Kashfa ya Uzinzi: Lissu amsafisha Mbowe

Kashfa ya Uzinzi: Lissu amsafisha Mbowe

Status
Not open for further replies.
soma vzr historia ujue kwa nini mke wa kwanza wa Madiba alimuacha na kuondoka, ukikosa kitabu tafuta movie ya Idris Elba Long walk to freedom utajua usikurupuke kumshambulia Lissu hapa...

take note sitetei ujinga wa mwenyekiti wao nakusahihisha kwenye historia

Kwani Madiba baada ya kuwa mtu mzima alijivunia huo ujinga?,


kumbuka kwa wakati huo Madiba hakuwa mwenyekiti wa ANC na wala hakuwa na role kubwa sana katika siasa za south Africa kwa wakati huo.

Ninachofahamu ni kwamba baada ya kutoka jela madiba alikiri kwamba jela ilimfanya areflect maisha yake ya zamani na kujuta kwa yale aliyoyafanya yakaumiza watu wengine. bila shaka miongoni mwa walioumizwa naye ni mke wake wa kwanza. JE MWENYEKITI MBOWE ANAHUZUNISHWA NA MATENDO ANAYOYAFANYA YANAYOMUUMIZA MKE WAKE HIVI SASA?.

Ni heri tukamwambia Mwenyekiti ajirekebishe kuliko kudismiss matendo yake. KAMA HAJALI FEELINGS ZA MTU ALIYEONDOKA KWA BABA NA MAMA YAKE AKAJA KWAKE , JE ATAJALI VIPI FEELINGS ZA RAIA ASIOWAJUA WANAOISHI KWA MLO MMOJA TU?
 
Ili kutenda haki inabidi wote tukubali kufuata maandishi ya dini na tuiache katiba. Katiba haisemi swala la ngono ya hiari ila inakataza kudhalilisha na kubaka wanawake na watoto. Ngono ya hiari haijatajwa kwenye katiba.

Kikristu biblia imekataza zinaaa, uzinzi, uasherati, kutamani mwanamke wa mtu na ngono kabla ya ndoa. Tukifuata biblia na tukatumia std za biblia wote wenye mimba bila ndoa hawafai kuwa viongozi kwani wanatenda dhambi, wote wanaoishi na mahawara hawafai, wote wenye mke zaidi ya mmoja hawafai kbisa kwani wanavunja mafundisho ya biblia.

Tukitumia biblia kama wengi wanavyotaka spika hafai kwani naye yupo tu hajaolewa na ana mtoto/au watoto. Mle bungeni kuna ngono mseto nyingi sana. Raisi ndio usiseme waumini wanachagua vioja havipendezi mbele ya mwenyezi Mungu ni machukizo.

Biblia inakata kusema uongo, wizi, kuuwa, kuzini, kutamani mali za watu. Nchi nyingi kama Iran ziliamua kufuata sheria za kidini kuongoza nchi na nchi nyingi za magharibi zilitoloha biblia kama chanzo chake cha maadili. Je Tanzania maadili yetu ni kitu gani tunafuata? Tujue ili tuweze kuwahukumu hawa viongozi kwa haki.

Naona wengi hapa wanatumia biblia kuhukumu, Je wenye dini nyingine wanasemaje?

Kufananisha ubakaji wa Pro Juma kapuya na ngono mseto hiari ni kosa kubwa. Kisheria hakuna kosa kama msichana ni zaidi ya miaka 18 na amekubali kula uroda na mtu yeyote. Ila kidini inakataza kabisa kwamba yeyote anayetafuna mwenzake kabla ya ndoa anatenda dhambi. Mwigulu alitenda dhambi ya uasherati kutemnbea na mke wa mtu. Wapo wengi sana hasa dodoma ni waasherati. Ila kwasababu ushahidi wetu wa ni wa mazingira biblia inakaza kuhukumu hasa kwa kufikirika.

Maswala ya ngono ni magumu sana. Ndoa nyingi zimeshikiliwa na ndoano. Nafikiri inabidi tuamue tuachane na swala la bei ya umeme, maisha magumu, ukosefu wa ajira, katiba mpya, ubovu wa barabara , huduma duni za jamii kama elimu, afya nk tujiketi kwenye ngono za viongozi hilo ndilo liwe sababu zetu kubwa za maendeleo.(hapo itabidi wengi tubaki nje) . Hii siasa za personal attack haziwezi kutusaidia sana. Tukiangalia ukweli swala la ngono mseto ni ugonjwa mkubwa sana TZ, karibu kila mwenye kajimshahara ana hawara mjini. Kila mwenye cheo analea watoto kadhaa nje ya ndoa, na kila mwanasiasa ana mchumba bungeni kati ya mama, dada, na bibi zetu waliopo. Kati ya wabunge kumi wa kike saba wana ngono mseto ndani ya bune, kati ya mawaziri kumi wa kike kumi wametoa ngono kupata vyeo kati ya wakurugenzi kumi wa kike kumi wanagawa ngono kwa waliowateuwa au kuwapendekeza.

Wanaume asilimia 95 waliopo dodoma wana nyumba ndogo zaidi ya moja. Ngono mseto ni ugonjwa mkubwa sana Tanzania. Mkuu wa kaya ukimchunguza sana utalia machozi mengi.

NINASEMA NGONO NJE YA NDOA NI DHAMBI, TALAKA NI CHUKIZO MBELE YA MUNGU NA NI DHAMBI KILA ATOAYE TALAKA NA KUOA TENA ANATENDA DHAMBI YA UASHERATI.
 
soma vzr historia ujue kwa nini mke wa kwanza wa Madiba alimuacha na kuondoka, ukikosa kitabu tafuta movie ya Idris Elba Long walk to freedom utajua usikurupuke kumshambulia Lissu hapa...

take note sitetei ujinga wa mwenyekiti wao nakusahihisha kwenye historia
Acha uongo, mandela ndiye aliyemuacha Evelyn .... according to court papers not movies.
Usimfananishe na mboye.
Na siyo kwamba Lissu amechemka tu, bali hata kitendo cha kwenda Global Publishers kimemuondoa heshima toka kwangu.
 
Kwani Madiba baada ya kuwa mtu mzima alijivunia huo ujinga?,


kumbuka kwa wakati huo Madiba hakuwa mwenyekiti wa ANC na wala hakuwa na role kubwa sana katika siasa za south Africa kwa wakati huo.

Ninachofahamu ni kwamba baada ya kutoka jela madiba alikiri kwamba jela ilimfanya areflect maisha yake ya zamani na kujuta kwa yale aliyoyafanya yakaumiza watu wengine. bila shaka miongoni mwa walioumizwa naye ni mke wake wa kwanza. JE MWENYEKITI MBOWE ANAHUZUNISHWA NA MATENDO ANAYOYAFANYA YANAYOMUUMIZA MKE WAKE HIVI SASA?.

Ni heri tukamwambia Mwenyekiti ajirekebishe kuliko kudismiss matendo yake. KAMA HAJALI FEELINGS ZA MTU ALIYEONDOKA KWA BABA NA MAMA YAKE AKAJA KWAKE , JE ATAJALI VIPI FEELINGS ZA RAIA ASIOWAJUA WANAOISHI
KWA MLO MMOJA TU?


Unajua kisa cha Babu Seya kuozea jela?...

Unajua kilichomkuta Naibu katibu mkuu wa ccm Igunga?

Vipi kuhusu Prof. wa ccm Alhaji Juma K.?

Vipi kuhusu mgombea Urais mtarajiwa EL wa ccm na Matrida B.
 
hivi kikwete hana nyumba ndogo na kama anayo naye aitweje?kama hakuna ushahidi hao wanaosema mbowe alikuwa na mukya aliwabeba wote?maana naona watu wanasema nusunusu.
 
Bila shaka ninyi mnaomshambulia Mh. Mbowe ni watakatifu sana na kama ivyo ndivyo mlivyo nasema Mbarikiwe sana lkn kama sivyo Mlaaniwe sana.

Someni Biblia...Yohana8:7
Asiyekuwa na dhambi na awe wa kwanza kurusha Jiwe.
 
unajua kisa cha babu seya kuozea jela?...

Unajua kilichomkuta naibu katibu mkuu wa ccm igunga?

Vipi kuhusu prof. Wa ccm alhaji juma k.?

Vipi kuhusu mgombea urais mtarajiwa el wa ccm na matrida b.

viongozi wa chadema ni lazima wajitofautishe na viongozi wa ccm
 
Nmekua Mfuatiliaji Wa Siasa Za Tz Kupata Uongoz Tanzania Watu Hufanya Sherehe Wanapongezana Waksema 2meula, Hii K2 Huwa Inanishangaza Sana Huwa Siishii Hapo Njoo Dodoma Sasa Kpnd Cha Bunge Waheshmiwa Utawakuta Wanakesha Na Mabinti Wabich Kwa Wakav Club84 Wanazin Mno Sasa Yamekuja Ya Mbowe Mwigulu Kuzn Na Mke Wa M2 Jaman Viongz Ninyi Ni Role Model Acheni Bwana Na Ham2fai
 
Nmekua Mfuatiliaji Wa Siasa Za Tz Kupata Uongoz Tanzania Watu Hufanya Sherehe Wanapongezana Waksema 2meula, Hii K2 Huwa Inanishangaza Sana Huwa Siishii Hapo Njoo Dodoma Sasa Kpnd Cha Bunge Waheshmiwa Utawakuta Wanakesha Na Mabinti Wabich Kwa Wakav Club84 Wanazin Mno Sasa Yamekuja Ya Mbowe Mwigulu Kuzn Na Mke Wa M2 Jaman Viongz Ninyi Ni Role Model Acheni Bwana Na Ham2fai

rubbish
usiandike ki Facebook hapa
 
sawa ndio maana Madiba na Clinton wanaheshimiwa pamoja na kuwa na madhaifu yao ya kibinadamu.

Niko pamoja na wewe, Ila pamoja na mazuri ya clinton jamii ya kimarekani haikumpa free ride katika ishu ya Monica, hawakumuacha tu kwa hoja ya "maisha binafsi", tofauti na sisi tunavyojaribu kufanya kwa viongozi wetu wanaofanya hayo
 
Hivi, kama ndoa ni public (which is not), tendo la ndoa nalo je?

Mkuu tukiruhusu hawa jamaa watupeleke huko itafika mahala watatuambia kiongozi asipomrizisha mkewe unyumba basi hafai. Tunataka mpiga goli tano kwenda mbele. Hapo ndio utakapo ona biashara ya viagra kwa wataka uongozi itakapo shika kasi.
 
weka na video yenyewe ndo hii MziziMkavu



Ojuku Abraham na Jelard Lucas


KATIKA kile kinachoonekana kama kumsafisha Mwenyekiti wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe dhidi ya kashfa ya uzinzi inayomuandama.

Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tindu Lissu amesema suala hilo ni maisha binafsi ya mtu, ambayo hayawezi kuhusishwa na wadhifa wake kwa namna yoyote.


Akizungumza katika mahojiano maalum ndani ya chumba cha habari cha Global Publishers Ltd, Bamaga, Mwenge jijini Dar es Salaam juzi, Lissu alisema kwa kadiri anavyofahamu, suala hilo ni binafsi linalopaswa kuachwa chumbani, kwa sababu kama litahusishwa na nafasi yake, ni sawa na kukubali kuwa mzee Nelson Mandela wa Afrika Kusini si lolote wala chochote.

"Maisha ya kimapenzi ya mzee Mandela yalikuwa ya ukakasi, kwa maana hiyo unataka tuseme kuwa kwa sababu hiyo, mzee huyu hakuwa kiongozi bora, unataka tuseme Bill Clinton wa Marekani hakuwa kiongozi bora kwa sababu tu alipata kashfa katika moja ya makorido ya Ikulu ya White House? Mimi nadhani haya mambo kama yapo au hayapo, hayahusiani na uwezo wa mtu kiuongozi, ni mambo ya chumbani yanayopaswa kuachwa huko," alisema Lissu.


Lissu alikuwa akirejea baadhi ya sababu zilizosababisha mgogoro kati ya chama chake na Naibu Katibu Mkuu wao aliyetimuliwa, Zitto Kabwe, anayedaiwa kushiriki kuandaa waraka wenye nia ovu, ambao pamoja na mambo mengine, ulitaka kufanyika kwa mabadiliko ya viongozi wa juu, akiwemo Mwenyekiti wa Taifa, kwa kudaiwa kuwa na elimu ndogo pamoja na kukosa uaminifu katika ndoa yake.

Aidha, hivi karibuni wakati wa kikao kilichomalizika cha Bunge mjini Dodoma, Freeman Mbowe alidaiwa kuvuruga ziara ya mbunge mmoja mwanamke (wa viti maalum) wa chama chake aliyekuwa katika ziara ya kibunge nje ya nchi, na badala yake kumtaka kuungana sehemu alipokuwepo.

Mbunge huyo wa Singida Mashariki, licha ya kukiri kuwepo kwa mgogoro unaokitikisa chama chao, lakini alisema hatimaye Chadema itashinda na kubakia imara na akasisitiza kuwa mwavuli wa mahakama alionao Zito ukiondoka, watamtimua.



Chanzo: LISSU AMSAFISHA MBOWE - Global Publishers
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tukiruhusu hawa jamaa watupeleke huko itafika mahala watatuambia kiongozi asipomrizisha mkewe unyumba basi hafai. Tunataka mpiga goli tano kwenda mbele. Hapo ndio utakapo ona biashara ya viagra kwa wataka uongozi itakapo shika kasi.

Mambo ya kinyumba, uzinzi, na mengine kama hayo sisi wengine hayatuhusu. Asiyeelewa hilo ni duanzi tu.

Wewe umcheat mke mimi kiniume nini? Hainihusu hata kidogo.
 
Viongozi wa CHADEMA ni majanga tupu.

Kwa hiyo kumbe Mh. Mbowe ni mzinzi kwa maana nyingine, tuhuma hizi ni za kweli.

Sasa kama maswala ya Uzinzi ni private affairs. Vipi hili swala la kupewa millions pesa za Tanzania na wale wale kila mara alikuwa akipanda kwenye majukwaa alikuwa anawaita mafisadi.

Pesa za huyu kada wa CCM alizochukua nazo ni private affairs

View attachment 132573

Tunaomba tufahamu mipaka ya private affairs nchini

Kama ameweza kuijibu hoja ya uzinzi, kwa nini hakutaka kuijibu hoja ya "double agent" kwa maana kuwa, mchana ni mpiga vita mafisadi na usiku ni mpokea pesa za mafisadi
Wewe unaweza kununuliwa kkukiwa mchana kweupe kwa kutokuwa na kumbukumbu au kwa uvivu wako wa kutofuatilia mambo kwa ufupi tu kwamba Rostam Aziz mwenyewe katamka kwamba hajawahi kuwapa Chadema wala mtu aaitwae Mbowe hela yoyote na pia kaongeza kwa kusema jamani niacheni nimeachana na siasa uchwara na sasa naomba mniache nitulie na Nimrod Mkono kasema hajawahi kumpa Freeman Mbowe pesa yoyote na Chadema yake sso mkuu nategemea utakuwa umenielewa na kama baado basi utaelewa KESHO.Kuhusu Uzinzi unaoongelewa ni kwamba nikukosa cha kuongea ndio maana nikasema tuachane na mambo binafsi kwani hakuna mwenye uhakika wa mia kwa mia kama walilala pamoja yeye na Mungu wao ndio anajua na huyo aliyemnyooshea mwenzake kidole si alishikwa UGONI live na mke wa kada mwenzake.Hapa cha muhimu ni kuongelea mambo yanayotutesa kwa maisha yetu ya kila siku na sio mambo ya watu binafsi kwani sote hatujaawaona tunaambiwa tu lakini mambo ya kupanda kwa bei za vyakula,umeme,ukosefu wa maji nk ambavyo tunaaviona na kutuumiza tunaviacha
 
Kama thread hii inavyokimbia tungekuwa tunajadili masuala ya kupanda kwa umeme ingekuwa vizuri lakini kuacha matatizo tuliyonayo tukajadili ujinga tunaonekana wote hatuna maana hivi akiletwa Mboe na Kapuya wakasema ambae hajawai kuzini awe wa kwanza kuwapiga mawe si wote tutakimbia hii nchi ina matatizo mengi ya kujadili tunashusha ili jukwaa la wasomi.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom