Karibu: Chuo cha Maji Ubungo, Dar es Salaam

Karibu: Chuo cha Maji Ubungo, Dar es Salaam

Jombaa hostel ni majanga tu nmewaulza wakuu wanasema huwa inatokea baht kwa watu bachelor kupata hostel....kama vipi ni pm tufanye mchakato wa geto maana hakuna njia nyingine zaid ya kupanga
 
Asanteni Wadau wetu wa Chuo cha Maji kwa maoni na Maswali mbalimbali. Mnaweza kuuliza zaidi maswali hapa tukasaidiana kujibu.
 
Kwa ambae ana soma chuo cha maji tafazali ni txt nikuhoji baazi ya vitu nahitaji kujiunga pale 0767799493
 
Kwa mimi niliesoma HGL nafaa kujiunga hapo chuoni ngazi ya diploma
Tunaangalia matokeo yako ya kidato cha nne na sio cha sita kwa diploma. Mwanafunzi awe na ufahuru wa atleast C moja na D tatu katika masomo ya science ya Physics, Chemistry, Biology, Mathematics na Geography.

Vilevile mwanafunzi asiwe na F ya Mathematics na maelezo kutoka NACTE, mwanafunzi ili ajiunge na Chuo chochote cha Diploma, lazima awe na D nne katika matokeo yake ya kidato cha nne.
 
Mimi sijaelewa jambo dogo tu.
Kiwango gani cha alama kinamwezesha mtu wa kidato cha nne kuanza na diploma moja kwa moja bila kupitia certificate?
 
Hivi kwa nini vyuo vyetu havina Mature Entry? Entry qualifications ni za hovyo hovyo kiasi unajiuliza wanalengwa watoto au watu wote wenye nia ya kujifunza taaluma fulani?

Elimu ya Tanzania inaenda kidagaa dagaa sana
 
hawawezi fanya hivyo coz kiko chini ya wizara i think .by the way tupo pamoja. Mazingira yakoje ?
Mwenzako alikuwa na ndoto za coet akaishia geti maji. Ww unamponda mtu wa BAED UDSM labda katimiza ndoto zake. Hivi wakija udsm students humu si watakuita kilaza wa kiwango cha lami.
 
Harafu ni watu wanaopiga kitabu kweli sio kama UDSM misifa kibao lakin wanaosoma ubungo maji wametulia sana hadi raha kwakweli
Huu uzi sio wa malumbano habari zako za inferiority complex acha kwenu na kama ulikosa nafasi ya UDSM kua mpole
Usichafue uzi wa watu.
 
Mimi sijaelewa jambo dogo tu.
Kiwango gani cha alama kinamwezesha mtu wa kidato cha nne kuanza na diploma moja kwa moja bila kupitia certificate?

Asante kwa Swali.
Diploma ya Chuo cha Maji ni ya Miaka Mitatu.
Mwaka wa Kwanza ni Certificate.
Mwaka wa Pili na wa Tatu ndio Diploma.

Huwezi kuanza moja kwa moja mwaka wa pili na watu, kwasababu kunabaadhi ya modules foundations zake zinatengenezwa kutokea mwaka wa kwanza.

Kwa maelezo zaidi tafadhali fika Chuoni au wasiliana nasi kwa namba za simu tajwa hapo juu. Asante.
 
Tunaangalia matokeo yako ya kidato cha nne na sio cha sita kwa diploma. Mwanafunzi awe na ufahuru wa atleast C moja na D tatu katika masomo ya science ya Physics, Chemistry, Biology, Mathematics na Geography.

Vilevile mwanafunzi asiwe na F ya Mathematics na maelezo kutoka NACTE, mwanafunzi ili ajiunge na Chuo chochote cha Diploma, lazima awe na D nne katika matokeo yake ya kidato cha nne.
Matokeo yang kidato cha nne ni haya
Geog C
Hist C
Maths D
Biology C
Engliash D
Civics D
Kiswahili C
Naweza kusoma chuo cha maji
Na je ada kwa masomo ya diploma ni shilingi ngapi?Na course ni miaka ngapi?
 
Matokeo yang kidato cha nne ni haya
Geog C
Hist C
Maths D
Biology C
Engliash D
Civics D
Kiswahili C
Naweza kusoma chuo cha maji
Na je ada kwa masomo ya diploma ni shilingi ngapi?Na course ni miaka ngapi?

Anaweza kusoma course ya Hydrogeology and Well Drilling au Hydrology and Meteorology.
Ada na michango mingine unaweza kuipata kwa kudownload form katika website ya Chuo.
Course zote ni miaka mitatu.
Asante.
 
Asanteni Wadau wetu wa Chuo cha Maji kwa maoni na Maswali mbalimbali. Mnaweza kuuliza zaidi maswali hapa tukasaidiana kujibu.
Je kwa matokeo haya ya kidato cha NNE naweza kujiunga apo,math C,geo C,bios C,chem D na phyz F, je vigezo vinaniruhusu kujiunga apo?????
 
Je kwa matokeo haya ya kidato cha NNE naweza kujiunga apo,math C,geo C,bios C,chem D na phyz F, je vigezo vinaniruhusu kujiunga apo?????
Na pia ni course ipi kwa apo ingenifaa kwa ufaulu huo,kama vigezo ntakuwa navyo mkuu
 
Back
Top Bottom