Kunguru Mjanja
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 2,036
- 3,929
Wakati homa ya mchezo wa Watani wa Jadi, Simba na Yanga ikiendelea kupanda huku zikiwa zimebaki saa chache, Mashabiki na Wachezaji wa timu hizo wameendelea kutambiana kuibuka na ushindi
Simba ambayo itakuwa mwenyeji, itaikaribisha Yanga katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar leo majira ya saa 11:00 jioni
Takwimu za timu hizo zinaonyesha safu zao za ushambuliaji zimekuwa na makali dakika 45 za kipindi cha pili ingawa Simba inaonyesha iko vizuri pia dakika 45 za mwanzo
Simba katika mechi 10 zilizopita imefunga magoli 10 kipindi cha pili na katika kipindi cha kwanza imefunga magoli 10 huku ikiruhusu goli moja katika kipindi hicho cha kwanza
Yanga nayo imekuwa moto kipindi cha pili kwa kufunga magoli 8 lakini imeruhuru magoli matano na katika Kipindi cha kwanza imefunga magoli 6 na kuruhusu kufungwa magoli matatu
Nitakuwa nikiweka hapa yanayojiri yote moja kwa moja kutoka Taifa-Jijini Dar
UPDATES
Mwamuzi wa Mchezo wa leo ni Mwana Mama, Jonesia Rukyaa
Mashabiki wa timu zote mbili wameanza kuingia uwanjani huku mchezo huo ukitarajiwa kuanza majira ya saa 11:00 jioni
Baadhi ya Mashabiki wa Yanga Wakiwa ndani ya Uwanja tayari
UPDATE YA VIKOSI
Kikosi cha Simba kitakachopambana na Yanga leo Januari 04
Kikosi cha Yanga dhidi ya Simba leo Januari 04
Simba inapata goli la kuongoza kupitia kwa Meddie Kagere
Klabu ya Simba inapata goli la kuongoza dhidi ya Klabu ya Yanga kupitia goli lililofungwa na Meddie Kagere katika dakika ya 42
Goli la Simba limepatikana kupitia mkwaju wa penati baada ya Meddie Kagere kuchezewa rafu na Beki Kelvin Yondani ndani ya eneo la hatari
======
MICHEZO: Klabu za Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika Uwanja wa Taifa jijini Dar baada ya timu hizo kutoka sare ya goli 2-2 katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara
Simba inapata goli la kuongoza kupitia penati ya Meddie Kagere katika dakika ya 42 na goli la pili la Simba lilitungwa na Deo Kanda katika dakika ya 47
Goli la Kwanza la Yanga lilifungwa na Balama Mapinduzi katika dakika ya 50 huku goli lake la pili likipatikana baada Mohamed Hussein kujifunga katika dakika ya 53
Simba ambayo itakuwa mwenyeji, itaikaribisha Yanga katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar leo majira ya saa 11:00 jioni
Takwimu za timu hizo zinaonyesha safu zao za ushambuliaji zimekuwa na makali dakika 45 za kipindi cha pili ingawa Simba inaonyesha iko vizuri pia dakika 45 za mwanzo
Simba katika mechi 10 zilizopita imefunga magoli 10 kipindi cha pili na katika kipindi cha kwanza imefunga magoli 10 huku ikiruhusu goli moja katika kipindi hicho cha kwanza
Yanga nayo imekuwa moto kipindi cha pili kwa kufunga magoli 8 lakini imeruhuru magoli matano na katika Kipindi cha kwanza imefunga magoli 6 na kuruhusu kufungwa magoli matatu
Nitakuwa nikiweka hapa yanayojiri yote moja kwa moja kutoka Taifa-Jijini Dar
UPDATES
Mwamuzi wa Mchezo wa leo ni Mwana Mama, Jonesia Rukyaa
Mashabiki wa timu zote mbili wameanza kuingia uwanjani huku mchezo huo ukitarajiwa kuanza majira ya saa 11:00 jioni
Baadhi ya Mashabiki wa Yanga Wakiwa ndani ya Uwanja tayari
Kikosi cha Simba kitakachopambana na Yanga leo Januari 04
Kikosi cha Yanga dhidi ya Simba leo Januari 04
Simba inapata goli la kuongoza kupitia kwa Meddie Kagere
Goli la Simba limepatikana kupitia mkwaju wa penati baada ya Meddie Kagere kuchezewa rafu na Beki Kelvin Yondani ndani ya eneo la hatari
======
MICHEZO: Klabu za Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika Uwanja wa Taifa jijini Dar baada ya timu hizo kutoka sare ya goli 2-2 katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara
Simba inapata goli la kuongoza kupitia penati ya Meddie Kagere katika dakika ya 42 na goli la pili la Simba lilitungwa na Deo Kanda katika dakika ya 47
Goli la Kwanza la Yanga lilifungwa na Balama Mapinduzi katika dakika ya 50 huku goli lake la pili likipatikana baada Mohamed Hussein kujifunga katika dakika ya 53