'Karume Hakuyakimbia Mapinduzi ya ZnZ'- Karume Jnr

John Okello ambaye aliongoza Mapinduzi ya Zanzibar alizaliwa mwaka 1937 huko Uganda katika kabila la Langi ambalo pia ni la Rais wa Zamani wa Uganda Milton Obotte. Alizaliwa akiitwa John Gideon Etuku. Wazazi wake walifariki Akiwa bado mdogo na kulazimika kwenda kulelewa na mjomba wake pamoja na wadogo zake wawili lakini kutokana na utukutu wake hakuweza kuishi kwa mjomba sababu alikuwa akipigwa na akakimbia kwenda kuanza vibarua huko Soroti katika Gineri ya kuchambua pamba. Inasemekana alitaka kwenda kujiunga na jeshi lakini hakufanikiwa kutokana na umri mdogo.

Katika harakati za kutafuta maisha alifika hadi Nairobi nchini Kenya na kuendelea hadi Mombasa ambapo alikuwa ukifanya kazi za vibarua. Alichukia kiuitwa boy , mtumishi, au mtumwa . Mwaka 1955 aliwekwa gerezani huko na akiwa humo alikutana na wapiganaji wa maumau waliokuwa wakipinga Ukoloni nchini Kenya kutoka kwao alipata hamasa ya Kupambana na ukoloni na ukandamizaji.

Mwaka 1959 akiwa na rafiki yake Mluo walienda Pemba katika eneo la Vitongoji na akawa anafanya kazi ya kugonga na kuuza mawe. Huko alipendwa na kuwa na ushawishi na ndipo alipoanza kuonesha nia yake ya kuuondoa utawala wa Sultan. Wakati anaondoka Pemba alipatia chama cha ASP nyumba yake ili waifanye ofisi ya chama.

Mwaka 1963 alihamia Unguja na kuanza kufanya kazi za kupaka rangi nyumba pamoja na kufanya kazi katika kiwanda cha kuoka mikate na akaendelea na vuguvugu la kisiasa.
Kumekuwa na Tetesi kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi na askari polisi na askari wa Mau mau lakini pia kuwa aliwahi kupigana wakati wa vita vya pili vya Dunia, dhana zote hizo si za kweli. Ukweli ni kuwa Okello hakuwahi kuwa mwanajeshi au kupata mafunzo ya kijeshi. Majigambo yake kuwa alikuwa na uzoefu wa kijeshi yalikuwa ni mbinu tu ya kumsaidia kuongoza mapinduzi

Alifanikiwa kuanzisha chama cha Mafundi rangi wa Unguja na Pemba na kupitia chama hicho aliweza kupenyeza ushawishi wake wa kufanya mabadiliko ya kumuondoa Sultan

Baada ya kufanikisha Mapinduzi aalimkaribisha Karume kuongoza serikali. Tatizo la Okello hakuwa na back up ya kisiasa na hakuweza kuaminika. Akatupwa na kufukuzwa bila shukrani. Mwanzoni alipelekwa Kenya lakini akafanya jitihada za kutaka kurudi nchini akakamatwa Mwanza na kufungwa. Lakini baadae akarudi Uganda.

Wakati Idd Amini alipompindua Obotte mwaka 1972 alikwenda kumpongeza. Lakini baadae akawa na Mawasiliano na kundi la Obotte lililokuwa Tanzania, katika harakati za kutaka kujiunga na kundi hilo alikamatwa na kuuwawa na Idd Amin.

Kwa hiyo tunaona kuwa Okello alikuwa Mwanamapinduzi. Kuongoza na kushiriki Mapinduzi ya Zanzibar haikuwa kwa ajili ya Mshahara, bali ilitokana na nia yake ya dhati ya kupinga ukoloni na ukandamizaji.
 
Siyo kuwa kila aaliyekuwa akiishi Zanzibar alikuwa anajua kiswahili. Okelo alikwenda kwanza Kenya kutafuta kazi, akapata kazi ya hovyo hovyo kwa vile hakuwa na elemu, aliposikia zanzibar kuna kazi za upolisi ndipo akaenda kujaribu na akafanikiwa. Kujua lugha huwa inategemea na kichwa cha mtu, wengine ni wazito na wengine ni wepesi. Tuliwahi kusimuliwa hadithi yote ya mapinduzi yale na Brigedia Yusufu Himid pamoja Kanali Abdallah Natepe mwaka 1976; wao wamo kwenye picha hii pamoja na Okello.

View attachment 1747055

Kimoja walichosema wote ni kuwa kwa vile Okello alikuwa haogopi kitu na alikuwa na lugha ya kutisha na sauti ya ukali sana kwa kutumia amri za kipolisi, ndiye aliyekuwa mbele ya mapinduzi yale na aliwatia hofu sana watu wa serikali. In fact alipovamia kituo cha polisi kupora silaha ni kwa vile alikuwa anafanyia kituo hicho hicho na alikuwa anajua silaha ziko wapi.

Ndani ya picha hiyo unaweza kuwaona Abdallah Natepe na nyuma ya Okello, na Yusuf Himid pembeni mwake.
Sorry mie imenikalia kama alipelekwa na watu waliokuwa wakimtumia, na hao ndio baada ya mission kumalizika haraka haraka walijaribu kumuondosha (kufuta ushahidi).

P:S
  1. Picha imepigwa baada ya mapinduzi haina mashiko.
 
Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.
Nawasalimu katika jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwatumia salaam zangu za kuadhimisha kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.

Nawatakia maadhimisho mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Kazi Iendelee!.

Paskali
 
John Okello ambaye aliongoza Mapinduzi ya Zanzibar alizaliwa mwaka 1937 huko Uganda katika kabila la Langi ambalo pia ni la Rais wa Zamani wa Uganda Milton Obotte. Alizaliwa akiitwa John Gideon Etuku.

Mwaka 1959 akiwa na rafiki yake Mluo walienda Pemba katika eneo la Vitongoji na akawa anafanya kazi ya kugonga na kuuza mawe. Huko alipendwa na kuwa na ushawishi na ndipo alipoanza kuonesha nia yake ya kuuondoa utawala wa Sultan. Wakati anaondoka Pemba alipatia chama cha ASP nyumba yake ili waifanye ofisi ya chama.

Mwaka 1963 alihamia Unguja na kuanza kufanya kazi za kupaka rangi nyumba pamoja na kufanya kazi katika kiwanda cha kuoka mikate na akaendelea na vuguvugu la kisiasa.

Alifanikiwa kuanzisha chama cha Mafundi rangi wa Unguja na Pemba na kupitia chama hicho aliweza kupenyeza ushawishi wake wa kufanya mabadiliko ya kumuondoa Sultan

Baada ya kufanikisha Mapinduzi aalimkaribisha Karume kuongoza serikali.

Kwa hiyo tunaona kuwa Okello alikuwa Mwanamapinduzi. Kuongoza na kushiriki Mapinduzi ya Zanzibar haikuwa kwa ajili ya Mshahara, bali ilitokana na nia yake ya dhati ya kupinga ukoloni na ukandamizaji.
Nawasalimu katika jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na kuwatumia salaam zangu za kuadhimisha kumbukumbu ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.

Nawatakia maadhimisho mema ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Kazi Iendelee!.

Paskali
 
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, tutayalinda kwa gharama yoyote.
Labda ungetupa more details kitu gani kinayafanya Mapinduzi yale yawe matukufu ? Roho za wazanzibari wasio na hatia ndio tunaadhimisha ? Keep in mind waislamu wote ni ndugu (dunia nzima), ndugu zetu walitolewa roho kwa kupigwa na Mapanga na akina Okello. Hiki ndio kinayafanya yawe matukufu (kutakwaswa ?).
 
Labda ungetupa more details kitu gani kinayafanya Mapinduzi yale yawe matukufu ? Roho za wazanzibari wasio na hatia ndio tunaadhimisha ? Keep in mind waislamu wote ni ndugu (dunia nzima), ndugu zetu walitolewa roho kwa kupigwa na Mapanga na akina Okello. Hiki ndio kinayafanya yawe matukufu (kutakwaswa ?).
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ndio jina rasmi la Mapinduzi yale, niliwahi kuuliza, Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
P
 
Leo ni Karume Day, nami naomba kujiunga na Watanzania wenzetu maadhimisho mema ya Karume Day na kuwatakia mapumziko mema.
RIP Abedi Amani Karume.
Paskali
 
Leo ni Karume Day, nami naomba kujiunga na Watanzania wenzetu maadhimisho mema ya Karume Day na kuwatakia mapumziko mema.
RIP Abedi Amani Karume.
Paskali

Huyo jamaa alikua ni dikteta mmoja mbaya sana, Hata jiwe ni mtoto mdogo tu mbele yake.
 
Huyo jamaa alikua ni dikteta mmoja mbaya sana, Hata jiwe ni mtoto mdogo tu mbele yake.
Fikilia Kama Leo tumeadhimisha miaka 50 ya kifo chake,ukichanganya na miaka yake,lazima ujiulize huyo mkewe wakati anaolewa alikuwa na miaka chini ya 18 au alikuwa mtu mzima? Na mpaka leo huyo mama ana miaka mingapi?
 
Fikilia Kama Leo tumeadhimisha miaka 50 ya kifo chake,ukichanganya na miaka yake,lazima ujiulize huyo mkewe wakati anaolewa alikuwa na miaka chini ya 18 au alikuwa mtu mzima? Na mpaka leo huyo mama ana miaka mingapi?

Jamaa chini ya utawala wake yamefanyika matukio ya ajabu mingi sana.
 
Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya Mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuwatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.
Wana bodi, japo tuko kwenye harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais na Wabunge, kuna swali linanitatiza kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, ambapo majibu yake sahihi, pia yanaweza kuwa ni kiashiria tosha cha mshindi wa urais wa Zanzibar, iwapo uchaguzi utakuwa huru na wa haki.

Swali hili lahusu ukweli haswa kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, 1964, baada ya kuibuka kwa kitabu kingine kiitwacho "Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru"
View attachment 2077603
kilichoandikwa na Mwanazouni wa Zanzibar, Dr. Harith Ghassany, kama kilivyofanyiwa mapitio na mwandishi Mohamed Said kwenye gazeti la Al-Nuur la leo.

Ghasanny anasema kumbe Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalitekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde (Wakata Mkonge) ambao waliongozwa na Mzee Mohamed Omar Mkwawa (Tindo) chini ya Amiri Jeshi wa jeshi la mamluki hao Victor Mkello (RIP). (kumbe amiri jeshi hakuwa Mganda John Okello pekee, bali pia Mkello yumo?!.

Mamluki hao walitumia zana zao za kukatia mkonge, zile sime za makali kuwili, walizisunda kwenye nguo zao za ndani na kusafirishwa kwa mitumbiwi usiku usiku kupitia Kipumbwi. Jee wale mashuhuda wa Mapinduzi yale Matukufu ya Zanzibar, wanayakubali haya?.

Pia mwandishi anamalizia kwa kusema hata mauaji ya Karume, hayakutekelezwa na wapinga Mapinduzi, bali ni miongoni mwa hao hao wanamapinduzi, baada ya kupishana kauli fulani fulani za uendeshaji wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

Nimesoma kitabu cha John Okello kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar,
View attachment 2077618
yeye anasema yake, vitabu kadhaa vya waandishi wazungu wanasema yao, historia tukuka ya Mapinduzi Matukufuya ya Zanzibar nayo nayo inasema kivyake, hivi hakuna any straight line yoyote kuhusu Mapinduzi hayo, ya Zanzibar?.
Jee yalipangwa na nani? Yalitekelezwaje?.
Nini haswa kilichotokea usiku ule wa Januari 11?.
Nani alifanya nini wapi?
Na mwisho tuzungumzie wafaidika wa Mapinduzi hayo Matukufu ya Zanzibar na bila kuwasahau wahanga wa Mapinduzi hayo ambao kwako yatakuwa sio Matukufu, ni kina nani haswa?, na kama kuleta amani na utangamano wa Zanzibar kuhusu Mapinduzi hayo kutahitajika kuundwa kwa Tume ya Ukweli na Upatanisho, "Truth and Reconciliation Commission" ili waliohasimiana kutokana na Mapinduzi hayo, wapatanishwe kwa maslahi mapana ya Zanzibar?.

Majibu ya maswali haya yatasaidia kujua mustakabali wa matokea ya uchaguzi wa Zanzibar kudhirihisha kuwa Wazanzibari ni wamoja, hakuna kundi la walishiriki Mapinduzi ndio wenye uhalali zaidi kuitawala Zanzibar kuliko wasioshiriki, after all kumbe Mapinduzi yenyewe, yametekelezwa na askari mamluki wa Kimakonde, toka mashamba ya mkonge Tanga!.

Pasco
Rejea za Mwandishi huyu kuhusu Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar
  1. Miaka 50 Ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Bado Kuna Maswali Bila Majibu -1
  2. Neno "Matukufu" Katika Mapinduzi ya Zanzibar, Lilitoka Wapi, na Yana Utukufu Gani?!,
  3. Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
 
Tarehe kama ya leo 11/01/1964 miaka 60 iliyopita, ndio Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yalifanyika!. Alfajiri ya Tarehe 12 Januari, 1964 ilikuwa ni kutangazwa tuu!.

Nawatakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Paskali
Si tulikubaliana ni mapinduzi matukufu ya Tanzania visiwani
 
Si tulikubaliana ni mapinduzi matukufu ya Tanzania visiwani
Tanzania visiwani ndio Tanzania Zanzibar kwa kifupi Zanzibar.
Nakutakia maadhimisho mema ya miaka 60 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
P
 
Back
Top Bottom