'Karume Hakuyakimbia Mapinduzi ya ZnZ'- Karume Jnr

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,178
Kwanza tuendelee kupeana pole kwa Msiba wa Kawawa.
Leo amezikwa na apumzike kwa amani.
Ila pia msiba huu umefungua baadhi ya mambo ambayo hayakupata kujulikana kabla mongoni mwake ni haya...

Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.

My Stake, January mwaka jana nilipata bahati ya kuisikiliza simulizi ya Mjane wa Karume, ambaye ndiye Mama yake Amani, Bi. Fatma Karume akieleza Karume alikuwa wapi wakati wa Mapinduzi, Bi. Fatma alikuwa mkweli zaidi kwa kusema mumewe alijihifadhi mahali, kwa vile hakuwa na uhakika mapinduzi yatafanikiwa, mpaka alipopata uhakika, ndipo akajitokeza. Ikumbukwe iliyeongoza Mapinduzi yale ni Mganda Field Marshal John Okelo na ndie aliyetangaza Mapinduzi kwenye Redio ya Sauti ya Zanzibar alfajiri ya tarehe 12 January,1964.

Hivi jamani, does it really make sense, nchi imepinduliwa usiku wa manane, na wewe alfajiri eti unahangaikia watoto warudi shule baada ya likizo, hivyo mnakosa usafiri, mnapanda mtumbwi, mnashukia Mbeni, mnaomba lifti ya Volkswagon ya watu, mnavamia kwa Kawawa, mnakataliwa kufunguliwa, was it just for watoto Amani na Ali kurejea Shule Malawi?.

Huu ni uthibitisho mwingine jinsi Mzee Kawawa alivyokuwa mtu wa watu. Umati uliojitokeza tangu jana kwenye heshima za mwisho na leo kwenye mazishi, ni uthibitisho wa hili.

RIP Mzee RASHIDI MFAUME KAWAWA, SIMBA WA VITA, UPUMZIKE KWA AMANI.
 
Akiwa aliyakimbia au hakuyakimbia, mie kama mzanzibari wa leo sioni umuhimu wowote.Ninachojua mie, Zanzibar ilipewa uhuru kama nchi nyengine zilizokuwa zimetawalia hapa barani Afrika.

Baada ya uhuru, gurupu fulani halikuridhishwa na waliokamata serekali wakaamua kutumia njia ya nguvu na vita kuindoa i.e Mapinduzi.

Kwa vile hilo gurupu lililopindua lilipata nguvu au hifadhi kutoka Tanganyika (hoja ya msingi ya kuundwa kwa mungano), imebidi hadi leo tuite Mapinduzi ndio uhuru wa kweli.

Lakini hakuna chochote Mapinduzi HAYAKUBALIKI kwenye ulimwengu wa demokrasia, hivyo Zanzibar haina budi kuyaweka kama ni historia na kuendelea kusherehekea uhuru wake wa 1963 kama ilivyo nchi nyengine yoyote iliokuwa koloni.

Huu ndio ufahamu wangu, mimi ni mzanzibari na kijana wa leo napenda kukabiliana na kila aina ya hoja.Lakini hoja hizi za kihistoria ni lazima viongozi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wakubali ukweli, kama mapinduzi sio jambo jema wala lakuomba.Huu ni uvunjwaji wa haki za kibinadamu!

Walioliwa wote kwenye mapinduzi hayo, walikuwa ni wazanzibari waliopachikwa labels za kibaguzi za kiarabu.Lakini amini usiamini, wafuasi hao waliopinduliwa ni wazanzibari na wengine hata rangi zao ni pure Afrikans au Zanzibaris.Si kweli kwamba Pemba nzima ina waarabu, wenye damu ya kiarabu ni chini ya 10%.Kuna sehemu Unguja pia ambazo zinadaiwa zilikuwa ndio hizo zilizokuwa na wafuasi wa serekali iliyopinduliwa, mfano Uzi, Bumbwini, Stone-Town...hizi sehemu zote haina waarabu, kama wapo ni wachache kama sehemu zengine zozote za Zanzibar.

Nawakilisha...
 
Field Marshal John Okello, Kiongozi wa Mapinduzi ya Zanzibar ya January 1964.
Naomba kuwasilisha...
 
Kwanza tuendelee kupeana pole kwa Msiba wa Kawawa.
Leo amezikwa na apumzike kwa amani.
Ila pia msiba huu umefungua baadhi ya mambo ambayo hayakupata kujulikana kabla mongoni mwake ni haya...

Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi.

Akisimulia Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa saa 2 tuu, tangu saa 8:00 usiku mpaka saa10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.
Hivyo kulikucha salama usalmini.

Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kuja Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali shuleni Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?.

Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.

Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?.
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.

Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.

Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.

My Stake, January mwaka jana nilipata bahati ya kuisikiliza simulizi ya Mjane wa Karume, ambaye ndiye Mama yake Amani, Bi. Fatma Karume akieleza Karume alikuwa wapi wakati wa Mapinduzi, Bi. Fatma alikuwa mkweli zaidi kwa kusema mumewe alijihifadhi mahali, kwa vile hakuwa na uhakika mapinduzi yatafanikiwa, mpaka alipopata uhakika, ndipo akajitokeza. Ikumbukwe iliyeongoza Mapinduzi yale ni Mganda Field Marshal John Okelo na ndie aliyetangaza Mapinduzi kwenye Redio ya Sauti ya Zanzibar alfajiri ya tarehe 12 January,1964.

Hivi jamani, does it really make sense, nchi imepinduliwa usiku wa manane, na wewe alfajiri eti unahangaikia watoto warudi shule baada ya likizo, hivyo mnakosa usafiri, mnapanda mtumbwi, mnashukia Mbeni, mnaomba lifti ya Volkswagon ya watu, mnavamia kwa Kawawa, mnakataliwa kufunguliwa, was it just for watoto Amani na Ali kurejea Shule Malawi?.

Huu ni uthibitisho mwingine jinsi Mzee Kawawa alivyokuwa mtu wa watu. Umati uliojitokeza tangu jana kwenye heshima za mwisho na leo kwenye mazishi, ni uthibitisho wa hili.

RIP Mzee RASHIDI MFAUME KAWAWA, SIMBA WA VITA, UPUMZIKE KWA AMANI.

It is a very interesting story.Siasa bwana kazi kweli kweli.
 
Ukweli ndio huu:

  • January 12, 1964 - John Okelo aliongoza mapinduzi ya kwanza kumwondoa Sultani wa Zanzibar na Pemba, Jamshid bin Abdullah - haya mapinduzi yalifuatiwa na umwagaji mkubwa wa damu.
  • Wakati wa mapinduzi waliokuwa viongozi wa vyama vikuu viwili, ASP na UPP walikuwa wanaishi Tanganyika ambako walijificha na ni Okelo aliyewapokea waliporudi Zanzibar baada ya mapinduzi kufanikiwa.
  • Baada ya mapinduzi Okelo aliunda Baraza la Mapinduzi na yeye kama Mwenyekiti wa kwanza alimteua kiongozi wa ASP, Abeid Karume kuwa Raisi wa Zanzibar na kiongozi wa UPP, Sheikh Abdulrahman Muhammad Babu kuwa Waziri Mkuu.
  • Karume kwa msaada wa Tanganyika aliongoza mapinduzi ya pili kumwondoa Field Marshall wa Zanzibar na Pemba na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, John Okelo - haya mapinduzi baridi yalipangwa Dar es Salaam.
Karume, asijaribu kupindisha historia - bado wengine tupo.
 
