Kashfa ya Ufisadi Bandari ya Dar

Kashfa ya Ufisadi Bandari ya Dar

GT,Mwanakijiji,

..labda bandari panatakiwa pafumuliwe kama walivyofanya wakati wanaanzisha TRA.

..au iundwe task-force kam kama ile ya Tume ya Jiji wapasafishe wakati utaratibu wa kuwa na mamlaka yenye ufanisi zaidi unafanyika.
 
GT,Mwanakijiji,

..labda bandari panatakiwa pafumuliwe kama walivyofanya wakati wanaanzisha TRA.

..au iundwe task-force kam kama ile ya Tume ya Jiji wapasafishe wakati utaratibu wa kuwa na mamlaka yenye ufanisi zaidi unafanyika.

JOK, wakiunda task force si kuna watu watakuwa wanapata ulaji?
 
Makontena kujaa pale bandarini ni ulaji wa hali ya juu wakuu wanajua na CCM wanapata mgao. Makontena yanayojaza yard ya bandari mengi ni yale ya transit ambayo huwezi kwenda kuyaweka kwenye yard ya nje ya bandari( amabayo hayakustahili kushushwa pale). Ila kwa kuwa haka kamchezo kanachezwa na wenye kampuni za meli, TICS na CCM ndo maana kameota mizizi. Dar Port sio transit port!!
Kwa kuwa kuna mizigo mingi ya ya kwenda ulaya, hasa madini toka DRC na Kahawa ya Burundi, meli zenye makontena ambayo yanakenda port zaidi ya Dar wanapunguza gharama kwa kuyashusha hapo Bandarini ili yaje yapakiwe na meli zingine yafikishwe kule yanakokwenda, then wao wanapakia mzigo ya kutoka DRC, Burundi na baadhi yetu sisi, kama Pamba, mbao, magogo nk. hivyo wanatengeneza kaela ka kueleweka kwa kuwa wanarudi na mzigo. Sasa hayo makontena kwa kuwa yanakuwa yanasubiri meli za kuyafikisha kule yanakokwenda, hayawezi kuondolewa pale yard Bandarini mpaka pale yatakapopata meli. Wakati huohuo wenye kampuni za meli wanakuwa wako tayari kulipa charge za kuyaweka pale hayo makontena na hii pesa wanayokula bila wasiawasi kwa kuwa haiko ndani ya mkataba.
Sasa meli zinazokuja zinakosa nafasi kwa kuwa kunakuwa hakuna mahali pa kuyapakulia, kwa lugha ingine yard inakuwa imejaa makontena ya transit.

Mkuu Kwa Taarifa tu bandari ya dar haipokei transhipment boxes za nchi nyingine, Mizigo yote inyosubiri meli ni ya Zanzibar na Tanga, msumbiji ambao mizigo ilkuwa inapita dar sasa inapita durbarn SA.Hivyo mizigo inayosubiri meli bandarini ni ya tanzania sababu inayofanya ijaye ni utendaji mbovu wa bandari Za Zanzibar na Tanga ambao wana uwezo wa kupakua konteiner 8-10 kwa shift ya maasaa nane.
 
Mwanakijiji said:
JOK, wakiunda task force si kuna watu watakuwa wanapata ulaji?

Mwanakijiji,

..hatuwezi kuwa na 0% ulaji, but we must keep on pushing to achieve that goal.

..kipaumbele chetu sasa hivi kiwe kuhakikisha kwamba kuna ufanisi ktk bandari zetu.

..TRA, bandari, reli, na barabara za kutoka nje ya nchi, zinategemeana kiufanisi.

..eneo moja likizembea basi mengine yanaathirika negatively.
 
Date::3/2/2009
Kikwete atangaza vita bandarini,wezi hatarini kupoteza kazi
Salim Said na Tumsifu Sanga
Mwananchi

RAIS Jakaya Kikwete amesema ana majina ya watu wa kitengo cha maktaba cha Bandari ya Dar es salaam wanaofanya ufisadi unaolikosesha taifa mamilioni ya fedha na kuahidi kuyakabidhi kwa wahusika ili washughulikiwe.

Kikwete alisema hayo jana baada ya kufanya ziara ya kushitukiza kwenye Bandari ya Dar es salaam kukagua utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa Januari 15 mwaka huu kwa wakuu wa Mamlaka ya Bandari (TPA).

Alisema kitengo cha maktaba kimekuwa kikifanya mchezo mchafu bandarini hapo kwa kushirikiana na wasafirishaji na kwamba, vibarua vya watu wa kitengo hicho viko hatarini.

“Waambieni watu wa kitengo cha maktaba kuwa mchezo wao unajulikana na orodha ya majina yao inajulikana, lakini bado kuwaumbua tu,” alisema Kikwete baada ya kumaliza ziara yake.

“Ndugu zangu sitawataja hadharani wala kwenye magazeti, bali nitakachofanya nitawaletea orodha ya majina, muwafukuze kazi. Kama wameshindwa kazi tutaleta watu wengine ambao wako tayari kufanya kazi kwa uaminifu.”

Alisema watu hao wamekuwa wakiwasiliana na wasafirishaji na kufanya ujanja wakati wa kujaza fomu za makontena yanayoingia nchini kwa kuandika mizigo tofauti na ile iliyomo ndani ya makontena hayo, ili yasipitishwe katika mashine ya uchunguzi (scanner) na hivyo kukwepa kulipa kodi kubwa.

Alisema mchezo huo hufanywa kwa makusudi ili kuwalaghai watu wa kitengo cha T. Scaner kutochunguza mizigo hiyo kwa mashine yao wakiamini kuwa hayana mzigo wa maana.

“Fomu imeandikwa ndani kuna mitumba, lakini kontena likikaguliwa unakuta magari ya kifahari. Kazi hii inawatajirisha wao na kulitia umasikini taifa letu,” alisema Kikwete.

“Tunahitaji scanner za kisasa ambazo zitakuwa na uwezo wa kuona hata chupa iliyomo ndani ya kontena.

“Lakini nashangaa mambo haya nayajua mimi, ninyi hamna habari. Sijui mnafanyaje kazi lakini fanyeni kazi kwa bidii na msifanyie mazoea.”

Ujanja wa kupitisha mizigo kwa njia ambayo hailipishwi ushuru unaolingana na thamani halisi, imesababisha kuwepo kwa mawakala wengi ambao husaidia mipango ya kutoa mizogo bandarini na kujipatia fedha nyingi ambazo zilitakiwa kuingia kwenye makasha ya serikali.

Utitiri wa makampuni ya uwakala huo ulipungua baada ya serikali ya awamu ya tatu kuanzisha utaratibu uliozitaka kampuni hizo kuweka dhamana ya Sh10 milioni kabla ya kuruhusiwa kufanya biashara, lakini sasa yamerudi kwa nguvu kubwa.

Kuhusu msongamano wa meli za mizigo, makontena na magari bandarini, Rais Kikwete alimuweka kiti moto mkurugenzi wa TPA, Efraem Mgawe kwa kumuhoji maswali ya papo kwa papo.

Mgawe alithibitisha kuwa tatizo la msongamano halijaondoka na kuchukua ahadi ya kulishughulikia kabla ya ziara nyingine ya rais ndani ya miezi miwili.

Rais alitaka kujua idadi ya kontena na magari ambayo yapo bandarini na ni kwa muda gani yamekaa hapo, swali ambalo Mgawe alionekana kutokuwa na jibu lake.

“Kama hujui, tunahitaji kutumia kompyuta katika kufanya kazi zetu hapa bandarini ili tunapohitaji takwimu kama hizi iwe ni rahisi... ukibonyeza kompyuta tu unazipata,” alisema Kikwete.

Katika yadi ya magari bandarini, rais alihoji magari ya wagonjwa (ambulance) yaliyopo, lakini kwa mara nyingine Mgawe alionekana kutokuwa na jibu, jambo ambalo lilionekana kumkera rais kiasi cha kusema: "Haiwezekani kwamba hujui.”

Baada ya kuona kuwa rais alikuwa amekasirika, Mgawe alijibu kuwa magari hayo ni ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada ya Elimu (Unesco).

