Herodi mambo Leo atubu full stopNdiyo maana nasema kumlinganisha msomi wa theology kama Pengo na Kakobe kwadababu kawafurahisha ama kasema kile watu wanataka kukisikia bila kuweka uwiano na siku yenyewe ni kutokujua.
Pengo ni mtu makini sana katika homily zake.
Nyinyi wenye akili uwa mnasikilizaga kakobe tuu?
naona umetumwa kuanzisha hoja za kidini na si vyema sana kukashifu vitabu vitakatifu ukitaka kuelewa vzur usome na historia ya watawala wa kipindi hicho sio unaongea bila fact..Akisema Herode pia ndiye Yule aliyemuua YOHANA MBATIZAJI baada ya kumueleza ukweli mfalme HERODE????
JE WANA UHUSIANO AU HUYU NI HERODE MWINGINE ANAYEMAANISHWA KATIKA MAHUBIRI HAYA??
AMA KWELI BIBLE NI MPYA KILA SIKU.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania kama sehemu ya utamaduni wake, Alhamisi tarehe 28 Desemba 2017 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa la Parokia ya Msimbazi, kwa ajili ya Watoto wa Utoto Mtakatifu Jimbo kuu la Dar es Salaam.
Maandiko Matakatifu yanasema kwamba, sauti ilisikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako!
Mfalme Herode alisababisha maafa na msiba mkubwa; kilio na majonzi kwa watu wake. Aliwauwa watoto ili kulinda na kudumisha Ufalme wake. Alihofia uwepo wa Kristo Yesu, akamtafuta kwa udi na uvumba, lakini hakufanikiwa kumpata.
Kardinali Pengo anaendelea kufafanua kwamba, katika tukio hili, Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu wanaonesha jinsi ambavyo walijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao, wakajisadaka kwa ajili ya usalama na tunza ya mtoto wao mchanga kiasi hata cha kukimbilia uhamishoni Misri.
Kwa upande mwingine, kuna Mfalme Herode aliyezua msiba mkubwa, mateso na huzuni, kwa kuwatoa watoto kafara ili aweze kutawala.
Anasema, hata leo hii, bado akina Herode wamo katika ulimwengu mamboleo. Hawa ni baa la njaa, umaskini na ujinga. Kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa vile tu ni watoto yatima!
Lakini pia kuna watoto wanaofanyishwa kazi za suluba na hata wakati mwingine kutumbukizwa katika mazingira hatarishi kama chambo cha uchumi wa familia au kwa baadhi ya watu waliokengeuka ambao hata wakati mwingine wanawajeruhi watoto wao ili waweze kuwatumbukiza katika biashara ya omba omba mitaani badala ya kwenda shule!
Kuna watoto wanaotolewa mimba hata kabla ya kuzaliwa, hivi ni vitendo vinavyofanywa na watu wakatili.
Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, amewataka watoto kusali kwa ajili ya kuwaombea akina Herode mamboleo ili waweze kutubu na kumwongokea Mungu kwa kusimama kidete kutetea Injili ya uhai tangu pale mtoto anapotunga mimba tumboni mwa mama yake, hadi mauti ya kawaida inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu!
Amewataka wazazi na walezi kuwajengea watoto wao mazingira bora zaidi yatakayowawezesha kuwa ni mashuhuda amini wa Mtoto Yesu katika maisha yao. Waamini washinde ubinafsi kwa kuongozwa na upendo wa Mungu kwa ajili ya maskini na wahitaji zaidi.
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi kusali kwa ajili ya kuwaombea watoto wanaoteseka sehemu mbali mbali kwa kutolewa mimba kabla hawajazaliwa; kwa kuteseka kutokana na baa la njaa na magonjwa na wale ambao wanabebeshwa silaha na kutumwa mstari wa mbele kama chambo kwenye mapigano.
Huu ni ujumbe makini kabisa unaotolewa na Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 28 Desemba 2017, Mama Kanisa anapoadhimisha Siku kuu ya Watoto Mashahidi waliouwawa na Mfalme Herode kwa hofu ya kupoteza kiti chake za kifalme, baada ya kuambiwa kwamba, Kristo Yesu, Mfalme wa Mataifa amezaliwa mjini Bethlehemu.
Tangu mwanzo, Mama Kanisa amewaangalia watoto hawa kama mashuhuda wa Fumbo la Umwilisho, watoto ambao hata kama hawakumwona Kristo Yesu, lakini walibahatika kupata Ubatizo wa Damu, kumbe, wao ni mashuhuda wa Kristo kwa njia ya sadaka ya maisha yao.
