Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Dah...hebu tupe sayansi yake inafanya vipi? Kadeti
 
Kuna jamaa yangu alikuwa kampuni moja ya ulinzi, kila asubuhi akirudi anakuta jamaa wameiba hata suruari,

Akawa anaweka umeme 'live wire' kwenye nondo kwa ndani.

Tangu siku alipokuta yebo yebo dirishani hiyo tabia iliisha hapo.
Ila mwanaume haipaswi kulala fofofo hadi asubuhi. Dawa ya hao vibaka ukiwakamata ni kuwafanyia tohara.
 
Ni shida sana, hata goba nilisikia kuna huu wizi. Inabidi mtu uingie gharama kubwa kulinda mali za ndani, magrill, fence, security guards nk. na vitu vyenyewe unavyolinda humo ndani ni TV, simu na laptop ambavyo havifiki hata milioni mbili. Kama ni umaskini wa watu basi umepindukia, yaani unatumia nguvu kuvunja nyumba ya mtu ili uibe TV ya laki tano!??
 
Na raha ya grili moto utokee na uanzie mlangoni.
 
Huu wizi umerudi tena hapa mjini.

Juzi kati jamaa zangu wa Mbezi kwa msuguli. Juzi kati jamaa zangu wa makuburi external waliibiwa TV, laptops, simu n.k.

Kuna namna tunatakiwa tufanye hapa Dar.

Mwenye dawa ya hawa wahuni ailete hapa.
 
Wanaiba smart phone? Hao wezi ni mafala tu na nyie mlioibiwa nina mashaka na elimu zenu
 
Poleni! hakuna hata nyumba ya mchawi mmoja au mwenye CCTV mtaan kwenu ? akawaokoa? ila nishajizoesha kuficha kila kitu uvunguni tangu niibiwe kwa style hiyo
Nabii Tito pia anaishi Sinza.
 
Poleni! hakuna hata nyumba ya mchawi mmoja au mwenye CCTV mtaan kwenu ? akawaokoa? ila nishajizoesha kuficha kila kitu uvunguni tangu niibiwe kwa style hiyo
CCTV kuna nyumba ilikuwa nazo, lakini imeshindwa kutambua sura kwa maana ilikuwa usiku.
 
Karibu na dirishani funga kamba nyembamba mfano wa Uzi ,harafu kaifunge kwenye chumba kama tatu,ambazo umeziweka juu ya kitu kamba ikiguswa chupa zinaanguka
 

Vipi wewe Mwerevu ,ambaye utajenga kwa mujibu Mawazo yako bila kuzingatia athari za Moto zikitokea atapona mtu kweli ndani ya hiyo Nyumba .
 
Kuna siku nilikuwa nimelala usiku kama wa saa saba hivi mara nikasikia kitu kama kina pekenya pekenya hivi,nikashtuka nikaona fimbo ndefu imepenyezwa dirishani imeitoa suruali kwenye enka ya nguo naiona inavutwa ili ityokee dirishani basi na mimi katika hali ya mshangao na ule usingizi nikairukia ile suruali.kumbe kwenye ile fimbo kwa mbele kule nchani wamechomeka kitu kama ndoano ili kunasia nguo,ikanichoma tukawa tunavutana lakini nilifanikiwa kuiokoa suruali yangu.baada ya hapo sikupata usingizi tena hadi asubuhi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…