Katazo la upimaji wa mbolea Serikali mnatesa wakulima

kluger

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
2,093
1,894
Salaam,

Huu ni msimo wa kilimo hapa nchini kwa wakulima wakubwa na wadogo.
Serikali kupitia viongozi wake wakuu imekuwa ikihamisha utumiaji wa mbolea na uanzishwaji wa viwanda vya kutengeneza mbolea.
Kwangu mimi hili nimeliona limekaa kisisa sana kuliko uhalisia.

Kwa nini?

1. Ukweli ni kwamba wakulima walio wengi hawamudu kununua Mbolea hiyo kwa kiasi kikubwa Yaani kuanzia 50 KGs

2. Ujazo huo ni zaidi ya mahitaji ya wakulima walio wengi ambao ni karibia asilimia 75 ambao wanamiliki mashamba madogo madogo tu

3. Nguvu kubwa ya vikosi vya Askari vinapita duka hadi duka kudhiniti upimaji wa mbolea ni ishara ya maagizo ya kisiasa

4. Kwa nini viongozi mnakuwa kama mnaishi dunia nyingine, ongeeni na wakulima kufahamu hali halisi. Wabunge na madiwani mpo kimya kama hamlifahamu na kupitisha kanuni zinazotesa wananchi wa hali ya chini


Mapendekezo nini kifanyike.

1. Kabla ya kupiga marufuku ni vyema kufanya tafiti halisi na kufahamu hali halisi

2. Serikali elekezeni viwanda kufunga mbolea katika ujazo kuanzia kilo 2, kilo 5, kilo 10, kilo 25 na kilo 50, ili kila mkulima anunue mbolea kadri ya uhitaji wake na si kulazimisha ununuzi wa kiasi kikubwa cha mbolea ambacho hawahitaji

Cha kushangaza kuna muuzaji mmoja wa mbolea alijitolea kuandikisha kila mkulima anayekuja na kiasi anachohitaji ili ikitimia idadi fulani ya kilo anawapatia mfuko wakulima hao wakagawane pia alipigwa marufuku.

Sasa serikali kwa nini mnatukomoa wakulima???

Ni hayo tu, wahusika kama hili litawafikia boresheni hali hiyo, mbolea hazinunuliki ni hasara tu, jifunzeni kwa wenzetu wakenya na wengine wanaofanya vizuri kwa kilimo cha kutumia MBOLEA.
 
Nilienda duka la pembejeo kununua mbolea pamoja na dawa za kuulia wadudu, nilitaka kupimiwa kiasi cha 15kgs kwa ajili ya bustani yangu ya mboga mboga, muuzaji akaniambia mbolea inauzwa kwa mfuko, yaani 50kgs!! Nilishangaa sana. Hii serikali inafanya maamuzi ya ajabu sana.
 
Nilienda duka la pembejeo kununua mbolea pamoja na dawa za kuulia wadudu, nilitaka kupimiwa kiasi cha 15kgs kwa ajili ya bustani yangu ya mboga mboga, muuzaji akaniambia mbolea inauzwa kwa mfuko, yaani 50kgs!! Nilishangaa sana. Hii serikali inafanya maamuzi ya ajabu sana.

Kabisa mkuu yaani ni mambo ya ajabu sana, tena yanafanywa na wazee wasomi watoto wa wakulima
 
Nilienda duka la pembejeo kununua mbolea pamoja na dawa za kuulia wadudu, nilitaka kupimiwa kiasi cha 15kgs kwa ajili ya bustani yangu ya mboga mboga, muuzaji akaniambia mbolea inauzwa kwa mfuko, yaani 50kgs!! Nilishangaa sana. Hii serikali inafanya maamuzi ya ajabu sana.
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.
 
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.
Nimekuelewa mkuu
 
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.
Hapa na mimi nimeelewa, suruhisho ni viwanda kufungasha walau kuanzia kilo 5, 10, nk..
 
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.

Sasa kama hiyo ndiyo sababu hao viongozi hawana ufikiri wa kutumia Mamlaka zao kuamrisha viwanda kupima ujazo mdogo, mbona ni jambo rahisi kufikiri na kuamua hivyo?
 
Dukani kwangu mimi napimisha, mnunuzi akihitaji kidogokidogo namlisha yamini kwanza then anapata mzigo! Waziri wa Kilimo ni taahira! Serekale inafanya maamuzi mengi ya kipumbavu yasiyozingatia hali halisi!
 
Hata mimi nipo dar kariakoo tunapata mbolea ya kipima kama bangi .bora viwanda vielekezwe tupate kipimo cha 5kg
 
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.
Nilitaka nimjibu hivi mtoa post, lkn Nashukuru umemjibu vema.
 
Dukani kwangu mimi napimisha, mnunuzi akihitaji kidogokidogo namlisha yamini kwanza then anapata mzigo! Waziri wa Kilimo ni taahira! Serekale inafanya maamuzi mengi ya kipumbavu yasiyozingatia hali halisi!

Ni kweli kabisa mkuu, ungekuwa karibu nami duka lako lingenifaa sana
 
Hata mimi nipo dar kariakoo tunapata mbolea ya kipima kama bangi .bora viwanda vielekezwe tupate kipimo cha 5kg

Kabisa mkuu, sasa cha kushangaza jambo kama hili wao hawalioni wanalea matumbo tu
 
Hii si la kulaumu kwani kufungua mbolea kunapoteza sehemu kubwa ya virutubisho vyake. Mkulima akinunua hiyo mbolea ilifunguliwa muda mrefu anakuwa amenunua makapi ambayo hayatamupa matokeo anayotarajia. Kwa hiyo tusilaumu serikali bali ni kuwashauri viwanda wafungashe kwenye vipimo vinavyonunulika na wakulima wadogo.
Unazungumza kwa nadharia, si kwa vitendo mkuu!! Unasema imefunguliwa muda mrefu kwa vipi? Unafikri wauzaji wenyewe mataahira kwamba wanaiacha iko wazi tu? Iko hivi,, mfuko ukishanguliwa kwa mfano amekuja mtu anahitaji kilo 2 anapimiwa baada ya hapo mfuko unafungwa tena tightly hivyo haukai wazi. Maana ukisema hivyo hata wakulima wanaonunua mfuko mzima kwenda nao mjumbani basi wanatumia makapi, kwa vile utakuta mkulima kaenda kuweka mbolea leo mfuko unabaki anarudi nayo nyumbani ataitumia tena baadaye! Kinachotakiwa hapa siyo katazo, bali ni elimu ya jinsi ya kutumia hiyo mbolea kwa wauzaji na wanunuzi wenyewe! Volatilization haiwezi ikawa inatokea kwa mwuzaji tu bila kumhusisha na mnunuzi mwenyewe! Hawa wadau wakifundishwa matumizi sahihi hilo tatizo haliwezi likawapo. Tunaleta makatazo ya kipumbavu bila kuzingatia hali halisi, majitu yamekalia kulea vitambi maofisini halafu yanakuja kukurupuka na maagizo ya kipumbavu!! Hilo wazo la vifungashio vidogo ni sahihi, lakini kabla halijatekelezwa watu waruhusiwe kuuza kidogo kidogo kwa bei yenye unafuu. Hapa wangesema wakulima wanaibiwa hapo ningewaunga mkono, maana unakuta mbolea inauzwa 1,500 = 2,000/= per kilo hapo mkulima amelizwa!!
 
Viongozi wa nchi hii badala ya kutumia shule zao kutatua na kutafuta suluhu kwa faida ya wananchi wao kazi yao ni kutoa tu matamko na makatazo
 
Back
Top Bottom