Ndo alivyotumwa na wapiga kura wake?
naafiki hoja hii,viti maalum ni mzigo kwa nchi,wabunge wa kuchaguliwa wanatosha kutuwakilisha.kuna vitimaalum mwingine alitaka wm asiulizwe maswali ya papo kwa papo kwa kuwa yanamdhalilisha yeye na serikali. Wanaharakati viondoeni vitimaalum bungeni. Ni aibu. Ni gharama za bure.
Kuna vitimaalum mwingine alitaka WM asiulizwe maswali ya papo kwa papo kwa kuwa yanamdhalilisha yeye na serikali. Wanaharakati viondoeni vitimaalum Bungeni. Ni aibu. Ni gharama za bure.
Wana jamvi,
Mbumbe wa kuteuliwa CCM Munda Tambwe Abdallah ameshauri Watanzania kuachana na mitandao maana inatuchonganisha na kutaka Nchi isitawalike kwa kusema mambo ya uongo ametolea mfano wa wikileak walivyotoa mazungumzo ya siri kati ya Mkurugenzi wa PCCB kuhusu Tanzania na rushwa ya watu wakubwa,kilichonishangaza kusema US wamekaa kimya baada ya PCCB kukanusha habari hizo na hivyo basi ni habari za uongo kwakuwa america ni Taifa kubwa na lenye vyombo makini vya upelelezi hayo ni mawazo mepesi,ukosefu wa uzalendo,unafiki mkubwa sana na hili watanzania wanajua na dunia inajua!
Amesifu PCCB kufungua kesi kubwa nyingi ni zipi hizo za EPA?KAGODA?TICS?TTCL?NBC?IPTL?RICHMOND?DEEP GREEN?DOWANS? wakati tuliona watu walisamehewa wakaambiwa warudishe basi! na hakuna mwenye ushahidi kama walirudisha! na wengine ole wako hata ulalamike haki yako utakamatwa na kuwekwa ndani kama Mbunge yule mama wa cuf na wengine! yote haya Watanzania wanaona na Dunia inajua! kwa hilo nalo katoa mawazo hafifu kabisa mpaka sasa najiuliza hivi ni vigezi gani vinatumika kuchagua wabunge? yaani Mbunge anachangia ukimsikiliza unaona amefisika kabisa kichwani mpaka unabaki unajiuliza ni unafiki au ujinga?
Anaposema tuachane na mitandao nashangaa sana ktk ulimwengu huu ambao sasa ni kama kijiji,technologia ya habari imeleta mapinduzi makubwa sana duniani na Mbunge anapo shauri watu waachane na technologia ya habari anashangaza sana ktk jamii hii ya kimambo leo,mimi leo hii nimemuona huyu mbunge amepitwa na wakati,ni mtu anaeamini mambo ya kale yasiyo na tija!amelala usingizi wa pono wala hajui kinachoendelea ulimwenguni,jamani tusikubali kupotoshwa na watu wa aina hii,wanakula pesa zetu bule,ni wanafiki au wajinga sana hawafai kuingia bungeni ni watu waliofilisika vichwani na hili watanzania wanajua na dunia inajua!
Amezungumzia kuhusu kuvuja kwa siri za serikali,sasa wataanza kuwaonea watu bure,Technologia imekua sana jamani siku hizi kuficha siri sio rahisi na ndio maana baraza la mawaziri lina kaa watu wanakuja nakala ya mambo yaliyo ongelewa na hii nzuri kweli maana tutajua sasa wasiotuonea wananchi huruma na mambo yanayofanyika yasiyo na tija kwa taifa.jamani serikali ibadilike ikumbatie technologia mtajitahidi kuficha lakini kwa hali ya sasa ni vigumu sana hata Pentagon watu wanapata information tu. Ushauri wa kujaribu kifcha siri ni kuachana kabisa na technologia ya digitali.serikli ipige maruku vitu vyote vinavyotumia technologia ya mawasiliano.pili serikali itete maslahi ya wananchi hapo kutakuwa hakuna haja ya kuficha tena maana mnaficha nini au mambo kama ya jando?
Craaaaaaaaaaaap ndio maana hata wachangiaji ni wachache
i like this!! ha ha ha ha ha..Hata wewe ni mchangiaji......so unataka wingi GANI???????
chakula cha waheshimiwa.Viti maalum?? Neno maalum lifafanuliwe!!!