Kardinali Pengo asema bado kuna akina Herode uchwara duniani!

Gerasmus

JF-Expert Member
May 23, 2016
400
341
Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania kama sehemu ya utamaduni wake, Alhamisi tarehe 28 Desemba 2017 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa la Parokia ya Msimbazi, kwa ajili ya Watoto wa Utoto Mtakatifu Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Maandiko Matakatifu yanasema kwamba, sauti ilisikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako!

Mfalme Herode alisababisha maafa na msiba mkubwa; kilio na majonzi kwa watu wake. Aliwauwa watoto ili kulinda na kudumisha Ufalme wake. Alihofia uwepo wa Kristo Yesu, akamtafuta kwa udi na uvumba, lakini hakufanikiwa kumpata.


Kardinali Pengo anaendelea kufafanua kwamba, katika tukio hili, Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu wanaonesha jinsi ambavyo walijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao, wakajisadaka kwa ajili ya usalama na tunza ya mtoto wao mchanga kiasi hata cha kukimbilia uhamishoni Misri.

Kwa upande mwingine, kuna Mfalme Herode aliyezua msiba mkubwa, mateso na huzuni, kwa kuwatoa watoto kafara ili aweze kutawala.

Anasema, hata leo hii, bado akina Herode wamo katika ulimwengu mamboleo. Hawa ni baa la njaa, umaskini na ujinga. Kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa vile tu ni watoto yatima!

Lakini pia kuna watoto wanaofanyishwa kazi za suluba na hata wakati mwingine kutumbukizwa katika mazingira hatarishi kama chambo cha uchumi wa familia au kwa baadhi ya watu waliokengeuka ambao hata wakati mwingine wanawajeruhi watoto wao ili waweze kuwatumbukiza katika biashara ya omba omba mitaani badala ya kwenda shule!

Kuna watoto wanaotolewa mimba hata kabla ya kuzaliwa, hivi ni vitendo vinavyofanywa na watu wakatili.


Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, amewataka watoto kusali kwa ajili ya kuwaombea akina Herode mamboleo ili waweze kutubu na kumwongokea Mungu kwa kusimama kidete kutetea Injili ya uhai tangu pale mtoto anapotunga mimba tumboni mwa mama yake, hadi mauti ya kawaida inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu!


Amewataka wazazi na walezi kuwajengea watoto wao mazingira bora zaidi yatakayowawezesha kuwa ni mashuhuda amini wa Mtoto Yesu katika maisha yao. Waamini washinde ubinafsi kwa kuongozwa na upendo wa Mungu kwa ajili ya maskini na wahitaji zaidi.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi kusali kwa ajili ya kuwaombea watoto wanaoteseka sehemu mbali mbali kwa kutolewa mimba kabla hawajazaliwa; kwa kuteseka kutokana na baa la njaa na magonjwa na wale ambao wanabebeshwa silaha na kutumwa mstari wa mbele kama chambo kwenye mapigano.

Huu ni ujumbe makini kabisa unaotolewa na Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 28 Desemba 2017, Mama Kanisa anapoadhimisha Siku kuu ya Watoto Mashahidi waliouwawa na Mfalme Herode kwa hofu ya kupoteza kiti chake za kifalme, baada ya kuambiwa kwamba, Kristo Yesu, Mfalme wa Mataifa amezaliwa mjini Bethlehemu.

Tangu mwanzo, Mama Kanisa amewaangalia watoto hawa kama mashuhuda wa Fumbo la Umwilisho, watoto ambao hata kama hawakumwona Kristo Yesu, lakini walibahatika kupata Ubatizo wa Damu, kumbe, wao ni mashuhuda wa Kristo kwa njia ya sadaka ya maisha yao.

Mama Kanisa daima anafundisha kwamba, kifodini ni sadaka kubwa ambayo Mwenyezi Mungu hupenda kuwakirimia waja wake.

Siku kuu ya Watoto mashahidi wa imani ilianza kuadhimishwa kunako karne ya tano. Watoto hawa wanafuatana na mashuhuda wa imani kama Stefano shahidi na Mwinjili Yohane ambao daima wamekuwa mstari wa mbele kusimamia imani, utu na heshima ya binadamu.