Zikiwa zimebakia siku kumi kabla ya sherehe za Mapinduzi, bandiko hili limekuja wakati muafaka katika maandalizi ya sherehe za miaka 46 ya Mapinduzi hayo.

Mapinduzi Daima
 
Ukweli ndio huu:

  • January 12, 1964 - John Okelo aliongoza mapinduzi ya kwanza kumwondoa Sultani wa Zanzibar na Pemba, Jamshid bin Abdullah - haya mapinduzi yalifuatiwa na umwagaji mkubwa wa damu.
  • Wakati wa mapinduzi waliokuwa viongozi wa vyama vikuu viwili, ASP na UPP walikuwa wanaishi Tanganyika ambako walijificha na ni Okelo aliyewapokea waliporudi Zanzibar baada ya mapinduzi kufanikiwa.
  • Baada ya mapinduzi Okelo aliunda Baraza la Mapinduzi na yeye kama Mwenyekiti wa kwanza alimteua kiongozi wa ASP, Abeid Karume kuwa Raisi wa Zanzibar na kiongozi wa UPP, Sheikh Abdulrahman Muhammad Babu kuwa Waziri Mkuu.
  • Karume kwa msaada wa Tanganyika aliongoza mapinduzi ya pili kumwondoa Field Marshall wa Zanzibar na Pemba na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, John Okelo - haya mapinduzi baridi yalipangwa Dar es Salaam.
Karume, asijaribu kupindisha historia - bado wengine tupo.
Mag3, alichosema Karume, ni kuwa ile Jumapili ya Januari 12, yeye alikuja bara kuwasindikiza shule Amani na Ali waliokuwa wakisoma Malawi, na sio kuyakimbia mapinduzi. Wanamsingizia tuu, aliwasindikiza wanae kurudi shule baada ya likizo, na alipofika bara, alikaa siku mbili tuu na kurejea ZnZ.
 
Ukweli ndio huu:

  • January 12, 1964 - John Okelo aliongoza mapinduzi ya kwanza kumwondoa Sultani wa Zanzibar na Pemba, Jamshid bin Abdullah - haya mapinduzi yalifuatiwa na umwagaji mkubwa wa damu.
  • Wakati wa mapinduzi waliokuwa viongozi wa vyama vikuu viwili, ASP na UPP walikuwa wanaishi Tanganyika ambako walijificha na ni Okelo aliyewapokea waliporudi Zanzibar baada ya mapinduzi kufanikiwa.
  • Baada ya mapinduzi Okelo aliunda Baraza la Mapinduzi na yeye kama Mwenyekiti wa kwanza alimteua kiongozi wa ASP, Abeid Karume kuwa Raisi wa Zanzibar na kiongozi wa UPP, Sheikh Abdulrahman Muhammad Babu kuwa Waziri Mkuu.
  • Karume kwa msaada wa Tanganyika aliongoza mapinduzi ya pili kumwondoa Field Marshall wa Zanzibar na Pemba na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, John Okelo - haya mapinduzi baridi yalipangwa Dar es Salaam.
Karume, asijaribu kupindisha historia - bado wengine tupo.

So happened to field Marshal John Okello?
 
Ukweli ndio huu:

  • January 12, 1964 - John Okelo aliongoza mapinduzi ya kwanza kumwondoa Sultani wa Zanzibar na Pemba, Jamshid bin Abdullah - haya mapinduzi yalifuatiwa na umwagaji mkubwa wa damu.
  • Wakati wa mapinduzi waliokuwa viongozi wa vyama vikuu viwili, ASP na UPP walikuwa wanaishi Tanganyika ambako walijificha na ni Okelo aliyewapokea waliporudi Zanzibar baada ya mapinduzi kufanikiwa.
  • Baada ya mapinduzi Okelo aliunda Baraza la Mapinduzi na yeye kama Mwenyekiti wa kwanza alimteua kiongozi wa ASP, Abeid Karume kuwa Raisi wa Zanzibar na kiongozi wa UPP, Sheikh Abdulrahman Muhammad Babu kuwa Waziri Mkuu.
  • Karume kwa msaada wa Tanganyika aliongoza mapinduzi ya pili kumwondoa Field Marshall wa Zanzibar na Pemba na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, John Okelo - haya mapinduzi baridi yalipangwa Dar es Salaam.
Karume, asijaribu kupindisha historia - bado wengine tupo.

Ukitupatia maelezo zaidi ya Okello na waliopanga hayo mapinduzi utafanya jambo la maana.Huu unaweza kuwa ukweli na inaingia akilini kuwa, mapinduzi hayafanywi na wanasiasa na Karume alikuwa ni mwanasiasa si mwanajeshi.Automatically, hawezi kuwa hata alikuwepo karibu!
 
So happened to field Marshal John Okello?
Baada ya Mapinduzi, ile 12/01/64, 16/01/64 Julius alimuita Okello huku bara, kufika tuu, aliwekwa chini ya ulinzi na kupigwa PI hadi Nairobi, akakataliwa, akapelekwa Uganda, akatiwa ndani. Wajeshi wa Tanganyika Rifles waliposikia kama Okello ameweza Zanzibar sasa yuko bara, kwa nini na wao wasifanye kweli. Nao 18/01/64 wakajaribisha, this time ilikuwa ni zamu ya Julius kutoroshwa na mtumbwi sijui kama alifichwa Zanzibar au aliishia Bongoyo.

Mambo yalipotulia, kesho yake 19/01/64 alilivunjilia mbali lile jeshi na 20/01/64 likaundwa JWTZ Sarakikya akiwa mkuu wa kwanza wa jeshi hilo.

Okello alionekana ni mtu hatari kote kote, kule Uganda aliachiwa, nasikia aliishia Kenya na mwishowe alijifia.

Paskali
 
Violence.JPG


Zanzibar is well known for it's "Shortest War in History". A 19th Century battle that lasted only about 45 minutes but served to demonstrate for all time the Iron fist beneath the pre-colonial European domination of East Africa.
What is less well known is the 20th Century record Zanzibar set for similar brevity in the Zanzibar Revolution of 1964. In this Revolution a government with over a century of continuity was toppled in less than a day. Essentially a Settler Society, with well defined Arabic, Indian, Swahili, Comoran and indigenous elements, and ruled by an Hereditary Sultan, the newly independent Nation of Zanzibar vanished in astounding suddenness.
That night was full of suspense and surprise, courage and despair. It began at 3 am on the day just before a large religious Holiday. The holiday prompted large numbers of people to congregate in and around Stone Town. They set up tents or just sleep under the palms while awaiting the opening of the festivities in the morning. Among the crowds were large numbers of young men, some of these men were followers of a minor politician named John Okello. Just how many men actually followed Okello into revolutionary battle is of some dispute.
Clove_Flag.gif

It is clear that by the end of that fateful day thousands had joined the revolutionaries but this was after the results were known. It's also true that Field Marshal Okello talked of having had 4 "battalions" in the field against the government forces that night, but how men many were really there when it counted?
Okello reported that the revolution began when he marched in the dead of night on the Ziwani Police Barracks (and Armory) at the head of the 250 men of his "4th Battalion". At 3:00 am he ordered his men to cut the wire surrounding this fortified compound. That was the first real revolutionary act and it served to "separate the men from the boys". Okello said of his men at the time, "The enormity of our predicament was suddenly obvious to them: we, armed with pangas, spears and a few motor car springs were going to face the risk of close combat with men armed with automatic rifles... ". All but 40 men deserted or refused to crawl through the wire.
These 40 men seized the Island of Zanzibar and toppled a dynasty that had ruled the islands through 12 Sultans for over 133 years.

