Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

JF kuna wapumbavu wengi kweli, mada serious watu wanachangia ujinga hadi kero

Dawa ya kudhibiti wezi kama hao ni kuweka zile chuma za dirishani zikiwa zimebanana tu ili asiweze kupitisha simu

Madirisha mengi yana ma grill yenye nafasi kubwa sana na mengine hayana kabisa,
Inabidi kubadili staili ya ujengaji wa nyumba kukabiliana na hatari hii
Na ikitokea dharura ya moto sijui utaokokaje hapo..
 
Ipo siku mtapewa kesi ya mauaji mkafungwa maisha au kunyongwa
Wajanja mnaibiwaje kijinga hivyo? Sinza kw wajanja eeh.
Poleni.
Huku kwetu tukimjua mwizi, tunamkaushia mpaka weekend siku tunajua kila mtu yuko nyumbani. Tunaenda kamata chukua mpaka kwenye open space kisha tairi linamuhusu. Kila mtu aone.
Tun zero tolerance.
 
Kuna jamaa yangu alikuwa kampuni moja ya ulinzi, kila asubuhi akirudi anakuta jamaa wameiba hata suruari,

Akawa anaweka umeme 'live wire' kwenye nondo kwa ndani.

Tangu siku alipokuta yebo yebo dirishani hiyo tabia iliisha hapo.
 
Sinza A ipo usawa upi?
Leo imekuwa ni vilio na hamaki kwa raia wa hapa Sinza A, baada ya kuamka asubuhi na kukuta madirisha yao yametobolewa na kukatwa kwa nyavu.

Inasemekana, walipuliza dawa ya usingizi ndipo wakafanya unyama huo. Watu wameibiwa pesa, laptops, simu, vitu vya ndani kibao.

Hapo unapoishi, kuna wizi wowote umefanyika?

Anayejua jinsi ya kujikinga na hiyo sawa, atupe elimu hapa.

Poleni wahanga wote wa wizi huo.

Nawasilisha!
 
Poleni sana.

Marekebisho kwenye fasihi sio KUIBIWA kwa muktadha wa habari yako ni KUIBWA.
 
Dawa ni kutoweka vitu vya thamani karibu na madirisha..
Niliwahi ibiwa simu 2010 kwa staili, mpaka leo huwa siachi simu kizembe zembe!
 
Kiboko yao ni kuFunga system ya Intruder Alarm kutoka KK Security / Gardaworld, ukipuliza dawa System hailali, hii inafungwa nchi nzima na unaweza kuchagua system itume sms kwenye simu ya watu wako wakaribu kadhaa, pia kwa ulinzi kamili ni kuunganisha system hiyo na control Room yetu ili pindi king'ora kinapolia wanatuma gari yenye Askari wa KK/Gardaworld kwaajili yakuangalia usalama kwenye eneo lako, inafungwa maofisini,nyumbani na pia inaweza kuunganishwa kwenye electricic fence yako. Wasiliana nami kwa WhatsApp number 0743171049 au email victor.valence@garda.com Nchi nzima.
Hii ndio suluhisho sahihi. Tatizo watanzania bado tunaishi kizamani mtu unaibiwa kitu halafu bado eti unauliza "nifanye nini" hivi ni kweli kwmb hujui cha kufanya?
 
Ma-grill ya namna hiyo sikushauri hata kidogo uyaweke likitokea lakutokea hatoki hata mmoja wenu mtakauka humohumo!

Mfano moto umetokea (God forbid) milango huwa inatabia ya kujikaza na mara nyingi huwa inakimbilia mahala unakoweza kutokea ndipo utawaka sana ni kama huwa inatumwa huko kwenye Grill's ndo hutashika kabisa.

Ushauri wangu weka Grills pana kiasi likitokea jambo ukivunja kichuma kimoja basi nafasi pana inapatikana kwa wewe ama yeyote kutoka nje
grill pana inawashawishi wezi wapate tamaa ya kuiba mpaka sofa
 
Leo imekuwa ni vilio na hamaki kwa raia wa hapa Sinza A, baada ya kuamka asubuhi na kukuta madirisha yao yametobolewa na kukatwa kwa nyavu.

Inasemekana, walipuliza dawa ya usingizi ndipo wakafanya unyama huo. Watu wameibiwa pesa, laptops, simu, vitu vya ndani kibao.

Hapo unapoishi, kuna wizi wowote umefanyika?

Anayejua jinsi ya kujikinga na hiyo sawa, atupe elimu hapa.

Poleni wahanga wote wa wizi huo.

Nawasilisha!
dar es salaam bwana!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom