dharau kama serikali yetu, OLE WENU NINYI. Kakobe sio TB JOSHUA,
Acheni uongo nyie. Mpo kuhubiri ufalme Wa Mungu au Wa duniani hapa?