The revolutionaries crawled to within 25 meters of the Barracks building. Inside, asleep were scores of paramilitary police. However like most sensible people on Zanzibar they slept on the upper floors of the building, where cooling ocean breeze could ventilate the hot tropical nights. Only two men were awake and on guard duty below.
Okello_bren2.jpg

John Okello and his men rushed at these guards. Automatic fire rang out and three of the 4th battalion men went down. However one of sentries also fell, downed by an arrow shot by a revolutionary named Albert. By then Okello had closed on the remaining sentry. It was here that the deciding moment of the revolution occurred. The two crashed together, the Field Marshall tells us that "I got hold of the gun, we fought and I managed to hit him in the cheek with the gun butt". The firing stopped.
His men were now at the gates of the armory where hundreds of modern weapons and thousands of rounds of ammunition were locked up. The police above, who were unarmed, (in keeping with standard peacetime practice, all weapons were locked away "for safekeeping" when the officers were off duty), attempted to storm down the single exterior staircase and enter the fray. However the 4th Battalion men unleashed a rain of spears, arrows and stones on the stunned troops and they piled up upon themselves on the narrow staircase. Okello's liberated rifle, which had only three bullets left, decided the issue with a short burst of fire. The police retreated back upstairs to look for ropes to lower men out of the windows.
It was too late. The doors of the armory gave way and the 4th Battalion rushed in. Soon every man was armed with a modern automatic rifle. The "Freedom Fighters" who had started the night armed with sharpened automobile springs now were the best equipped force on the Island. They poured a fuselage of fire into the upstairs rooms and very shortly the surviving police surrendered.

The Sultan's forces made one serious attempt to counter attack the rebels. The "flying squad" arrived on the scene about an hour after the defeat of the Ziwani garrison. These 75 or so men had only light duty firearms and were no match for the now heavily armed Battalion ensconced in the fortified Armory. The rebels allowed the Sultans' paramilitary police to approach and then poured an overwhelming storm of fire into them. The firing was so intense that the surrounding bush caught fire and the police retreated in despair.
Sultans_escape.jpg


With their new base secure, guns were distributed to the other three Battalions (who had encircled but not yet attacked other key sites). In short order the few other police posts and the communications centers were overrun and captured. The most serious resistance was offered by the Malindi Police Station, where firing could still be heard in the late hours of the morning. However by noon the Sultan had fled, the rest is history.
 
Mie bado nimeachwa na maswali mengi kushinda majibu...Majina yote ni Okello, Albert hawa walikuwa ni wazanzibari?

Au walikuwa na support kutoka wapi ya kufanya mapinduzi haya?Kuna mmoja amesema kuwa Okello pia alitaka kumfanyia mapinduzi Mwalimu....wakati Okello ni mganda ninavyojua mimi kwa habari za kusoma hapa na pale, sasa huyu jamaa alikuwa na support gani na alikuwa na interests gani za kuhama kwao na kuja huku Tanganyika na Zanzibar kufanya vurugu.
 
Mie bado nimeachwa na maswali mengi kushinda majibu...Majina yote ni Okello, Albert hawa walikuwa ni wazanzibari?

Au walikuwa na support kutoka wapi ya kufanya mapinduzi haya?Kuna mmoja amesema kuwa Okello pia alitaka kumfanyia mapinduzi Mwalimu....wakati Okello ni mganda ninavyojua mimi kwa habari za kusoma hapa na pale, sasa huyu jamaa alikuwa na support gani na alikuwa na interests gani za kuhama kwao na kuja huku Tanganyika na Zanzibar kufanya vurugu.

Okello alikuwa polisi hapo Zanzibar ingawa alikuwa ametokea Uganda.



Bila kujali ni nani aliyeongoza mapinduzi yale, yalikuwa siyo halali kabisa. Yaliondoa serikali halali iliyopatika kwa mujibu wa katiba na kuweka serikali ya kimabavu, na kusababisha vifo vya watu wasiokuwa na hatia karibu laki nzima na zaid.
 
Na Joseph Mihangwa
NIMEPOKEA maswali mengi na hoja mbalimbali kutoka kwa wasomaji wa gazeti hili kutokana na makala yangu iliyochapishwa katika toleo la 30 Aprili 2008 iliyobeba kichwa cha habari kisemacho: "Karume na zimwi la Mapinduzi."
Karibu hoja zote na maswali zililenga kutaka ufafanuzi juu ya kutaka kufahamu kama kweli muasisi wa taifa la Zanzibar, Hayati Abeid Aman Karume, hakushiriki katika mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964.
Wengi waliuliza, "Kama Karume hakushiriki, kwa nini historia inapotoshwa?"
Katika makala yangu nilieleza kwa ufupi kwamba inawezekana kabisa wazo la mapinduzi halikuwamo akilini mwa Karume.
Nilisema Karume ambaye tangu mwanzo alipendelea kuona Serikali ya mseto kati ya vyama vya Zanzibar Nationalist Party (ZNP), Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP) na chama chake- Shirazi Party (ASP), kama njia pekee ya kuleta umoja wa kitaifa.
Ingawa kuna taarifa kwamba Waziri Mkuu wa wakati huo, Mohamed Shamte, alikataa ombi la Karume, upo ushahidi kuwa serikali hiyo iliundwa mwaka 1961.
Katika serikali hiyo ya mpito, Karume alipewa na alikubali kupokea nafasi ya uwaziri wa Siha (Afya).
Hii ni ishara tosha kwamba chama cha ASP kiliutambua ushindi wa serikali ya ZNP na ZPPP; hoja inayojitokeza sasa kwamba Zanzibar ilipata uhuru 12 Januari 1964, badala ya 10 Desemba 1963 ni dhaifu na isiyo na mashiko.
Kuna madai pia kwamba Karume hakuwahi kuwa rais wa Zanzibar. hii ni kwa sababu rais huchaguliwa chini ya Katiba; mtu anayeongoza Mapinduzi huitwa "Kiongozi wa Mapinduzi."
Vilevile, Karume hakuwahi kuchaguliwa hata mara moja na wananchi wa Zanzibar. Pia chini yake, Zanzibar haikuwahi kuwa na katiba.
Kuhusu mapinduzi, Karume mwenyewe aliwahi kukiri kwamba aliondoka Zanzibar mara tu harakati za mapinduzi zilipoanza.
Hatua hiyo inadhihirisha kwamba Karume aliyakimbia mapinduzi hayo. Ni kutokana na kutojua mapema kilichokuwa kikiendelea.
Hizi si taarifa ya uzushi. Ni taarifa sahihi na zinazothibitishwa na mtandao wa Wikipedia Encyclopedia.
Kwa mujibu wa mtandao huo, "Abeid Karume hakuwa Zanzibar usiku ule Mapinduzi yalipofanyika."
Wengi wanasema Mapinduzi haya yalipangwa na Wakulima, Wakwezi na Wavuvi. Hapana! Mapinduzi yalipangwa na watu wenye kuelewa mambo na wenye ujuzi wa kutosha wa kutumia silaha.
Hawa ni baadhi ya polisi wasio Wazanzibari walioachishwa kazi baada ya uhuru wa Desemba 1963 na kubakia Zanzibar wakiumia kimaisha bila kazi.
Maana kama mapinduzi yalipangwa na wakulima, wavuni na wakwezi, kundi hili lilipata wapi uzoefu wa silaha na mbinu za kivita hata kuteka vituo vya usalama na kupora silaha?
Waliopanga kufanya mapinduzi wanafahamika. Hawa hawakuwa Wazanzibari asilia. Ni pamoja na Field Marshal (John Okello (Mganda) na msaidizi wake, Absalom Anwi Ingen (Mjaluo kutoka Kenya).
Wengine ni Saidi Washoto (Tanganyika) sasa Tanzania Bara, Mohamed Kaujore (Mmakonde wa Msumbiji) na Hamisi Darwesh (Tanganyika).
Walikuwapo pia akina Abdallah Mfaranyaki (Tanganyika), Saidi Natepe (Tanganyika), Seif Bakari (Tanganyika) na Edington Kisasi (Mchaga wa Kilimanjaro-Tanganyika).
Vyombo vya habari navyo vinatoa ushuhuda juu ya nani aliongoza Mapinduzi. Gazeti la serikali ya Tanganyika (The Standard) la 13 Januari 1964, liliandika katika ukurasa wake wa mbele kwamba:
"Wapigania Uhuru waliokuwa na silaha wamekitwaa Kisiwa cha Zanzibar. Wamekamata majengo yote muhimu ya Serikali kwa muda usiozidi saa 24. Usiku Kiongozi wa Mapinduzi alitangaza muundo wa Serikali mpya ya Jamhuri ya Zanzibar na Pemba …".
Kiongozi huyo alikuwa Okello, ambaye katika tangazo lake la Mapinduzi alipanga Baraza lake la Mawaziri.
Field Marshal John Okello (Waziri wa Ulinzi na Utangazaji na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi); Sheikh Abeid Amani Karume (Rais wa Serikali ya Mapinduzi) na Kassim Hanga, Makamu wa Rais.
Mawaziri wake walikuwa ni Abdurahman Babu (Ulinzi na Mambo ya Nje), Aboud Jumbe (Afya na Huduma za Jamii) na Othman Sharrif (Elimu).
Okello aliwateua pia Hasnu Mukame kuongoza Wizara ya Kilimo na Idris Abdul-wakili kuongoza Wizara ya Biashara.
Haukupita muda Okello akamtaja Hasnu Makame kuwa Waziri wa Fedha na Salehe Sadallah (Kilimo).
Okello alimaliza kwa kusema, "Serikali sasa inaendeshwa nasi –Jeshi. Ni juu ya kila raia, mweusi, maji ya kunde au mweupe kutii amri……".
Gazeti hilo "The Standard," lilizidi kuthibitisha kuwa Field Marshal amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari katika ofisi za kurushia matangazo.
Gazeti lilisema, "lundo la bastola lilikuwa mbele ya meza yake. Walinzi wenye silaha mbalimbali walisimama kumzunguka kwa utii na nidhamu…."
"…ni yeye aliyepanga kuiangusha Serikali ya Zanzibar akisaidiwa na Kamati Kuu yake ya watu waliopewa siku 14 tu za mafunzo msituni."
Ali Muhsin Ali Barwan, aliyekuwepo Zanzibar siku ya Mapinduzi anaeleza katika Kitabu chake "Conflicts and Harmony in Zanzibar," kwamba "…John Okello, askari mamluki, aliongoza mauaji ya kinyama …. Watu 12,000 walichinjwa…"
Nalo gazeti la The Spectator la nchini Uingereza katika toleo lake la 7 Februari 1964, chini ya makala iliyosema "Gidion's Voice" pamoja na lile la 12 Februari 1964 "How it Happened", linaeleza kuwa ni John Gidion Okello aliyeongoza mapinduzi.
Gazeti linafika mbali zaidi na kusema, "ni yeye aliyewavuta wote waliokuja kushirikiana naye katika kutekeleza mapinduzi hayo."
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haroub Othman (Mzanzibar), katika kitabu kiitwacho, "Mwalimu The Enfluence of Nyerere-Uk 172," anathibitisha kuwa uhuru wa Zanzibar ulipatikana 10 Desemba 1963.
Anasema Sultan alikuwa Mkuu wa Nchi, na kupewa mamlaka ya kuteuwa mrithi wake. Serikali hiyo ilipinduliwa ndani ya majuma matano tu na "Masiha mjinga," ambaye ni kiongozi wa wanaharakati John Okello.
Okello alisimika Baraza la Mapinduzi ndani ya kipindi kifupi chini uongozi wa Karume.
Hata Amiri Mohamed anakiri katika kitabu chake "A Guide to a History of Zanzibar" kwamba Okello ndiye aliyetawala Uwanja wa Mapinduzi kwa miezi miwili mfululizo kuanzia 12 Januari 1964 hadi alipokamatwa na kufukuzwa nchini akiwa ziarani Tanganyika. Aliambiwa ni mhamiaji asiyetakiwa visiwani humo.
Anasema ya kuwa Okello akiwa na wapiganaji wapatao 400 aliongoza mashambulizi na baada ya kukamilisha kazi aliendelea kutoa maagizo kupitia kituo cha radio.
Anasema, "ukweli wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanaona kuwa Okello ndiye alikuwa rais wa kwanza halali wa Serikali mpya ya Mapinduzi yenye Baraza kamili la Mawaziri.
Hakuna mahali popote wala kumbukumbu za historia, kuonyesha kwamba Abeid Amani Karume aliwahi, katika hatua yeyote ile, kupanga, kuongoza au kushiriki katika Mapinduzi hayo ya 12 Januari 1964.
Sasa kama ni hivyo, kwa nini historia ilipotoshwa na ushiriki wa Okello kutopewa uzito unaostahili?
Jibu linatolewa na Michael F. Lofchie, katika Kitabu chake Was Okello's Revolution a Consiracy kuanzia uk 36 hadi 42. Anasema, "Okello alifanya Mapinduzi ya Zanzibar…..Njama za kumwondoa Zanzibar ni za kuficha ukweli unaochukiza…."
Kutokana na hali hiyo, majigambo, hila na hadaa za rais wa sasa wa Zanzibar, kwamba baba yake (Abeid Amani Karume), ndiye aliyeendesha mapinduzi hayo, hayana msingi na kuendeleza kuyasikiliza, ni kufinyanga historia.

jmihangwa@yahoo.com. 0713 -526972

 
Kumbe JF bado ni source ya habari kwa blogs nyingine. Nimeinasa hii kwenye blog yao yaani wamekata na kupaste kama ilivyo bila hata mention ya jamiiforum as if ni habari yao.
Karume aliyakimbia mapinduzi?