Wakati huo huo , Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF linasema, Mwaka 2017 umeshuhudia idadi kubwa ya watoto duniani, ikikabiliwa na mashambulizi mbali mbali hasa huko Iraq, Siria, Yemen, Nigeria, Sudan ya Kusini na Myanmar, maeneo ambayo pia yametajwa na Baba Mtakatifu Francisko wakati akitoa ujumbe wa Noeli kwa Mwaka 2017 kwa ajili ya mji wa Roma na Ulimwengu katika ujumla wake, maarufu kama “Urbi et Orbi ”.

Huko nchini Nigeria na Cameroon, Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram kimefanya mauaji ya watoto 135. Huko DRC, watoto 850 wamelazimika kukimbia makwao. Takwimu zinaonesha kwamba, zaidi ya watoto 350, 000 wanakabiliwa na utapia mlo wa kutisha.
Hali ya maisha ya watoto Sudan ya Kusini ni mbaya sana kutokana na vita, njaa na utapiamlo wa kutisha. Zaidi ya watoto 19, 000 wamelazimishwa kwenda kupigana mstari wa mbele kama chambo na kwamba, zaidi ya watoto 2, 300 wameuwawa kikatili tangu vita ya wenyewe kwa wenyewe ifumuke upya nchini humo kunako mwaka 2013. Nchini Somalia zaidi ya watoto 1, 740 wameingizwa kwenye vikosi vya kijeshi na kupelekwa mstari wa mbele! UNICEF inawataka wadau mbali mbali kushikamana katika kuwahudumia watoto, ili waweze kupata chakula na lishe bora; elimu, malezi; ulinzi na usalama, ili waweze kufurahia maisha ya utoto wao!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.

Vatican News!

My take: asante sana baba mwadhama kwa tafakari ya kimataifa.
 
Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania kama sehemu ya utamaduni wake, Alhamisi tarehe 28 Desemba 2017 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa la Parokia ya Msimbazi, kwa ajili ya Watoto wa Utoto Mtakatifu Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Maandiko Matakatifu yanasema kwamba, sauti ilisikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako!

Mfalme Herode alisababisha maafa na msiba mkubwa; kilio na majonzi kwa watu wake. Aliwauwa watoto ili kulinda na kudumisha Ufalme wake. Alihofia uwepo wa Kristo Yesu, akamtafuta kwa udi na uvumba, lakini hakufanikiwa kumpata.


Kardinali Pengo anaendelea kufafanua kwamba, katika tukio hili, Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu wanaonesha jinsi ambavyo walijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao, wakajisadaka kwa ajili ya usalama na tunza ya mtoto wao mchanga kiasi hata cha kukimbilia uhamishoni Misri.

Kwa upande mwingine, kuna Mfalme Herode aliyezua msiba mkubwa, mateso na huzuni, kwa kuwatoa watoto kafara ili aweze kutawala.

Anasema, hata leo hii, bado akina Herode wamo katika ulimwengu mamboleo. Hawa ni baa la njaa, umaskini na ujinga. Kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa vile tu ni watoto yatima!

Lakini pia kuna watoto wanaofanyishwa kazi za suluba na hata wakati mwingine kutumbukizwa katika mazingira hatarishi kama chambo cha uchumi wa familia au kwa baadhi ya watu waliokengeuka ambao hata wakati mwingine wanawajeruhi watoto wao ili waweze kuwatumbukiza katika biashara ya omba omba mitaani badala ya kwenda shule!

Kuna watoto wanaotolewa mimba hata kabla ya kuzaliwa, hivi ni vitendo vinavyofanywa na watu wakatili.


Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, amewataka watoto kusali kwa ajili ya kuwaombea akina Herode mamboleo ili waweze kutubu na kumwongokea Mungu kwa kusimama kidete kutetea Injili ya uhai tangu pale mtoto anapotunga mimba tumboni mwa mama yake, hadi mauti ya kawaida inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu!


