Nadhani kuna haja ya kujua ni kwa kiasi gani bandari inaweza changia uchumi wa nchi hii.
Mkuu, Mh.Dr akijifunga kibwebwe akamshauri JK kwamba Wakurugezi karibu wote pale Wizarani wahamishiwe Wizara nyingine kabisa; bila kufanya hivyo watamkwamisha TU. Mkuu si rahisi Wizara hii ikawa inakuwa na matatizo miaka nenda rudi alafu mtu ukategemea miujiza kutoka kwa jamaa hao hao waliopewa dhamana ya kuiongoza, tunasahau kwamba Waziri ni Kiongozi wa muda kwenye Wizara lakini Wakurugenzi/watendaji niwa kudumu mpaka wastaafu, na mtu akikaa kwenye nafasi moja muda mrefu anajisahau sana na kufikili Wizara ni mali yake au ya ukoo.
Wakurugenzi wakuu wanao teuliwa kuongoza Agencies za Wizara hiyo wanakuwa vetted na Wizara yenyewe wakati mwingine watu wenye uwezo wanatupiliwa mbali badala yake wanateuliwa maswahiba wao tu - mifano tunayo; nikiona wanalalamika kwamba mashirika yao tanzu mambo hayaendi vizuri huwa nawashangaa sana.
Mkuu Bandari yetu ni HUB kwa nchi zinazo izunguka Tanzania, kwa kujibu swali lako bandari hii ina uwezo mkubwa kuchangia mapato makubwa kuliko sector nyingine hapa nchini, we sema tatizo letu ni ukosefu wa ubunifu na kutojali - wenzetu Wakenya ni mahili sana katika nyanja za bihashara, uwezi kuona wana-mix bihashara na starehe, alafu wana mbinu nyingi ya kushawishi wateja na kujitangaza, kwao mteja ni mfalme hiwe Bandarini, Mahotelini na katika nyanja za kitalii -sisi hilo hatuna! Hutujuhi jinsi ya ku-handle wateja, tunawajibu ovyo ovyo tu, njoo kesho njoo kesho-pale longroom ndio usiseme yaani hata mantiki ya kutumia komputa pale ni kama utani vile, wizi uliyo kubuhu pale bandarini siyo kwa magari tu hata makontena yanapotea kabisa au unakuta yamebomolewa na mali imekwisha chukuliwa na wezi - yaani wizi Tanzania umekithili.
Siku moja niliwahi kusafiri na Wacongo wanakwenda Zambia, mambo walio nieleza kuhusu Bandari yetu na usafirishaji wa mizigo kutumia TRAIN ulinifanya nilishikwe aibu sana kuhusu Taifa letu. Mwisho walisema kwa nini Bandari na TRAIN msiwape WAZUNGU au Wachina mkawapa mshahara mkubwa wakaendesha/kuongoza mashirika hayo kwa niaba ya Serikali yenu!!!! We sikiliza wageni mapendekezo wanayo toa - unafikili mimi kama Mtanzania nilijisikiaje?