Bongolander
How in the world the private security company conduct check up in the airport. Tanzanian is dead, and trust me i'm not responsible for the funeral.
jamani naomba mpiganaji moja, ambaye ana active network na watu wa bandari afuatilie swala hili pale Bandari,kufahamu ni nini kinaendelea hususan masuala ya ajira,halafu atupe data kamili.
nasikia uchungu sana kwa sababu ni juzi juzi tu walitangaza kazi nyingi sana na mimi niliomba lakini mpaka leo kimya kabisa, miezi kama miwili imepita,isije kuwa ni hako kamchezo kao hako ka kifisadi.
Bongolander
How in the world the private security company conduct check up in the airport. Tanzanian is dead, and trust me i'm not responsible for the funeral.
hii kesi inaweza kuchukua miaka 2
na hawa jamaa hawatolipwa kitu
sasa hapo ndipo mtakapooona legal system yetu iliyooza
Baada ya kulalamikiwa tangu enzi za Mkapa, Bandari ya DAR walijidai watarekebisha na watarahisisha utaratibu wa kutoa mizigo
Sasa hivi unaambiwa kuwa hali imezidi kuwa mbaya. Yaani Meli ikishashusha makontena Dar inaelekea Mombasa basi wewe unaweza kutoa Contena au LORI lako kule Mombasa kwa chini ya masaa 12 tuu wakati DAR kuna UHAKIKA wa mizigo kukwama kwa MIEZI 4 mpaka 6
Sasa nishachoka kuwa mzalendo mfuata bendera
Nawashauri ndugu zanguni, kama muna Mizigo yenu au Magari yenu basi maneno MOMBASA
Na suala lingine ni la NUMBER PLATE registration
Hivi kama Tanzania ni nchi moja kwa nini Gari ziwe na number plate za ZANZIBAR? kwa faida ya nani? na kwa nini mtu ulipie kuwa na number plate za Zanzibar wakati nayo ni Tanzania? jE UNAPATA MATATIZO KUTOA MAGARI YAKO DAR?
Solution: SHUSHA GARI ZAKO ZANZIBAR achana na DAR kule kuna wazimu mtupu
CARGO AIRPORT:
Kule nako hali ni mbaya zaidi kuliko na solution za kule sizijui ila najua kuwa ukishusha ile moniitor ya APPLE COMPUTER basi jiandae kuambiwa kuwa NI KIFAA CHA SINEMA hivyo utatozwa kodi ya TV
ndio hali hiyo huko Nyumbani mnakopigiwa makelele muende kupeleka Investments
Wewe muongo..hawezi kushindwa kutoa gari for 2 months..au hana hela ya kulipa ushuru
Tuna uhakika wa kuwa na bandari mbili mpya na za kisasa kabisa, moja tunaiweka Moshi na Moja tunaiweka Mbeya. Oooopsss, huko hakuna bahari.
Bwagamoyo na Mtwara.
Bandari ya Dar tutaiwacha iwe ya majahazi tu.
Ndugu zangu katika yote yanayokera Tanzania, msisahau uwanja wa ndege. Kwenye viwanja vyote vya ndehe nilivyowahi kupitia uwanja wa ndege wa Tanzania ni karaha sana, hasa ukiwa mtanzania mweusi.
Kuna kampuni inayoitwa ultimate security ambayo kazi yake ni kufanya kazi za ulinzi wa majengo, lakini wameingizwa airport wanalofanya ni kunyanyasa tu watanzania weusi. Akipita mtanzania mhindi au mzungu hawamsumbui, kwa sababu kwanza kiingereza wanashindwa kuongea. Kisingizio chao wanasema eti wanataka kuhakikisha kuwa hakuna anayesafirisha dawa za kulevya, wakati wanaofanya kazi hiyo wanawalinda sana and they never go through cumbersome and humiliating procedures that others have to follow.
Nyumbani jamani kutazidi kuwa ovyo tu. Uzalendo unatushinda hata huku kunakoitwa kuna wabaguzi atleast ukiwa na passport na visa wanakuheshimu sana. Inasikitisha.
Kwa maamuzi haya tu ni vigumu kwa mambo kunyooka. KUnahitajika 'overhaul' ya mfumo mzima wa uendeshaji wa bandari maana ilishegeuswa kuwa ni kitegauchumi cha kukindi fulani cha watu. Kusimamishawatu wawili watatu wala haitasaidia sanaLets hope haya maamuzi ya Mwakyembe yatasidia kufanya mambo yanyoke
..........mpaka kero mkuu!dah!ingekuwa daladala,nshashuka mieYaani, this country bwana kila mahali matatizo tuuuuuuuu. Kila kukicha matatizo tuuuuuuuuu!Dead Dead Dead Dead!