Amewataka wazazi na walezi kuwajengea watoto wao mazingira bora zaidi yatakayowawezesha kuwa ni mashuhuda amini wa Mtoto Yesu katika maisha yao. Waamini washinde ubinafsi kwa kuongozwa na upendo wa Mungu kwa ajili ya maskini na wahitaji zaidi.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi kusali kwa ajili ya kuwaombea watoto wanaoteseka sehemu mbali mbali kwa kutolewa mimba kabla hawajazaliwa; kwa kuteseka kutokana na baa la njaa na magonjwa na wale ambao wanabebeshwa silaha na kutumwa mstari wa mbele kama chambo kwenye mapigano.

Huu ni ujumbe makini kabisa unaotolewa na Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 28 Desemba 2017, Mama Kanisa anapoadhimisha Siku kuu ya Watoto Mashahidi waliouwawa na Mfalme Herode kwa hofu ya kupoteza kiti chake za kifalme, baada ya kuambiwa kwamba, Kristo Yesu, Mfalme wa Mataifa amezaliwa mjini Bethlehemu.

Tangu mwanzo, Mama Kanisa amewaangalia watoto hawa kama mashuhuda wa Fumbo la Umwilisho, watoto ambao hata kama hawakumwona Kristo Yesu, lakini walibahatika kupata Ubatizo wa Damu, kumbe, wao ni mashuhuda wa Kristo kwa njia ya sadaka ya maisha yao.

Mama Kanisa daima anafundisha kwamba, kifodini ni sadaka kubwa ambayo Mwenyezi Mungu hupenda kuwakirimia waja wake.

Siku kuu ya Watoto mashahidi wa imani ilianza kuadhimishwa kunako karne ya tano. Watoto hawa wanafuatana na mashuhuda wa imani kama Stefano shahidi na Mwinjili Yohane ambao daima wamekuwa mstari wa mbele kusimamia imani, utu na heshima ya binadamu.


Wakati huo huo , Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF linasema, Mwaka 2017 umeshuhudia idadi kubwa ya watoto duniani, ikikabiliwa na mashambulizi mbali mbali hasa huko Iraq, Siria, Yemen, Nigeria, Sudan ya Kusini na Myanmar, maeneo ambayo pia yametajwa na Baba Mtakatifu Francisko wakati akitoa ujumbe wa Noeli kwa Mwaka 2017 kwa ajili ya mji wa Roma na Ulimwengu katika ujumla wake, maarufu kama “Urbi et Orbi ”.

Huko nchini Nigeria na Cameroon, Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram kimefanya mauaji ya watoto 135. Huko DRC, watoto 850 wamelazimika kukimbia makwao. Takwimu zinaonesha kwamba, zaidi ya watoto 350, 000 wanakabiliwa na utapia mlo wa kutisha.
Hali ya maisha ya watoto Sudan ya Kusini ni mbaya sana kutokana na vita, njaa na utapiamlo wa kutisha. Zaidi ya watoto 19, 000 wamelazimishwa kwenda kupigana mstari wa mbele kama chambo na kwamba, zaidi ya watoto 2, 300 wameuwawa kikatili tangu vita ya wenyewe kwa wenyewe ifumuke upya nchini humo kunako mwaka 2013. Nchini Somalia zaidi ya watoto 1, 740 wameingizwa kwenye vikosi vya kijeshi na kupelekwa mstari wa mbele! UNICEF inawataka wadau mbali mbali kushikamana katika kuwahudumia watoto, ili waweze kupata chakula na lishe bora; elimu, malezi; ulinzi na usalama, ili waweze kufurahia maisha ya utoto wao!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.

Vatican News!

My take: asante sana baba mwadhama kwa tafakari ya kimataifa.
Ndiyo maana nasema kumlinganisha msomi wa theology kama Pengo na Kakobe kwadababu kawafurahisha ama kasema kile watu wanataka kukisikia bila kuweka uwiano na siku yenyewe ni kutokujua.
Pengo ni mtu makini sana katika homily zake.
 
Ndiyo maana nasema kumlinganisha msomi wa theology kama Pengo na Kakobe kwadababu kawafurahisha ama kasema kile watu wanataka kukisikia bila kuweka uwiano na siku yenyewe ni kutokujua.
Pengo ni mtu makini sana katika homily zake.
ameandika nini kisichojulikana. haya ni mastory ya siku zote, miaka yote, karne zote. Sidhani kama ana reflection ya kinachoendelea hapa kuwa akina Ben wamepotezwa na mtu kulinda ufalme wake, NEVER!
 