“Pamoja na matatizo haya yote ya bandarini kutokuwa na maelezo ya kutosha... huu ni ulegevu wa watendaji au uzembe, lakini nikisema uzembe nitakuwa nimewatukana,” alisema.

Rais alisema amelizuia Shirika la Wakala wa Meli (Nasaco) kulipiga mnada eneo lao lililo bandarini hapo na kwamba amewataka waliuze kwa TPA ili ilitumie katika upanuzi na kupunguza msongamano wa magari na makontena.

“Kama kuna kesi na wanadaiwa, si mkilinunua watapata fedha ya kuwalipa hao wanaowadai? Lakini hata hivyo niachieni mimi nitalishughulikia kuhakikisha kuwa mnalipata,” aliahidi Kikwete.

Akitoa ripoti ya utendaji ya TPA kuhusu maagizo ya Rais Kikwete aliyoyatoa Januari 15, Mgawe alisema wamepandisha ushuru wa kuweka mizigo bandarini na kuwa makontena yote yaliyofikisha siku 21 yatapigwa mnada na kitengo cha forodha.

“Kwa awamu ya kwanza tutapiga mnada makontena 1,063 Machi 16 mwaka huu,” alisema Mgawe.

Alisema ufanisi umeongezeka kutokana na kupata magari manne mapya ya kupakulia mizigo (crane) na kwamba mawili yameshafungwa na kuanza tangu juzi na kwamba idadi ya meli nje ya bandari imepungua na kufikia meli 15 kutoka 23 ilivyokuwa Januari 26 mwaka huu.

“Pia kontena zimepungua... jana kulikuwa na kontena 8,322 kutoka kontena 10,504 zilizokuwepo bandarini Januari 26. Ufanisi gatini umeongezeka na Ticts wamefikia asilimia 80 ya lengo la kontena 1,000 kwa kipindi cha saa 24 wakati TPA imefikia wastani wa asilimia 75 ya lengo la kontena 200 kwa saa 24,” alisema.

Waziri wa Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa aliahidi kuwa atasimamia suala la kuunganisha mtandao wa kompyuta kutoka TPA hadi TRA ili kurahisisha kazi.
 
kikwete is very colloquial. Sipendi hizi habari za ziara za kushitukiza, however revealing they may be sold as. Sipendi habari za kumuuliza mtu anayeendesha shirika kubwa kama hili maswali ya hapo kwa papo, bila hata ya kumpa taarifa, this guy is not running a coffee shop.

Kama rais anataka kufanya kweli afanye kweli, kama alivyosema Scarface "You wanna shoot, shoot, don't talk" .Katika kusema kitengo cha maktaba kinafanya vibaya bila kuwataja majina watu, anawapaka matope woote wanaofanya kazi katika kitengo hicho, hata wale wasio makosa.Hii inaweza kuvunja morale. This is an all or nothing at all issue, kama unataka kuwataja wataje kikamilifu, vinginevyo kaa kimya, usiseme kwamba hutaki kuwaumbua kwani kwa kukitaja kitengo chao bila kuwataja majina umewaumbua wote, wanaohusika na wasiohusika.

Huyu rais kibogoyo kabisa, huyo Mgawe kamteua mwenyewe sasa anaona public opinion inamsuta anataka kummwaga.

Hivi Kikwete alivyomteua Assistant Port Manager, mtu mdogo sana na asiye uzoefu wa senior management, mtu ambaye hata kwenye board of directors meeting alikuwa hayumo, kwenda ku run hili shirika nyeti alitegemea nini?
 
Sasa kama raisi ana majina kwa nini wasikamatwe haraka na kupelekwa mahakamani?

Anasubiri nini?
 
kikwete is very colloquial. Sipendi hizi habari za ziara za kushitukiza, however revealing they may be sold as. Sipendi habari za kumuuliza mtu anayeendesha shirika kubwa kama hili maswali ya hapo kwa papo, bila hata ya kumpa taarifa, this guy is not running a coffee shop.

Kama rais anataka kufanya kweli afanye kweli, kama alivyosema Scarface "You wanna shoot, shoot, don't talk" .Katika kusema kitengo cha maktaba kinafanya vibaya bila kuwataja majina watu, anawapaka matope woote wanaofanya kazi katika kitengo hicho, hata wale wasio makosa.Hii inaweza kuvunja morale. This is an all or nothing at all issue, kama unataka kuwataja wataje kikamilifu, vinginevyo kaa kimya, usiseme kwamba hutaki kuwaumbua kwani kwa kukitaja kitengo chao bila kuwataja majina umewaumbua wote, wanaohusika na wasiohusika.

Huyu rais kibogoyo kabisa, huyo Mgawe kamteua mwenyewe sasa anaona public opinion inamsuta anataka kummwaga.

Hivi Kikwete alivyomteua Assistant Port Manager, mtu mdogo sana na asiye uzoefu wa senior management, mtu ambaye hata kwenye board of directors meeting alikuwa hayumo, kwenda ku run hili shirika nyeti alitegemea nini?

Hivi Mgawe alikuwa junior manager? Hivi waliokuwa senior wake na hawakupewa hiyo Position ni aki na nani
 
Kwani ile orodha ya wanaojihusisha na uingizaji wa madawa ya kulevya nchini iliishia wapi?
 
Hivi Mgawe alikuwa junior manager? Hivi waliokuwa senior wake na hawakupewa hiyo Position ni aki na nani

The entire board of directors wa THA, pamoja na watu wengine weengi tu waliokuwa katika ngazi ya ukurugenzi katika makampuni tofauti (Especially waliokwishakaa pale bandari na kupajua kama the Daus and Mbakilekis of this world).

My point ni kwamba wamemrusha huyu bwana ngazi nzima ya uongozi (from Assistant Port Manager to Director General) jamaa hajawahi hata kuwa director.

Now I am not against fasttracking talent when there is talent, lakini mtu mwenyewe inaonekana hawezi mikiki mikiki ya hiki kiti, na huwezi kubisha mtu akisema kuwa moja ya sababu inayoweza kuchangia hilo ni kwa sababu hana uzoefu wa uongozi wa juu, jamaa ametoka kuwa assistant wa meneja wa bandari ya Dar kwenda kuwa bosi wa bosi wake wa zamani ( boss wa director of Engineering ambaye ni boss wa Port Manager)

Lakini Kikwete mwenyewe hakuchaguliwa kwa merit, sasa utategemeaje yeye achague watu kwa merit? Na utategemeaje ufanisi katika system ambayo haiheshimu merit?

Kitu kinachonishangaza sio jinsi tunavyoshindwa, bali tunavyotegemea tusishindwe katika system tuliyoiweka sisi wenyewe.

Hili si la Kikwete peke yake kwa kuwa kilaza, bali kila Mtanzania aliyemchagua Kikwete ameshiriki by proxy.

Mtanzania kamchagua Kikwete kiongozi mbovu, Kikwete kwa sababu kiongozi mbovu hana mkakati, haheshimu merit, kaenda kumchagua a very junior and inexperienced port officer aende kuwa CEO .Granted matatizo ni mengi, na mengi wala si ya TPA, yanatoka huko TRA na TICTS, lakini sehemu yenye matatizo mengi kama hii kwa nini uongeze matatizo kwa kumchagua mtu ambaye hana uzoefu wala track record?
 
Huu si usanii wa uleule tu? Raisi kutumia resources zetu kutishiana nyau na mafisadi hairidhishi. Tulipaswa kusikia Raisi kawafukuza kazi na kuwafilisi kina fulani kwa vile walifanya hivi. Leo eti raisi anasema mkicheza nitapeleka orodha yenu kwa..... Raisi anaendashitaki kwa nani? Kikwete afnye kitu wengine waogope waache.
 