Rais Karume akizungumza kwenye TBC, amekanusha ule uvumi wa Karume kuyakimbia Mapinduzi ya mwaka 1964.
Akieliezea Rais Karume amesema mapinduzi ya Zanzibar yalifanyika kwa muda wa masaa 2 tuu, kuanzia saa 8:00 usiku hadi saa 10 alfajiri ya Jumamosi ya tarehe 11/01/1963 kuamkia Jumapili tarehe 12/01/1964.Hivyo kulikucha salama usalmini.
Hivyo Jumapili hiyo, yeye Karume alikuwa na safari ya kwenda Dar es Salaam ili awapeleke watoto wake, Amani na Ali masomoni huko Malawi (Kuna hoja iliwahi tolewa Karume ni Mnyasa wa Malawi, alikuja Zanzabar kama kuli Bandarini Zanzibar) hivyo watoto kumbe walisoma kwao?
Karume akaendelea kusema kuwa hiyo Jumapili asubuhi, walitafuta usafiri wakakosa, hivyo wakasafiri na mtumbwi toka Zanzibar saa 7 mchana, wakafika Mbweni saa 11 jioni.
Waliposhuka pwani ya mbweni, Baba yake akaomba lifti kwa bwana mmoja alikuwa na gari ya Volkswagon, yule bwana akamuuliza nikupeleke wapi?
Ndipo Karume akasema nipeleke kwa Kawawa. Hivyo Karume na wanae wawili ndani ya Vokswagon mpaka getini kwa Kawawa.
Kufika pale, akajitambulisha, walinzi hawana taarifa zake, and by then who was Karume, walinzi wakomgomea kumfungulia. Ndipo akaomba kutuma ujumbe kwa Kawawa aliyekuwa ndani, ili atoe ruhusa waruhusiwe kuingia.
Kawawa kusikia Karume yupo nje, badala ya kutoa amri afunguliwe, alishuka moja kwa toka toka ndani ghorofani, akaja mpaka nje ya geti na kumpokea Karume yeye mwenyewe in person, walinzi kuona mpaka bosi kashuka, wasifungue milango wenyewe?.
Huo ndio ukawa mwanzo wa Amani kumuona Kawawa.
Kesho yake Juliasi akaja kuawatembelea hapo kwa Kawawa na jioni yake Karume akawaacha wanaye kwa Kawawa, yeye akarudi zake Zanzibar, huku nyuma watoto wakaenda shule, na yeye akaenda kutangazwa Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, hivyo wale wote wanaodai eti Karume aliyakimbia Mapinduzi, si wakweli, wanamsingizia tuu.
January mwaka jana tulipata bahati ya kuisikiliza simulizi ya Bi.Fatma Karume, ambaye ndiye Mama yake Amani. Bi. Fatma Karume akieleza Karume alikuwa wapi wakati wa Mapinduzi, Bi. Fatma alikuwa mkweli zaidi kwa kusema mumewe alijihifadhi mahali, kwa vile hakuwa na uhakika mapinduzi yatafanikiwa, mpaka alipopata uhakika, ndipo akajitokeza. Ikumbukwe iliyeongoza Mapinduzi yale ni Mganda Field Marshal John Okelo na ndie aliyetangaza Mapinduzi kwenye Redio ya Sauti ya Zanzibar alfajiri ya tarehe 12 January,1964.
Hivi jamani, inaingia akilini, nchi imepinduliwa usiku wa manane, na wewe alfajiri eti unahangaikia watoto warudi masomoni baada ya likizo, hivyo mnakosa usafiri, mnapanda mtumbwi, mnashukia Mbeni, mnaomba lifti ya Volkswagon ya watu, mnavamia kwa Kawawa, mnakataliwa kufunguliwa, hii ilikuwa kweli anaharakia watoto warudi masomoni au anakimbia Mapinduzi?

Januari 2, 2010 | Gawanyo Makala

7 maoni Karume aliyakimbia mapinduzi?

  • 470388ca084474f3bcabd0fefbf220d6
    mrfroasty
    Januari 2, 2010 katika 5:14 um · Jibu
    Akiwa aliyakimbia au hakuyakimbia, mie kama mzanzibari wa leo sioni umuhimu wowote.Ninachojua mie, Zanzibar ilipewa uhuru kama nchi nyengine zilizokuwa zimetawalia hapa barani Afrika.
    Baada ya uhuru, gurupu fulani halikuridhishwa na waliokamata serekali wakaamua kutumia njia ya nguvu na vita kuindoa i.e Mapinduzi.
    Kwa vile hilo gurupu lililopindua lilipata nguvu au hifadhi kutoka Tanganyika (hoja ya msingi ya kuundwa kwa mungano), imebidi hadi leo tuite Mapinduzi ndio uhuru wa kweli.
    Lakini hakuna chochote Mapinduzi HAYAKUBALIKI kwenye ulimwengu wa demokrasia, hivyo Zanzibar haina budi kuyaweka kama ni historia na kuendelea kusherehekea uhuru wake wa 1963 kama ilivyo nchi nyengine yoyote iliokuwa koloni.
    Huu ndio ufahamu wangu, mimi ni mzanzibari na kijana wa leo napenda kukabiliana na kila aina ya hoja.Lakini hoja hizi za kihistoria ni lazima viongozi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wakubali ukweli, kama mapinduzi sio jambo jema wala lakuomba.Huu ni uvunjwaji wa haki za kibinadamu!
    Waliuliwa wote kwenye mapinduzi hayo ni wazanzibari waliopachikwa labels uarabu.Lakini amini usiamini, wafuasi hao waliopinduliwa ni wazanzibari na wengine hata rangi zao ni pure Afrikans au Zanzibaris.Si kweli kwamba Pemba nzima ina waarabu, wenye damu ya kiarabu ni chini ya 10%.Kuna sehemu Unguja pia ambazo zinadaiwa zilikuwa ndio hizo zilizokuwa na wafuasi wa serekali iliyopinduliwa, mfano Uzi, Bumbwini, Stone-Town…hizi sehemu zote hazina waarabu, kama wapo ni wachache kama sehemu zengine zozote za Zanzibar.
    Nawakilisha…
  • 8e26250b533dc649c5563520f735c545
    Mwanambaya
    Januari 2, 2010 katika 6:52 um · Jibu
    HOJA ZAKO MRFROAST NI ZA MSINGI. NATHAMINI MICHANGO YAKO YENYE KUJENGA. UNAONEKANA NI MTU MJUVI. ENDELEA VIVYO HIVYO…
  • 6ce1dd33dbc7bd97e58d890b4172da63
    Mzenji
    Januari 2, 2010 katika 8:32 um · Jibu
    Mie simtetezi wa mapinduzi, ila uhuru wa Zanzibar hauwezi kuwa huo wa 1963 ukizingatia Sultan nae pia alikuwa mkoloni Zanzibar kama hao waingereza. Sasa utasemaje Zanzibar ilipata uhuru 1963 wakati Sultan bado alibaki kuwa ndie mtawama wa Zanzibar
  • 470388ca084474f3bcabd0fefbf220d6
    mrfroasty
    Januari 2, 2010 katika 9:33 um · Jibu
    @Mzenji
    Ni vyema kwa wazanzibari kuchukulia watu wenye jinsia zote wanaoishi visiwani humo kuwa ni wazanzibari.Kwa kutumia mtazamano wa kuwa Zanzibar kuna jinsia tofauti, waarabu, wahindi, wazungu na waafrika bila ya shaka Sultani nae alikuwa ni mzanzibari.Na huwezi kusema alikuwa mkoloni, kufanya hivyo ni kuonesha ubaguzi na chuki tuu.Ambayo itakubidi useme hadi leo mtu mwenye asili ya kihindi au kiarabu aliomo visiwani humo, hana haki ya kukamata madaraka.
    Mie binafsi yangu sipendi mfumo wa kifalme, lakini wakati huo huo siwezi kuyatukuza mapinduzi.Yaliyotokea yametokea, lakini tusiseme kuwa mauaji ya 1964 yalikuwa halali….yametokezea tuu, kuna sehemu nyingi tuu yametokezea mauaji ikiwemo Ruanda, Burundi…hii yote ni mifano tuu ya athari za chuki na ukabila usiokuwa na maana.Na kwa Zanzibar, hakuna tofauti na nchi nyengine yoyote makabila ya watu tofauti yanaishi humo…watu wa dini tofauti wamo humo…kwa hiyo tukubali tuu, hata kama Raza akisema anagombea urais…basi tukubali kama ni mzanzibari madhali anaishi humo na raia wa humo…bila ya kutizama kama asili ya kihindi!!!
    Sasa kama Raza tutamkubali, ni kwanini tusiwakubali hao wenye asili ya kiarabu kama ni wazanzibari????Kumbuka kuna nchi ambazo ni pure afrikans, nazo pia zina mifumo ya kifalme…kuna mfalme Mswati n.k…na joho linavaliwa hadi leo Zanzibar kwenye maharusi, tusije tukaanza kupandishiana chuki na kuvuana uzanzibari …ati mfalme alivaa joho, basi si mzanzibari ni mkoloni!!!
    Sasa wazanzibari wote waliokuwa wakiishi visiwani humo nao walikuwa wakoloni?Maana utawala huo wa kifalme ulikuwa na support kubwa kutoka Pemba, Uzi, Stone-Town, Bumbwini, humu mote mulikuwa kumejaa wakoloni???Au waarabu???….tuacheni jamani haya mapinduzi tuyawekeni kama ni tukio lilitokezea, baada ya yote hayo hata tukisema lilikuwa tukio jema au baya haitusaidii chochote baada ya kupandiziana chuki baina ya waliondokewa na wapenzi wao kwenye familia zao.
    Naamini kwa dhati kama kusherehekea uhuru wa 1963 ni jambo la busara katika kujenga maridhiano na ustahamilivu wa makabila yaliomo visiwani humo.
  • c59544bcc6d74517a5f5183d3300f620
    Ustadh Pengo
    Januari 3, 2010 katika 5:19 mu · Jibu
    Mimi nasema waarab na wahindi bado kupewa urais katika nchi za Kiafrika kama wao msimamo wao ni watu weusi (Waafrica) hawawezi kuwa na hata ukurugenzi katika nchi zao. Tutawakubali kama watanzania au wanzanzibar ndani ya hiyo Tanzania hao wahindi bado wanatubagua na hao warabu pia tunakuwa nao wanapokuwa na shida tu. mapinduzi wache tuyaite vile vile Mapinduzi kama ni mabadiliko tu. Si tunakuoneni watu wa kisiwa cha pili yaani Pemba mnapenda sana kuoa watu wenye asili ya kiarabu hala fu mnadhalilisha mbona wao hawapendi kuoa wafrika halisi , wangeonesha hayo madogo madogo basi tungesahau mapinduzi. Lakini wao ndio wenye kufanya sisi tuone mapinduzi ndio mkmbozi na itabi vile vile.
  • 6ce1dd33dbc7bd97e58d890b4172da63
    Mzenji
    Januari 3, 2010 katika 6:20 mu · Jibu
    Mrfroasty, sijasema kwamba huyo Jamshid si zanzibari, Mzanzibari kamili kama mimi na wew ila kwa nin tawala wa kizungu afrika ulikuwa wakikoloni ila wa kisultan ambao ulianzia 1840 usiwe ukoloni? Au hukusoma katika historia Zanzibar kulikuwa na tawala za jado kama usultan? Mapinduzi nakubali kwamba yana connotation mbaya sio Zanzibar tu ulimwengu mzima. Kila alipofanyika mapinduzi, basi kunaashiria kwamba demokrasia ilishindikana au kukiukwa na kupelekea watu chungu nzima wasionahatia yeyote kupoteza maisha.
    Swala la ubaguzi halipo zanzibar tu, ulimwengu mzima karne na makarne watu wanabaguana ila huu ubaguzi wa rangi ndio bado culprit hadi leo hii, licha kwamba katika nchi ya marekani tumeona rais wa kwanza mwenye damu nyeusi ila hata huko bado ni tatizo sugu. Watu weupe wanaogoza zaidi kuwaona wenzao weusi inferior na hawana thamani sawa na wao. Sisi wazanzibari culture yetu imekuwa influenced sana na uarabu hadi, hata wale wazanzibari wenye damu kidogo sana ya uarabu basi kuna desturi ya kujiona bora kuliko weusi kabisa.
    Waarabu zanzibar hawabaguliwi ila wanabagua, hakuna hata ishara ya kubaguliwa, ubaguzi wa upemba na uunguja ndio sumu, mimi ni mpemba mweusi sina babu wala bibi hata mmoja mwenye asili ya kiarabu ninaemjua ila katika serikali ya Zanzibar ntakuwa outcast sawa na mpemba mwengine mwenye damu ya kiarabu. Mimi sioni tatizo kwa Zanzibar kuwa na rais mwenye asili ya kiarabu au kihindi ilimradi aelewe kwamba yeye si rais wa wawahindi au waarabu bali wa Zanzibar.
    Kuhusu suala la ndoa, siku zote mtu huoa mke anaependezewa nae, sasa sioni ajabu kwa mtu mweusi kuamua kuoa muarabu kama kapendezewa, na pia watu wengi wanafikia uamuzi huo ili kupata kizazi kilichochanganya ambapo watoto wataweza kukubalika kwenye jamii zote. Ila ulivosema Ustaadh Pengo ni kweli kwamba ndoa nyingi kati ya weusi na waarabu huwa ni mume mweusi tena mwenye uwezo, kuoa mke muarab na sio vice versa, hapa ndio maana nikasema kwamba waarabu Zanzibar hawabaguliwi ila wao ndio wabaguzi.
    Nawasilisha.
  • 36b39ef6043636912f9775afdfb7b35a
    Pasco
    Januari 3, 2010 katika 9:22 mu · Jibu
    Heshima Mbele wana Mzalendo Net.
    Mimi ndie mwandishi wa habari hii, ni ustaarabu tuu wa kazi za maandishi, unapochukua habari fulani au kazi fulani bila idhini, unawajibika kutoa attribution ya source ‘kwa mujibu wa jamiiforums' ili kutoa haki ulikoipata.
    Ni lengo la kila mtoa habari isambae kadri iwezekanavyo ila pia muitendee haki ilikopatikana.
    Asante na endelezeni kazi nzuri kuhabarisha jamii.
 
Huko Zenj wote ni Kina ali babu sio?
Ndio, Zanzibar wapo wakristo, hindus na makabila mengine.Lakini asilimia zaidi 95% majina yao ni yenye asili ya kiarabu kutokana na uislamu na sababu zengine.

Na mpelelezi yoyote akiona Okello, Albert, James ni lazima aanze kushtuka hawa watu ni kweli wazanzibari?Na ukitizama kwa ndani sijakosea sana, ni kweli Okello alikuwa mganda.

Kumbe JF bado ni source ya habari kwa blogs nyingine. Nimeinasa hii kwenye blog yao yaani wamekata na kupaste kama ilivyo bila hata mention ya jamiiforum as if ni habari yao.

Pasco hiyo habari nimeichapa mie hapo kwenye blogi hiyo, sio pure copy paste.Nimefanya few editing, ili iweze kufit na mijadala ya blogi hiyo.

Nikashindwa kuweka chanzo, kutokana na kuwa habari sio fully copy pasted.

Nimefanya editing na kuweka chanzo, badala ya comment zako.

On the other part, JF bado ni chanzo kikubwa cha habari hususan kwa blogs ambazo huchapa habari za magazeti au forums kama JF.

Samahani kama nimekera na hiyo editing...
 
Pasco hiyo habari nimeichapa mie hapo kwenye blogi hiyo, sio pure copy paste.Nimefanya few editing, ili iweze kufit na mijadala ya blogi hiyo.

Nikashindwa kuweka chanzo, kutokana na kuwa habari sio fully copy pasted.

Nimefanya editing na kuweka chanzo, badala ya comment zako.

On the other part, JF bado ni chanzo kikubwa cha habari hususan kwa blogs ambazo huchapa habari za magazeti au forums kama JF.

Samahani kama nimekera na hiyo editing...

Asante MrFroasty for coming uu and being open.
Hata ukifanya editing, bado unaobligation ya kumention source.
Kwa vile original source ni media, TBC, kwa kutoitaja jamiiforum kama source yako, unawaambia wasomaji wako, aliyesikiza TBC ni Mzalendo Net.

Mwisho, Mr. Froasty, sijakereka wala, ndio nazidi kufurahi kwa kadri habari inavyosambaa na kuwafikia wengi zaidi nikiamini lengo la blogs zote ni kutoa/kusambaza habari na kuchochea mijadala.

Asante.
 
najiuliza sina jibu,

je kama kweli karume hakuwa na mchango wowote
katika mapinduzi ya zanzibar kama baadhi ya post zinavyoashiria, ilikuwaje
akaweza kumuondoa okello bila resistance kubwa kutoka kwa waliomuunga
mkono okello? kwani kwa kuongoza mapinduzi kwenye "field" nina hakika
alikuwa anao watu ambao walikuwa tayari kupoteza maisha yao kwa kumuunga
mkono yeye. kwani nijuavyo mimi "bond" inayojengeka katika uwanja wa vita ni kubwa sana.
 
Na Joseph Mihangwa
NIMEPOKEA maswali mengi na hoja mbalimbali kutoka kwa wasomaji wa gazeti hili kutokana na makala yangu iliyochapishwa katika toleo la 30 Aprili 2008 iliyobeba kichwa cha habari kisemacho: “Karume na zimwi la Mapinduzi.”
Karibu hoja zote na maswali zililenga kutaka ufafanuzi juu ya kutaka kufahamu kama kweli muasisi wa taifa la Zanzibar, Hayati Abeid Aman Karume, hakushiriki katika mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964.
Wengi waliuliza, “Kama Karume hakushiriki, kwa nini historia inapotoshwa?”
Katika makala yangu nilieleza kwa ufupi kwamba inawezekana kabisa wazo la mapinduzi halikuwamo akilini mwa Karume.
Nilisema Karume ambaye tangu mwanzo alipendelea kuona Serikali ya mseto kati ya vyama vya Zanzibar Nationalist Party (ZNP), Zanzibar and Pemba People’s Party (ZPPP) na chama chake- Shirazi Party (ASP), kama njia pekee ya kuleta umoja wa kitaifa.
Ingawa kuna taarifa kwamba Waziri Mkuu wa wakati huo, Mohamed Shamte, alikataa ombi la Karume, upo ushahidi kuwa serikali hiyo iliundwa mwaka 1961.
Katika serikali hiyo ya mpito, Karume alipewa na alikubali kupokea nafasi ya uwaziri wa Siha (Afya).
Hii ni ishara tosha kwamba chama cha ASP kiliutambua ushindi wa serikali ya ZNP na ZPPP; hoja inayojitokeza sasa kwamba Zanzibar ilipata uhuru 12 Januari 1964, badala ya 10 Desemba 1963 ni dhaifu na isiyo na mashiko.
Kuna madai pia kwamba Karume hakuwahi kuwa rais wa Zanzibar. hii ni kwa sababu rais huchaguliwa chini ya Katiba; mtu anayeongoza Mapinduzi huitwa “Kiongozi wa Mapinduzi.”
Vilevile, Karume hakuwahi kuchaguliwa hata mara moja na wananchi wa Zanzibar. Pia chini yake, Zanzibar haikuwahi kuwa na katiba.
Kuhusu mapinduzi, Karume mwenyewe aliwahi kukiri kwamba aliondoka Zanzibar mara tu harakati za mapinduzi zilipoanza.
Hatua hiyo inadhihirisha kwamba Karume aliyakimbia mapinduzi hayo. Ni kutokana na kutojua mapema kilichokuwa kikiendelea.
Hizi si taarifa ya uzushi. Ni taarifa sahihi na zinazothibitishwa na mtandao wa Wikipedia Encyclopedia.
Kwa mujibu wa mtandao huo, “Abeid Karume hakuwa Zanzibar usiku ule Mapinduzi yalipofanyika.”
Wengi wanasema Mapinduzi haya yalipangwa na Wakulima, Wakwezi na Wavuvi. Hapana! Mapinduzi yalipangwa na watu wenye kuelewa mambo na wenye ujuzi wa kutosha wa kutumia silaha.
Hawa ni baadhi ya polisi wasio Wazanzibari walioachishwa kazi baada ya uhuru wa Desemba 1963 na kubakia Zanzibar wakiumia kimaisha bila kazi.
Maana kama mapinduzi yalipangwa na wakulima, wavuni na wakwezi, kundi hili lilipata wapi uzoefu wa silaha na mbinu za kivita hata kuteka vituo vya usalama na kupora silaha?
Waliopanga kufanya mapinduzi wanafahamika. Hawa hawakuwa Wazanzibari asilia. Ni pamoja na Field Marshal (John Okello (Mganda) na msaidizi wake, Absalom Anwi Ingen (Mjaluo kutoka Kenya).
Wengine ni Saidi Washoto (Tanganyika) sasa Tanzania Bara, Mohamed Kaujore (Mmakonde wa Msumbiji) na Hamisi Darwesh (Tanganyika).
Walikuwapo pia akina Abdallah Mfaranyaki (Tanganyika), Saidi Natepe (Tanganyika), Seif Bakari (Tanganyika) na Edington Kisasi (Mchaga wa Kilimanjaro-Tanganyika).
Vyombo vya habari navyo vinatoa ushuhuda juu ya nani aliongoza Mapinduzi. Gazeti la serikali ya Tanganyika (The Standard) la 13 Januari 1964, liliandika katika ukurasa wake wa mbele kwamba:
“Wapigania Uhuru waliokuwa na silaha wamekitwaa Kisiwa cha Zanzibar. Wamekamata majengo yote muhimu ya Serikali kwa muda usiozidi saa 24. Usiku Kiongozi wa Mapinduzi alitangaza muundo wa Serikali mpya ya Jamhuri ya Zanzibar na Pemba …”.
Kiongozi huyo alikuwa Okello, ambaye katika tangazo lake la Mapinduzi alipanga Baraza lake la Mawaziri.
Field Marshal John Okello (Waziri wa Ulinzi na Utangazaji na Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi); Sheikh Abeid Amani Karume (Rais wa Serikali ya Mapinduzi) na Kassim Hanga, Makamu wa Rais.
Mawaziri wake walikuwa ni Abdurahman Babu (Ulinzi na Mambo ya Nje), Aboud Jumbe (Afya na Huduma za Jamii) na Othman Sharrif (Elimu).
Okello aliwateua pia Hasnu Mukame kuongoza Wizara ya Kilimo na Idris Abdul-wakili kuongoza Wizara ya Biashara.
Haukupita muda Okello akamtaja Hasnu Makame kuwa Waziri wa Fedha na Salehe Sadallah (Kilimo).
Okello alimaliza kwa kusema, ”Serikali sasa inaendeshwa nasi –Jeshi. Ni juu ya kila raia, mweusi, maji ya kunde au mweupe kutii amri……”.
Gazeti hilo “The Standard,” lilizidi kuthibitisha kuwa Field Marshal amefanya mkutano wake wa kwanza na waandishi wa habari katika ofisi za kurushia matangazo.
Gazeti lilisema, “lundo la bastola lilikuwa mbele ya meza yake. Walinzi wenye silaha mbalimbali walisimama kumzunguka kwa utii na nidhamu….”
“…ni yeye aliyepanga kuiangusha Serikali ya Zanzibar akisaidiwa na Kamati Kuu yake ya watu waliopewa siku 14 tu za mafunzo msituni.”
Ali Muhsin Ali Barwan, aliyekuwepo Zanzibar siku ya Mapinduzi anaeleza katika Kitabu chake “Conflicts and Harmony in Zanzibar,” kwamba “…John Okello, askari mamluki, aliongoza mauaji ya kinyama …. Watu 12,000 walichinjwa…”
Nalo gazeti la The Spectator la nchini Uingereza katika toleo lake la 7 Februari 1964, chini ya makala iliyosema “Gidion’s Voice” pamoja na lile la 12 Februari 1964 “How it Happened”, linaeleza kuwa ni John Gidion Okello aliyeongoza mapinduzi.
Gazeti linafika mbali zaidi na kusema, “ni yeye aliyewavuta wote waliokuja kushirikiana naye katika kutekeleza mapinduzi hayo.”
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haroub Othman (Mzanzibar), katika kitabu kiitwacho, “Mwalimu The Enfluence of Nyerere-Uk 172,” anathibitisha kuwa uhuru wa Zanzibar ulipatikana 10 Desemba 1963.
Anasema Sultan alikuwa Mkuu wa Nchi, na kupewa mamlaka ya kuteuwa mrithi wake. Serikali hiyo ilipinduliwa ndani ya majuma matano tu na “Masiha mjinga,” ambaye ni kiongozi wa wanaharakati John Okello.
Okello alisimika Baraza la Mapinduzi ndani ya kipindi kifupi chini uongozi wa Karume.
Hata Amiri Mohamed anakiri katika kitabu chake “A Guide to a History of Zanzibar” kwamba Okello ndiye aliyetawala Uwanja wa Mapinduzi kwa miezi miwili mfululizo kuanzia 12 Januari 1964 hadi alipokamatwa na kufukuzwa nchini akiwa ziarani Tanganyika. Aliambiwa ni mhamiaji asiyetakiwa visiwani humo.
Anasema ya kuwa Okello akiwa na wapiganaji wapatao 400 aliongoza mashambulizi na baada ya kukamilisha kazi aliendelea kutoa maagizo kupitia kituo cha radio.
Anasema, “ukweli wachunguzi wa mambo ya kisiasa wanaona kuwa Okello ndiye alikuwa rais wa kwanza halali wa Serikali mpya ya Mapinduzi yenye Baraza kamili la Mawaziri.
Hakuna mahali popote wala kumbukumbu za historia, kuonyesha kwamba Abeid Amani Karume aliwahi, katika hatua yeyote ile, kupanga, kuongoza au kushiriki katika Mapinduzi hayo ya 12 Januari 1964.
Sasa kama ni hivyo, kwa nini historia ilipotoshwa na ushiriki wa Okello kutopewa uzito unaostahili?
Jibu linatolewa na Michael F. Lofchie, katika Kitabu chake Was Okello’s Revolution a Consiracy kuanzia uk 36 hadi 42. Anasema, “Okello alifanya Mapinduzi ya Zanzibar…..Njama za kumwondoa Zanzibar ni za kuficha ukweli unaochukiza….”
Kutokana na hali hiyo, majigambo, hila na hadaa za rais wa sasa wa Zanzibar, kwamba baba yake (Abeid Amani Karume), ndiye aliyeendesha mapinduzi hayo, hayana msingi na kuendeleza kuyasikiliza, ni kufinyanga historia.

jmihangwa@yahoo.com. 0713 -526972


ina maana mwandishi hajui wakina okello,natepe, darwesh, mfaranyaki na bakari ni makabila gani? mbona kataja kisasi (mchaga), na kaujore ( mmakonde) na ingen (mjaluo). je kuna kitu anajaribu kuficha hapa au ni mtindo tu wa uandishi? jee mwinyi nae ni mzanzibar? kwani karume tayari inasemekana ni mmalawi.

inakuwaje muandishi autambue uhuru wa 10 disemba 1963 na sultani kama mzanzibar kisha akane uzanzibar wa akina natepe?

naamini kulaani mapinduzi na mauaji yaliyoambatana nayo ni tofauti na kukana uraia wa wahusika wa mapinduzi kwani kwa kufanya hivyo ni sawa na kusema "yale hayakuwa mapinduzi bali ni uvamizi kutoka nje".
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom