figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,492
- 54,895
Jeshi la Polisi Mkoani Katavi linamsaka Hamim Mussa na wenzake wawili wakituhumiwa kuwanywesha wananchi maji yanayodaiwa kuwa ya Baraka katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa uliopo Mpanda Mjini na kusababisha kifo cha mtu mmoja na mwingine kulazwa.
Kaimu Kamanda wa Jeshi hilo Mkoani Katavi Benedict Mapugila ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Mpanda Radio kuhusu tukio hilo ambapo mtuhumiwa amesemekana kuwa ametoroka mara baada ya kutokea kwa madhara hayo.
Mmoja wa manusra wa katika tukio hilo Kulusum Shabani pamoja na mambo mengine amesema tukio hilo limetokea Jumamosi ya Oktba 6 mwaka huu baada kunywa maji hayo kwa maelekezo ya Hamim Mussa anayetajwa kuwa ni Mganga kutoka Mkoani Mwanza.
Hata hivyo Uongozi wa Hospitali ya wilaya ya Mpanda umesema haujapata taarifa za tukio hilo kwa kuwa waathiriwa wa tukio hilo walikuwa wamelazwa katika Zahanati ya Afya iliyopo Mpanda Mjini.
Kwa mjibu wa Shehe wa Mkoa wa Katavi Mwalimu Ally Hussein amesema wamelipokea tukio hilo kwa maskitiko na kulikuwa kuna watu 3 kati yao wanawake wawili waliokuwa wakishughulikia matibabu hayo ambao ndio wanaosakwa na jeshi la polisi baada ya kutokomea kusikojulikana.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt.Omary Sukari amesema atatoa taarifa kamili mara baada ya kupata ripoti ya tukio hilo.
Kaimu Kamanda wa Jeshi hilo Mkoani Katavi Benedict Mapugila ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na Mpanda Radio kuhusu tukio hilo ambapo mtuhumiwa amesemekana kuwa ametoroka mara baada ya kutokea kwa madhara hayo.
Mmoja wa manusra wa katika tukio hilo Kulusum Shabani pamoja na mambo mengine amesema tukio hilo limetokea Jumamosi ya Oktba 6 mwaka huu baada kunywa maji hayo kwa maelekezo ya Hamim Mussa anayetajwa kuwa ni Mganga kutoka Mkoani Mwanza.
Hata hivyo Uongozi wa Hospitali ya wilaya ya Mpanda umesema haujapata taarifa za tukio hilo kwa kuwa waathiriwa wa tukio hilo walikuwa wamelazwa katika Zahanati ya Afya iliyopo Mpanda Mjini.
Kwa mjibu wa Shehe wa Mkoa wa Katavi Mwalimu Ally Hussein amesema wamelipokea tukio hilo kwa maskitiko na kulikuwa kuna watu 3 kati yao wanawake wawili waliokuwa wakishughulikia matibabu hayo ambao ndio wanaosakwa na jeshi la polisi baada ya kutokomea kusikojulikana.
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt.Omary Sukari amesema atatoa taarifa kamili mara baada ya kupata ripoti ya tukio hilo.