Katavi: Baadhi ya Shule hali ya kuripoti Wanafunzi hairidhishi Mwaka 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko ameagiza watendaji wote wa Mitaa na Vitongoji wakishirikiana na maafisa elimu kuhakikisha wanatoka maofisini na badala yake wawatafute Wanafunzi wote wanaopaswa kuwa shule ili kuendelea na masomo.

Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kufanya ziara katika Halimashauri ya Wilaya ya Tanganyika ikiwa ni katika kuangalia hali ya Wanafunzi kuripoti shule ambapo amekuta hali hairidhishi, hivyo ikamlazimu kuagiza Watendaji wa Mitaa na Vitongoji kwa kushirikiana na Maafisa Elimu kuhakikisha Wanafunzi wote wanaopaswa kuwa darasani wanafika ili kuendelea na masomo.

Aidha, ameagiza Halmashauri zote mkoani humo kumpatia kila siku taarifa ya hali ya Wanafunzi kuripoti shule huku akisisitiza Wazazi na Walezi kuchangia chakula kwa ajili ya wanafunzi wawapo shule.

Naye, Halima Naison ambaye ni Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mpandandogo na Fredrick Kalele ambaye ni Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Ifukutwa wamesema mbali na idadi kutoridhisha lakini watajitahidi kushirikisha viongozi wa dini ili kuwapata wanafunzi hao huku Katibu Tawala wa Halmashauri ya Tanganyika, Lincolin Tamba akisisitiza Maafisa Elimu na Maafisa Tarafa kufuatilia Wanafunzi ambao hawajaripoti shule.
 
Hali ya uchumi kwa wazazi wengi kwa sasa ni ngumu mno!kununua vifaa vya shule ni changamoto,halafu utawasikia wanasiasa eti uchumi umekua, elimu ni bure na bla bla kibao
 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mwanamvua Mrindoko ameagiza watendaji wote wa Mitaa na Vitongoji wakishirikiana na maafisa elimu kuhakikisha wanatoka maofisini na badala yake wawatafute Wanafunzi wote wanaopaswa kuwa shule ili kuendelea na masomo.

Kauli hiyo ameitoa mara baada ya kufanya ziara katika Halimashauri ya Wilaya ya Tanganyika ikiwa ni katika kuangalia hali ya Wanafunzi kuripoti shule ambapo amekuta hali hairidhishi, hivyo ikamlazimu kuagiza Watendaji wa Mitaa na Vitongoji kwa kushirikiana na Maafisa Elimu kuhakikisha Wanafunzi wote wanaopaswa kuwa darasani wanafika ili kuendelea na masomo.

Aidha, ameagiza Halmashauri zote mkoani humo kumpatia kila siku taarifa ya hali ya Wanafunzi kuripoti shule huku akisisitiza Wazazi na Walezi kuchangia chakula kwa ajili ya wanafunzi wawapo shule.

Naye, Halima Naison ambaye ni Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Mpandandogo na Fredrick Kalele ambaye ni Mwalimu Mkuu Shule ya Msingi Ifukutwa wamesema mbali na idadi kutoridhisha lakini watajitahidi kushirikisha viongozi wa dini ili kuwapata wanafunzi hao huku Katibu Tawala wa Halmashauri ya Tanganyika, Lincolin Tamba akisisitiza Maafisa Elimu na Maafisa Tarafa kufuatilia Wanafunzi ambao hawajaripoti shule.
Viongozi wa dini wanahusikaje kiongozi?
 
Back
Top Bottom