Hivi kikwete alitegemea director general afahamu wamiliki wa zaidi ya magari 8000 yaliyoko pale bandarini kwa majina? Yaani usanii mwingine hauna hata dili! Nashangaa naangalia tbc na mwandishi wa habari anashangaa mkuu wa bandari kutofahamu wanye zile ambulance. Wapapmbe wanaomzunguka rais ni mazuzu ndo maaana rais mwenyewe ni zuzu la kutupa
 
...this is unfair lakini mimi niko kule kule WE DARE TALK OPENLY

...BODI na MENEJIMENTI ya THA wanavyofanya kwa sababu wanamwogopa ROSTA,KARAMAGI ambao ni wadau wakubwa wa TICS. Usiku huuu nimehesabu MIGAWE au meli zilizojazana kule baharini na nimeishia 21...yaani zote zile zinashindwa kutia nanga kwa sababu hakuna nafasi..,huu ni UJUNGA,UZEMBE NA UFISADI wa hali ya juuu ya wafuatao:

...SHUKURU KAWAMBWA alishawaambia akina Mollel kama wameshindwa kazi basi serikali itaivunja bodi lakini nashangaa wakikaa kwenye vikao vyao vya unywaji wanamtukana eti waziri ana mambo ya kiswahili na anatafuta attention! wanayoyasema kuhusu JK ndio siwezi hata kusema humu.

al muhimu ni kuwa nilituma Kontena mwezi wa 11 toka Hanoi mwishoni mwa mwezi wa 11 na kilichotokea ni kuwa mpaka leo naambiwa bado meli haijapewa nafasi ya kuingia...to be fair wanaotuma magari dogo wao meli zao zinapata nafasi hivyo kama kuchelewa ni miezi miwili

...Unajua LUHIGO japo alikuwa ni mshenzi mshenzi na mla rushwa enzi zake lakini JAMAA KAZI ALIKUWA NAFANYA....i am not gonna knock him him down

...Inaniumz akuwa serikali imekosa pesa nyingi toka kwangu kwa sababu ya uzembe wa hao niliowataja kwa sababu wanaogopa kuwaambia TICS kuwa wamebreach contract yao na kazi wameshindwa WHY ? kwasababu zaidi wanamwogopa ROSTAM na kampuni yake...jambo ambalo Jakaya hana kinyongo in the wake of huu ufisadi left and right

...Suggestion yangu ni kuwa mindhali KIMEI wa CRDB au jule bosi wa TRA wanafanya kazi nzuri tuuu kwa nini JK asimuapoint mmojawao kwenda kuisort out THA? maana Mgawe na GENGE lake la MAFISANI naona wameshindwa kazi ...

Luhigo kafanya "ushenzi" gani na "kala rushwa" kivipi?

Umejuaje wanamuogopa Rostam kwa assessment ya tatizo la shirika through kuhesabu meli kutoka baharini kama mzamiaji wa "sauzi"? Au unahisi wanamuogopa tu Rostam kwa vile siku moja watamuhitaji kumwomba mkopo binafsi ka Mtikila? Do you have a clue or two about the setbacks of Harbors Authority management?

Kama kinachokuumiza ni Tanzania kukosa hizo kodi ni kwa nini ume suggest kwamba wakamtoe kiongozi wa Revenue Authority, ambae unaona anafanya kazi nzuri kule, wamlete Bandari? Sasa, kama kweli concern yako ni forodha inayokosekana, je ni wapi wanahitaji uongozi bora zaidi, wanaokusanya kodi Mamlaka ya Bandari au wanaohakikisha kodi za Mamlaka ya Bandarai na za nchi nzima zinakusanywa? Au kilichokuumiza ni kwamba kama ulivyosema mwenyewe "al muhimu ni kwamba nilituma kontena mwezi wa 11..." and all that yiddy yad? Uko well oriented kweli wewe?

Ukakimbia kuja JamiiForums kutangaza kuwa viongozi wote wa Mamlaka ya Bandari ni mafisadi na kudai wamba "we dare to talk openly," lakini unasema kuna ka siri umekabakiza moyoni kuhusu mambo ambayo kina Mollel wanamsema Kikwete! Ndio ume dare nini hapo? I mean, umekula wewe leo?

Makontena yanachelewesha kwa sababu hakuna nafasi halafu unaongeza "to be fair wanaotuma magari dogo wao meli zao zinapata nafasi..." Kwa hiyo, I guess magari madogo yanakuja kwenye viboxi na vi mitumbwi vidogo vidogo na hivyo vinaweza kuwa sqeezed through the crowded moors of the harbor, unlike magari makubwa kama yako, right? That's the only way that your assertion is gonna make sense here, no other way. I'll tell you what, why don't you put all these large cars and cargo you are importing in ports throughout the east coast of Africa, put them all in one leased aircraft and ship 'em or shove 'em, that way you won't have to hussle with these "washenzi...wala rushwa," it's quicker too, I'm sure your accountant will have told you that, might end up saving you time and money, big Kahuna.

Eti Luhigo alikuwa "mla rushwa" na "mshenzi", hapo hapo unasema "alikuwa akifanya kazi...i am not gonna knock him down"? Sasa hiyo siyo knock tayari? Au sielewi hiyo "knock down," what you mean "knock down" anyway, I mean, that right there is a knock already, a criticism, if that's what you mean by "knock down."

I mean, I don't know whether it's the drug you're taking or the drug you need to be taking, but do something!
 
Acheni kumzungumzia babake mtu nyie....shauri yenu mwenyewe arudi hapa...mtaipata
 
GT,
bandarini panahitaji DG mtoto wa mjini aliyeoa mwanamke aliyechezwa.
 
Hivi kikwete alitegemea director general afahamu wamiliki wa zaidi ya magari 8000 yaliyoko pale bandarini kwa majina? Yaani usanii mwingine hauna hata dili! Nashangaa naangalia tbc na mwandishi wa habari anashangaa mkuu wa bandari kutofahamu wanye zile ambulance. Wapapmbe wanaomzunguka rais ni mazuzu ndo maaana rais mwenyewe ni zuzu la kutupa

Si unajua mfalme hata akitembea uchi wapambe watampongeza kwa kuchagua suti nzuri?

Yaani kuna sehemu nyingine Kikwete anataka kuuchanganya Unyerere/Sokoine/Mwinyi/Mrema katika kikombe kimoja halafu anatokea kituko kikubwa kuliko the worst aspects of all these people.
 
Katika suala la NSSF na vifo Tabora ulitetea uwezo mkubwa wa Dr. Dau kiutendaji. Nakupa wewe benefit of the doubt kwa sababu hata Rais inaonekana anaamini hivyo.

Tofauti yangu na wewe kuhusu Dr Dau haikuanzia kwenye vifo vya Tabora bali vilianza kwenye DR MASAU na hospitali ya THI ambako uliamua deliberately kupotosha ukweli juu ya mkataba wake na NSSF

Nilitetea na bado natetea uwezo wa kazi wa Dr Dau kwa sababu niko on the ground na mifano hai nimeiona hapa Dar na mikoani...mfano nyumba za polisi Keko na University kule Dodoma,kesho Daraja etc..na uwezo huu si mimi tuu bali ni mpaka Rais pia

Sasa kwa kadiri unavyomjua na kutokana na ukweli kwamba alishakuwa Bandari, unafikiri ni mtu ambaye anaweza kuleta uongozi unaohitajika sana (hii ni pamoja na kupata bodi mpya of course)?
tafadhali rudia jibu langu hapo juuu...
Kama huoni yeye ana uwezo wa kuinua Bandari na kuwa ni bora aendelee kubakia NSSF unafikiri ni nani mwingine ambaye unaweza kumpendekeza kushika nafasi hiyo hasa kutokana na matatizo ya Bandari uliyoyaonesha? Ungempendekeza nani?
Mjomba tuko watu milioni 40 wapo watu wenye uwezo mkubwa sana kuliko Dau ambao wanaweza kuirekebisha THA kuliko yeye...mmoja wapo ni huyo Kitilya wa TRA,Malingila wa Brealla, Kimei wa CRDB, Ndullu wa BOT na wengineo...
 
Hivi kazi ya Rais wa Tanzania ni kupita kila nyumba na kukagua kama imefagiliwa? Inanikumbusha O-level wakati headmaster anapita madarasani usiku kuona kama tupo prep. na tunasoma.

Guys, this is just beyond my imaginations. I thought the Prez. is Commander-In-Chief.

Hivi kweli unaweza kudekeza watu na uwajibikaji wao wakati serikali inakosa mamilioni?

Hao watendaji wabovu bado unawaambia kuwa utawatangaza utafirkiri ni ngoma ya kienyeji?

Be serious for God sake!
 
Back
Top Bottom