Baba askofu ananifungia mwaka kwa amani kabisa. Kwa kweli abalikiwe.
Japo Wafuasi wa CCM. Hawataki kukubali ukweli. Askofu yuko Sahihi.
 
ameandika nini kisichojulikana. haya ni mastory ya siku zote, miaka yote, karne zote. Sidhani kama ana reflection ya kinachoendelea hapa kuwa akina Ben wamepotezwa na mtu kulinda ufalme wake, NEVER!
Hata kina mbowe hawakuzungumza juu ya ben mpaka ndugu zake. Kwanini unadhani matendo mabaya yanatendwa kwa wapinzani tu. Si ninyi mlinyamaza wakati wa kibiti? Unataka Pengo aongee nini kuhusu ben?
 
Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania kama sehemu ya utamaduni wake, Alhamisi tarehe 28 Desemba 2017 ameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwenye Kanisa la Parokia ya Msimbazi, kwa ajili ya Watoto wa Utoto Mtakatifu Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Maandiko Matakatifu yanasema kwamba, sauti ilisikiwa Rama, kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako!

Mfalme Herode alisababisha maafa na msiba mkubwa; kilio na majonzi kwa watu wake. Aliwauwa watoto ili kulinda na kudumisha Ufalme wake. Alihofia uwepo wa Kristo Yesu, akamtafuta kwa udi na uvumba, lakini hakufanikiwa kumpata.


Kardinali Pengo anaendelea kufafanua kwamba, katika tukio hili, Bikira Maria na Mtakatifu Yosefu wanaonesha jinsi ambavyo walijitahidi kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao, wakajisadaka kwa ajili ya usalama na tunza ya mtoto wao mchanga kiasi hata cha kukimbilia uhamishoni Misri.

Kwa upande mwingine, kuna Mfalme Herode aliyezua msiba mkubwa, mateso na huzuni, kwa kuwatoa watoto kafara ili aweze kutawala.

Anasema, hata leo hii, bado akina Herode wamo katika ulimwengu mamboleo. Hawa ni baa la njaa, umaskini na ujinga. Kuna watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi kwa vile tu ni watoto yatima!

Lakini pia kuna watoto wanaofanyishwa kazi za suluba na hata wakati mwingine kutumbukizwa katika mazingira hatarishi kama chambo cha uchumi wa familia au kwa baadhi ya watu waliokengeuka ambao hata wakati mwingine wanawajeruhi watoto wao ili waweze kuwatumbukiza katika biashara ya omba omba mitaani badala ya kwenda shule!

Kuna watoto wanaotolewa mimba hata kabla ya kuzaliwa, hivi ni vitendo vinavyofanywa na watu wakatili.


Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, amewataka watoto kusali kwa ajili ya kuwaombea akina Herode mamboleo ili waweze kutubu na kumwongokea Mungu kwa kusimama kidete kutetea Injili ya uhai tangu pale mtoto anapotunga mimba tumboni mwa mama yake, hadi mauti ya kawaida inapomfika kadiri ya mpango wa Mungu!


Amewataka wazazi na walezi kuwajengea watoto wao mazingira bora zaidi yatakayowawezesha kuwa ni mashuhuda amini wa Mtoto Yesu katika maisha yao. Waamini washinde ubinafsi kwa kuongozwa na upendo wa Mungu kwa ajili ya maskini na wahitaji zaidi.

Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwenye mitandao ya kijamii, anawaalika waamini pamoja na watu wote wenye mapenzi kusali kwa ajili ya kuwaombea watoto wanaoteseka sehemu mbali mbali kwa kutolewa mimba kabla hawajazaliwa; kwa kuteseka kutokana na baa la njaa na magonjwa na wale ambao wanabebeshwa silaha na kutumwa mstari wa mbele kama chambo kwenye mapigano.

Huu ni ujumbe makini kabisa unaotolewa na Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi, tarehe 28 Desemba 2017, Mama Kanisa anapoadhimisha Siku kuu ya Watoto Mashahidi waliouwawa na Mfalme Herode kwa hofu ya kupoteza kiti chake za kifalme, baada ya kuambiwa kwamba, Kristo Yesu, Mfalme wa Mataifa amezaliwa mjini Bethlehemu.

