Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,638
- 697,929
Kwa kiingereza tungeita street food festival).
Hizi karamu sio za msimu bali zimekuwa sehemu ya maisha ya watu daily uswahilini, usijali sana ubora na usalama wake, vina ladha yake fulani ikikukamata huchomoki.
Hivi ni vyakula ambavyo hapo zamani kabla dunia haivua shumizi na kuvaa bikini vilikuwa vinapewa wanyama ama sana sana utavikuta kwenye vilabu vya pombe za kienyeji aka mataputapu, ila kwa dunia ya leo kila kitu ni dili hakuna kinachotupwa kwakuwa hata kondom yenye manii ina wateja
1. Supu ya mapupu/bandama ya ng'ombe
Hivi ni sehemu ya viungo vya ndani kwenye tumbo la ng'ombe lakini visivyo na thamani kama maini figo na utumbo. Hivi vinaitwa faida ya mchunaji, huwezi kuvikuta buchani. Siku hizi huko uswazi utavikuta jioni mitaani watu wakifurahia
2. Supu ya pua ya ng'ombe (sio kichwa)
Hii nayo ni mixer ya kongosho, koromeo, nyuchi kwa maana ya uke na njia ya uzazi na kwa uchache uume ambao siku hizi umekuwa dili sana kwa mambo mengine hivyo ni adimu kwenye supu
3. Mishkaki ya 100
Hivi vimishkaki vina addiction mbaya kabisa ni vitamu na ni laini balaa unaweza kujikuta unamaliza buku bila kutegemea, lakini unajua asili yake ninini? Mwanzoni vilikuwa sehemu ya faida ya mchunaji na mwamba ngozi.. Ngozi kabla ya kuwambwa hutolewa nyama zote sasa hizi huwa vinyama vidogo vidogo! Hivi havitupwi bali hutengenezwa huto tumishkaki twa mia. Kibaya ni kwamba baada ya soko kuwa kubwa wauzaji walifikia kuwalisha watu mpaka ndama waliofia tumboni, paka na umbwa! Hivyo unapokula sikilizia utamu wa ladha zaidi kuliko mengine
4. Mzigo wa kwio
Hapa ni kombinega ya kichwa(halohalo)
Miguu (no 11) na utumbo (cheni block)
Miguu inasokomezwa mdomoni na kutokea shingoni kisha utumbo unaviringwa kushikamanisha vizuri miguu na kichwa kisha vinakaangwa!
Utamu wake acha kabisa, baadhi ya mimba zimepatikana huku.
5. Korodani za mbuzi (wanga tupu)
Kituo maarufu kilikuwa Kwasokota Temeke nje ya ile bar nimeisahau jina.. Watu walikuwa wanatoka Kino kwenda Sokota kula kende za mbuzi za kuchoma! Siku hizi vituo ni vingi Uswazini
6. Supu ya ubongo wa ng'ombe
Hii ina watu wake na oda zake! Ila wengi huhofia kupewa supu ya ubongo wa kondoo maana ubongo wake una mdudu ukimla lazima dishi liyumbe
7. Supu ya jicho la ng'ombe
Hii nayo ina wateja maalum na sio wengi, na wao huitumia kwa mahitaji maalum. Wengi hawaipendi kwakuwa sometimes ikiwekwa kwenye bakuli ni kama lile jicho linakuangalia supu hii hujumuishwa na masikio ya ng'ombe pia
8. Kichuri (damu ya ng'ombe)
Mwanzoni ilikuwa ni kwa baadhi ya makabila lakini siku hizi uswazi unaikuta kichuri iliyokaushwa ikabanikwa nakuwa kama maini
9. Vyakula bahari (ngisi, pweza na kamba)
Mwanzoni vililiwa na watu wachache tena wa Pwani tuu, lakini siku hizi vinasafirishwa hadi mikoani.. Vinawamalizia pesa watu acha kabisa na ndio vyakula pekee ambavyo utavikuta uswazi na ushuani
10. Kacholi, sambusa, ndizi za kuchoma, kababu nk
Hivi ni visindikizi vya baadhi ya vyakula vingi vya vyama vilivyotajwa hapo juu na huwa pembeni yake hukosi mbilimbi, pilipili kachumbari nknk.. Kumbuka kwenye hizo sambusa kuna za nyama na za viazi. Lakini ni afadhali za viazi
Kati ya vyote hivi hakuna kinachozidi 2000 na bei ya chini ni shilingi mia.. Kwa sehemu kubwa ni vyakula visivyozingatia kanuni za afya na usalama wake kwakweli ni mdogo sana kuanzia maandalizi mpaka eneo la kuuzia.. Ila mwili wa binadamu una tabia ya kujibadili na kuendana na mazingira uliopo! Kuharisha na kutapika ni mara moja au mbili tu. Baada hapo ni mwendo mdundo
NB: Usiombe mkeo mjamzito mimba yake ikawa inataka kacholi na pweza wa Kwamtogole. Hata kama unakaa masaki utawasha gari uende na ole wako umpelekee za kwakopa atajua tu
Hizi karamu sio za msimu bali zimekuwa sehemu ya maisha ya watu daily uswahilini, usijali sana ubora na usalama wake, vina ladha yake fulani ikikukamata huchomoki.
Hivi ni vyakula ambavyo hapo zamani kabla dunia haivua shumizi na kuvaa bikini vilikuwa vinapewa wanyama ama sana sana utavikuta kwenye vilabu vya pombe za kienyeji aka mataputapu, ila kwa dunia ya leo kila kitu ni dili hakuna kinachotupwa kwakuwa hata kondom yenye manii ina wateja
1. Supu ya mapupu/bandama ya ng'ombe
Hivi ni sehemu ya viungo vya ndani kwenye tumbo la ng'ombe lakini visivyo na thamani kama maini figo na utumbo. Hivi vinaitwa faida ya mchunaji, huwezi kuvikuta buchani. Siku hizi huko uswazi utavikuta jioni mitaani watu wakifurahia
2. Supu ya pua ya ng'ombe (sio kichwa)
Hii nayo ni mixer ya kongosho, koromeo, nyuchi kwa maana ya uke na njia ya uzazi na kwa uchache uume ambao siku hizi umekuwa dili sana kwa mambo mengine hivyo ni adimu kwenye supu
3. Mishkaki ya 100
Hivi vimishkaki vina addiction mbaya kabisa ni vitamu na ni laini balaa unaweza kujikuta unamaliza buku bila kutegemea, lakini unajua asili yake ninini? Mwanzoni vilikuwa sehemu ya faida ya mchunaji na mwamba ngozi.. Ngozi kabla ya kuwambwa hutolewa nyama zote sasa hizi huwa vinyama vidogo vidogo! Hivi havitupwi bali hutengenezwa huto tumishkaki twa mia. Kibaya ni kwamba baada ya soko kuwa kubwa wauzaji walifikia kuwalisha watu mpaka ndama waliofia tumboni, paka na umbwa! Hivyo unapokula sikilizia utamu wa ladha zaidi kuliko mengine
4. Mzigo wa kwio
Hapa ni kombinega ya kichwa(halohalo)
Miguu (no 11) na utumbo (cheni block)
Miguu inasokomezwa mdomoni na kutokea shingoni kisha utumbo unaviringwa kushikamanisha vizuri miguu na kichwa kisha vinakaangwa!
Utamu wake acha kabisa, baadhi ya mimba zimepatikana huku.
5. Korodani za mbuzi (wanga tupu)
Kituo maarufu kilikuwa Kwasokota Temeke nje ya ile bar nimeisahau jina.. Watu walikuwa wanatoka Kino kwenda Sokota kula kende za mbuzi za kuchoma! Siku hizi vituo ni vingi Uswazini
6. Supu ya ubongo wa ng'ombe
Hii ina watu wake na oda zake! Ila wengi huhofia kupewa supu ya ubongo wa kondoo maana ubongo wake una mdudu ukimla lazima dishi liyumbe
7. Supu ya jicho la ng'ombe
Hii nayo ina wateja maalum na sio wengi, na wao huitumia kwa mahitaji maalum. Wengi hawaipendi kwakuwa sometimes ikiwekwa kwenye bakuli ni kama lile jicho linakuangalia supu hii hujumuishwa na masikio ya ng'ombe pia
8. Kichuri (damu ya ng'ombe)
Mwanzoni ilikuwa ni kwa baadhi ya makabila lakini siku hizi uswazi unaikuta kichuri iliyokaushwa ikabanikwa nakuwa kama maini
9. Vyakula bahari (ngisi, pweza na kamba)
Mwanzoni vililiwa na watu wachache tena wa Pwani tuu, lakini siku hizi vinasafirishwa hadi mikoani.. Vinawamalizia pesa watu acha kabisa na ndio vyakula pekee ambavyo utavikuta uswazi na ushuani
10. Kacholi, sambusa, ndizi za kuchoma, kababu nk
Hivi ni visindikizi vya baadhi ya vyakula vingi vya vyama vilivyotajwa hapo juu na huwa pembeni yake hukosi mbilimbi, pilipili kachumbari nknk.. Kumbuka kwenye hizo sambusa kuna za nyama na za viazi. Lakini ni afadhali za viazi
Kati ya vyote hivi hakuna kinachozidi 2000 na bei ya chini ni shilingi mia.. Kwa sehemu kubwa ni vyakula visivyozingatia kanuni za afya na usalama wake kwakweli ni mdogo sana kuanzia maandalizi mpaka eneo la kuuzia.. Ila mwili wa binadamu una tabia ya kujibadili na kuendana na mazingira uliopo! Kuharisha na kutapika ni mara moja au mbili tu. Baada hapo ni mwendo mdundo
NB: Usiombe mkeo mjamzito mimba yake ikawa inataka kacholi na pweza wa Kwamtogole. Hata kama unakaa masaki utawasha gari uende na ole wako umpelekee za kwakopa atajua tu