Kariakoo Derby: Simba SC 2 - 2 Yanga SC | Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara - Uwanja wa Taifa Dar

Kunguru Mjanja

JF-Expert Member
Aug 22, 2012
2,036
3,929
Wakati homa ya mchezo wa Watani wa Jadi, Simba na Yanga ikiendelea kupanda huku zikiwa zimebaki saa chache, Mashabiki na Wachezaji wa timu hizo wameendelea kutambiana kuibuka na ushindi

Simba ambayo itakuwa mwenyeji, itaikaribisha Yanga katika mchezo wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar leo majira ya saa 11:00 jioni

58D89E3A-FE40-4817-85BB-0035DE2AE94A.jpeg

Takwimu za timu hizo zinaonyesha safu zao za ushambuliaji zimekuwa na makali dakika 45 za kipindi cha pili ingawa Simba inaonyesha iko vizuri pia dakika 45 za mwanzo

Simba katika mechi 10 zilizopita imefunga magoli 10 kipindi cha pili na katika kipindi cha kwanza imefunga magoli 10 huku ikiruhusu goli moja katika kipindi hicho cha kwanza

Yanga nayo imekuwa moto kipindi cha pili kwa kufunga magoli 8 lakini imeruhuru magoli matano na katika Kipindi cha kwanza imefunga magoli 6 na kuruhusu kufungwa magoli matatu

Nitakuwa nikiweka hapa yanayojiri yote moja kwa moja kutoka Taifa-Jijini Dar

UPDATES
96C599EE-9E64-45E2-9DD5-152D05BB09F7.jpeg

Mwamuzi wa Mchezo wa leo ni Mwana Mama, Jonesia Rukyaa

82A39C76-9607-4826-A7C4-B34D6282C803.jpeg

Mashabiki wa timu zote mbili wameanza kuingia uwanjani huku mchezo huo ukitarajiwa kuanza majira ya saa 11:00 jioni

AA6BE1AB-7CE8-428C-90B7-12822AC2BD0E.jpeg

Baadhi ya Mashabiki wa Yanga Wakiwa ndani ya Uwanja tayari
UPDATE YA VIKOSI
8885963C-CDA3-4759-8B7A-842FBC9EFD90.jpeg

Kikosi cha Simba kitakachopambana na Yanga leo Januari 04

A27B928F-9314-40CB-90E2-A2267392B27B.jpeg

Kikosi cha Yanga dhidi ya Simba leo Januari 04​

Simba inapata goli la kuongoza kupitia kwa Meddie Kagere
424272F7-C810-43BC-B245-7A9BB70907A6.png
Klabu ya Simba inapata goli la kuongoza dhidi ya Klabu ya Yanga kupitia goli lililofungwa na Meddie Kagere katika dakika ya 42

Goli la Simba limepatikana kupitia mkwaju wa penati baada ya Meddie Kagere kuchezewa rafu na Beki Kelvin Yondani ndani ya eneo la hatari


======

MICHEZO: Klabu za Simba na Yanga zimeshindwa kutambiana katika Uwanja wa Taifa jijini Dar baada ya timu hizo kutoka sare ya goli 2-2 katika Mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara

Simba inapata goli la kuongoza kupitia penati ya Meddie Kagere katika dakika ya 42 na goli la pili la Simba lilitungwa na Deo Kanda katika dakika ya 47

Goli la Kwanza la Yanga lilifungwa na Balama Mapinduzi katika dakika ya 50 huku goli lake la pili likipatikana baada Mohamed Hussein kujifunga katika dakika ya 53
IMG_20200104_190541_049.jpg

azamtvtz_20200104_7.jpg
 
Kukosekana kwa Lamini Moro kunatoa nafasi kubwa beki mgumu Ali Sonzo kuanza mechi ya leo. Je hii itakua na maana ktk mechi hii muhimu? Nitaeleza mapungufu ya Ali Zonzo na baadhi ya wachezaji wa Yanga ambao wasipokua makini leo ni hstari kubwa kwa Yanga.

Ali Sonzo: Control sebule nzima, hana utulivu na anabutua sn mpira bila kujali anampa nani. Hali hii ni hatari sn kwa Simba ambao bila shaka watajaza viungo wao mafundi hivyo itasababisha Simba kushinda golini kwa Yanga mda wote.

Shishimbi: Anipaga pasi mkaa nyingi na kupoteza mpira kirahisi sn. Ni mkabaji mzuri sn japo ni rahisi kupewa kadi. Kuna huwa anapoteza mipira eneo lake hatari hivyo lazma kocha amtaharishe mapema la sivyo atachomesha.
Makame: Huyu ni kumba kumba. Aspokua makini red cad itamhusu. Nae hana umiliki mzuri wa mpira.

Kaseke: Mara nyingi anashindwa kumiliki pasi anayopewa na hivyo kupelekea mpira kutoka nje kirahisi kabsa. Pasi na krosi zake nyingi hazina macho. Control yake pia si nzuri, anatatizo la kukosa umakini anapokaribia goli. Mashuti yake mengi hayana target. Kuna muda huwa anakua mchoyo au anachelewa kutoa pasi bila sababu.

Molinga: Huyu ningekua kocha nisingempa nafasi ya kuanza kutokana na tatizo lake la uzito ns kukusa flexibility. Ieweleke kuwa Simba ina wachezaji wengi wajanja na wanyumbulifu. Hivyo kuanza na Molinga ni kuanza na mzigo.
Wachezaji wengine wanamapungufu ila wanauwafadhari. Kwa ujumla bado pande za kushoto na kulia hakuko salama sn.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: BDN

Similar Discussions

Back
Top Bottom