Tangu mwanzo, Mama Kanisa amewaangalia watoto hawa kama mashuhuda wa Fumbo la Umwilisho, watoto ambao hata kama hawakumwona Kristo Yesu, lakini walibahatika kupata Ubatizo wa Damu, kumbe, wao ni mashuhuda wa Kristo kwa njia ya sadaka ya maisha yao.

Mama Kanisa daima anafundisha kwamba, kifodini ni sadaka kubwa ambayo Mwenyezi Mungu hupenda kuwakirimia waja wake.

Siku kuu ya Watoto mashahidi wa imani ilianza kuadhimishwa kunako karne ya tano. Watoto hawa wanafuatana na mashuhuda wa imani kama Stefano shahidi na Mwinjili Yohane ambao daima wamekuwa mstari wa mbele kusimamia imani, utu na heshima ya binadamu.


Wakati huo huo , Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto, UNICEF linasema, Mwaka 2017 umeshuhudia idadi kubwa ya watoto duniani, ikikabiliwa na mashambulizi mbali mbali hasa huko Iraq, Siria, Yemen, Nigeria, Sudan ya Kusini na Myanmar, maeneo ambayo pia yametajwa na Baba Mtakatifu Francisko wakati akitoa ujumbe wa Noeli kwa Mwaka 2017 kwa ajili ya mji wa Roma na Ulimwengu katika ujumla wake, maarufu kama “Urbi et Orbi ”.

Huko nchini Nigeria na Cameroon, Kikundi cha kigaidi cha Boko Haram kimefanya mauaji ya watoto 135. Huko DRC, watoto 850 wamelazimika kukimbia makwao. Takwimu zinaonesha kwamba, zaidi ya watoto 350, 000 wanakabiliwa na utapia mlo wa kutisha.
Hali ya maisha ya watoto Sudan ya Kusini ni mbaya sana kutokana na vita, njaa na utapiamlo wa kutisha. Zaidi ya watoto 19, 000 wamelazimishwa kwenda kupigana mstari wa mbele kama chambo na kwamba, zaidi ya watoto 2, 300 wameuwawa kikatili tangu vita ya wenyewe kwa wenyewe ifumuke upya nchini humo kunako mwaka 2013. Nchini Somalia zaidi ya watoto 1, 740 wameingizwa kwenye vikosi vya kijeshi na kupelekwa mstari wa mbele! UNICEF inawataka wadau mbali mbali kushikamana katika kuwahudumia watoto, ili waweze kupata chakula na lishe bora; elimu, malezi; ulinzi na usalama, ili waweze kufurahia maisha ya utoto wao!

Na Padre Richard A. Mjigwa, C.PP.S.

Vatican News!

My take: asante sana baba mwadhama kwa tafakari ya kimataifa.
Wakubwa mmeshindwa kuomba sawasawa na matakwa ya MUNGU aliye hai mnawatwika watoto mzigo wa kuomba! AIBUUUUU!

Is like YESU KRISTO aombewe na Petro.

Mwadhama dhalili.
 
Kashindwa kulinganisha kilichoandikwa na uhalisia. Ujinga,umaskini na maradhi kamwe havitishii mtawala. Angetoa mifano ya Nchi nyingine kama hapa kwet u hamna.
 
ameandika nini kisichojulikana. haya ni mastory ya siku zote, miaka yote, karne zote. Sidhani kama ana reflection ya kinachoendelea hapa kuwa akina Ben wamepotezwa na mtu kulinda ufalme wake, NEVER!

Una ushahidi?....nyie ndo walewale mkiitwa kutoa ushahidi mnasema..... nilisoma kwenye social media....zero brain
 
Adui wa sasa wa malezi ya mtoto duniani ni vita, na vita hutokana na dhulma. Ikiwa dhulma ni chanzo cha vita ni jukumu la viongozi wetu wa kiroho kuwaasa viongozi wetu wa kisiasa waongoze nchi zetu kwa haki kuepuka dhulma na uonevu ili kujiepusha na ghasia, ili wazee, wanawake na watoto tuwaepushe na vita ambayo mara nyingi huathiri kada hizo, badala ya kutuletea simulizi za kale kumuhusu Herode.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom