Kati ya Suzuki carry na Guta kipi bora?

Kati ya Suzuki carry na Guta kipi bora?

Kwa maoni yangu chukua GUTA ya KIHINDI TOYO mwaka jana nilichukua moja cc250.
Mungu ni mwema mambo yameenda vzr kiasi nimeongeza moja juzi cc200.
Pia kwenye service akuna galama kubwa kwa GUTA ya KIHINDI TOYO.
Chuma nasubilia this week TRA wamalixie usajili wao kitu kiingie kwa njia.
Mkuu tunaweza chonga kitu pm?
 
Hivi ni sababu zipi zinnazowafanya watu wadai guta ina nguvu kuĺiko suzuki carry wakati kitaalamu specs zake ni zaidi ya guta,mfano engine displacement na horsepower?Kumbuka the bigger the volume,the powerful the engine.
Kiuhalisia ndo ipo hivo ila ukienda ukubwa wa engine Suzuki inaonekana Ina cc kubwa lkn ukiziwekea mzigo ule ule utakuta baada ya mwaka mmoja engine ya Suzuki inakua haijiwezi kabisa, asilimia 70 utakuta body ya zamani engine mpya.

Sababu hasa nafikiri zipo mbili Kwa mtazamo wangu, haya maguta yana gia inaitwa rock diff, ikiwekwa hiyo gia kale kadude sijui kanatoaga wapi ule ubavu.
Sababu ya pili, gari hata kabla haijawekea mzigo tayari yenyewe ni mzigo, namaanisha body ya Suzuki Ina vyuma vingi na mambo mengine lakn guta ni jepesi likiwa bila mzigo, Kwa hiyo litadai mzigo mkubwa ili kuendana na power yake tofauti na carry.
 

Attachments

  • markup_1000024702.png
    markup_1000024702.png
    1.9 MB · Views: 82
Kiuhalisia ndo ipo hivo ila ukienda ukubwa wa engine Suzuki inaonekana Ina cc kubwa lkn ukiziwekea mzigo ule ule utakuta baada ya mwaka mmoja engine ya Suzuki inakua haijiwezi kabisa, asilimia 70 utakuta body ya zamani engine mpya.

Sababu hasa nafikiri zipo mbili Kwa mtazamo wangu, haya maguta yana gia inaitwa rock diff, ikiwekwa hiyo gia kale kadude sijui kanatoaga wapi ule ubavu.
Sababu ya pili, gari hata kabla haijawekea mzigo tayari yenyewe ni mzigo, namaanisha body ya Suzuki Ina vyuma vingi na mambo mengine lakn guta ni jepesi likiwa bila mzigo, Kwa hiyo litadai mzigo mkubwa ili kuendana na power yake tofauti na carry.
Bado sijapata hiyo mantiki

Kwa guta hiyo gia unayoongelea ni kama ipe 4wd ambayo hata kwenye Kirikuu ipo na sio gia ya kutembelea all the time ni sehemu korofi tu ukimaliza unaitoa

Na pia unataka kusema guta hazichakai? mimi nimeshuhudia guta zinapiga kazi ndani ya mwaka zinakuwa spana mkononi

Specs tu zenyewe zinasema Hizi Kirikuu zenye engine ya 650cc zinatakiwa zisizidishe mzigo wa kg 350....Wakati hizi guta nyingi zenye 250cc ukomo ni kg 200, Lakino unakuta carry ama guta imebeba zaidi ya kg 800! sasa kwanini zisichoke

Kimsingi Carry ina uwezo zaidi
 
Nimeongeza chuma ya pili juzi mwendo ni TOYO gutta.Ya mwanzo ni cc250 na hii mpya ni cc200. Utofauti ni TOYO india na wahoo ni mchina.

KAZI ni kipimo cha UTU
View attachment 3003272
Tupe experience ya bei ya hiyo Toyo 250

Na kwanini umependelea Toyo na si Wanhoo wala Sinoray?
 
Bado sijapata hiyo mantiki

Kwa guta hiyo gia unayoongelea ni kama ipe 4wd ambayo hata kwenye Kirikuu ipo na sio gia ya kutembelea all the time ni sehemu korofi tu ukimaliza unaitoa

Na pia unataka kusema guta hazichakai? mimi nimeshuhudia guta zinapiga kazi ndani ya mwaka zinakuwa spana mkononi

Specs tu zenyewe zinasema Hizi Kirikuu zenye engine ya 650cc zinatakiwa zisizidishe mzigo wa kg 350....Wakati hizi guta nyingi zenye 250cc ukomo ni kg 200, Lakino unakuta carry ama guta imebeba zaidi ya kg 800! sasa kwanini zisichoke

Kimsingi Carry ina uwezo zaidi
Guta la 250cc linabeba mpaka tani 1.5,la 200cc ndo tani 1 kamili

Zaman guta za 200cc ziliandikwa max zibebe nusu tani
 
Kirikuu ni mfano wa gari mpasuko wa moyo, kwanza kirikuu ni dhambi 😂😂
Kirikuu hakibebi wamama watatu wakubwa!
 
Katika maisha yangu ya kijiwe nmeona guta ndo zinasanya zaidi kuliko hicho ki gari.
Nafikir sababu ni kama ifuatavyo;
1. Guta inaingia hata sehemu mbaya mfano kwenye shamba, porini ambako gari Kwa jinsi llivyo haliwezi maana guta ipo juu hichi ki gari kipo chini kinatitia.
2. Wateja wengi hawaogopi kufuata guta ili likambebe mzigo tofauti na hicho ki gari mteja akishaa kiona anaogopa Kwa kuhofia atakodi Kwa bei kubwa kikambebe mahindi yake shamba.
3. Guta inabeba mpaka kilo 1000 Tani 1 sawa na hichi ki gari lkn ulaji wa mafuta guta utapenda. Very economical.!!!
4. Matangenezo ya guta yapo chini hata mafund boda wakakurekebishia lkn pia hata malipo ya Kodi serikalini guta yapo chini na hawakamati hovyo ka gari.
5. Guta utaishi nalo miaka mingi tofauti na gari. Guta likidondok watu 2 mnainua na kazi inaendelea ila hicho ki gari baba unaenda kupaki juu ya mawe ka huna pesa mingi.

Ukitaka return nunua guta ila sio kama hako ulikoonesha hapo, chukua WANHOO 250 AU 300. Pia sinoray nzuri Ina tera kubwa zaidi na inapiga tipa.

Nina uziefu kiasi flani maana nmetoka kuwa mtoto wa kijiweni sana tu.!
Mkuu sijui bado upo Jf, ila shukrani sana, mnano mwishoni mwa December 2024 niliingia Daressalaam nikachukua Sinoray cc250 Q7, nimekaa nalo takribani mwaka 1 na miezi 5 majuzi nimeliuza, na jana nimenunua lingine naendelea na kazi

Hakika mkuu ulitoa maelezo kwa vile ulivyoweza lakini maelezo yako yalinipa mwanga mkubwa sana
 
Mkuu sijui bado upo Jf, ila shukrani sana, mnano mwishoni mwa December 2024 niliingia Daressalaam nikachukua Sinoray cc250 Q7, nimekaa nalo takribani mwaka 1 na miezi 5 majuzi nimeliuza, na jana nimenunua lingine naendelea na kazi

Hakika mkuu ulitoa maelezo kwa vile ulivyoweza lakini maelezo yako yalinipa mwanga mkubwa sana
Bado nipo, hongera mpambanaji.!
 
Back
Top Bottom