Mama Kanisa daima anafundisha kwamba, kifodini ni sadaka kubwa ambayo Mwenyezi Mungu hupenda kuwakirimia waja wake.
Siku kuu ya Watoto mashahidi wa imani ilianza kuadhimishwa kunako karne ya tano. Watoto hawa wanafuatana na mashuhuda wa imani kama Stefano shahidi na Mwinjili Yohane ambao daima wamekuwa mstari wa mbele kusimamia imani, utu na heshima ya binadamu.
Wakati huo huo , Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF linasema, Mwaka 2017 umeshuhudia idadi kubwa ya watoto duniani, ikikabiliwa na mashambulizi mbali mbali hasa huko Iraq, Siria, Yemen, Nigeria, Sudan ya Kusini na Myanmar, maeneo ambayo pia yametajwa na Baba Mtakatifu Francisko wakati akitoa ujumbe wa Noeli kwa Mwaka 2017 kwa ajili ya mji wa Roma na Ulimwengu katika ujumla wake, maarufu kama “Urbi et Orbi ”.
Huko nchini Nigeria na Cameroon, Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram kimefanya mauaji ya watoto 135. Huko DRC, watoto 850 wamelazimika kukimbia makwao. Takwimu zinaonesha kwamba, zaidi ya watoto 350, 000 wanakabiliwa na utapia mlo wa kutisha.
Hali ya maisha ya watoto Sudan ya Kusini ni mbaya sana kutokana na vita, njaa na utapiamlo wa kutisha. Zaidi ya watoto 19, 000 wamelazimishwa kwenda kupigana mstari wa mbele kama chambo na kwamba, zaidi ya watoto 2, 300 wameuwawa kikatili tangu vita ya wenyewe kwa wenyewe ifumuke upya nchini humo kunako mwaka 2013. Nchini Somalia zaidi ya watoto 1, 740 wameingizwa kwenye vikosi vya kijeshi na kupelekwa mstari wa mbele! UNICEF inawataka wadau mbali mbali kushikamana katika kuwahudumia watoto, ili waweze kupata chakula na lishe bora; elimu, malezi; ulinzi na usalama, ili waweze kufurahia maisha ya utoto wao!
Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.
Vatican News!
My take: asante sana baba mwadhama kwa tafakari ya kimataifa.
Ni wachache sana wanaomwelewaNdiyo maana nasema kumlinganisha msomi wa theology kama Pengo na Kakobe kwadababu kawafurahisha ama kasema kile watu wanataka kukisikia bila kuweka uwiano na siku yenyewe ni kutokujua.
Pengo ni mtu makini sana katika homily zake.
Nilitaka kuandika Neno zito la karne kwa huyo "Pango" sema nimekumbuka kuna Ban humu Jf
MwalimumkuumamayakoWapi nimeandika nina msikiliza kakobe? Kama una washwa sema ukunwe dada.
Si lazima aongelee hayo mambo kila mara. Ameongea kutokana na maudhui ya siku husika. Kila tarehe 28 Desemba 2017 huwa anaadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya Watoto wa Utoto Mtakatifu, Jimbo kuu la Dar es Salaam.ameandika nini kisichojulikana. haya ni mastory ya siku zote, miaka yote, karne zote. Sidhani kama ana reflection ya kinachoendelea hapa kuwa akina Ben wamepotezwa na mtu kulinda ufalme wake, NEVER!
Ni vigumu kumwelewa kama hufahamu staili ya mahubiri yake. Mara nyingi huwa anachohubiri ni kama vile anatafsiri kutoka katika lugha fulani ya kigeni. Huwa napenda sana staili yake.Mimi sijamwelewa Pengo kabisaa
zero brain mama yakoUna ushahidi?....nyie ndo walewale mkiitwa kutoa ushahidi mnasema..... nilisoma kwenye social media....zero brain
Acheni hizo, Kardinali Pengo hawezi kuwa mtegemezi hivyo wakati Jimbo analoongoza linatoa ruzuku nyingi tu sehemu nyingine za ukatoliki kutokana na kuwa na rasilimali za kutosha ikiwemo watu. Msidhani Pengo huwa anaongea yale kwa njaa njaa, ana maana yake ambayo pengine si lazima watu waijue, maana unaweza ukaweka vitu hadhharani ukasababisha vuruguPengo ashanogewa breakfast ya ikulu aha