Mkuu LUBEDE, kwanza kabisa pole kwa yaliyokukuta. Kwa kweli yakupasa umshukuru Mungu kwa kukufunulia na kukuonyesha tabia za huyo mwanamke ambaye wewe ulidhani ndio chaguo sahihi katika maisha yako.
Kuna msemo wa zungu unaosema "There are two things which defines a person. His/her patience when he has nothing and his/her attitude when he/she has everything." Kama hiyo kazi imemfanya huyo mwanamke akuone huna thamani kwake basi ujue huyo hakufai. Tabia ya wanawake kama hao ni ya wale ambao wanatanguliza fedha, mali na anasa za huu ulimwengu mbele kuliko utu. Kwa kweli badala ya kulalamika yakupasa umshukuru Mungu kwa kukuonyesha tabia ya huyo mwanamke before its too late maana huwezi jua, pengine huko mbeleni angeweza kukufanyia mamb makubwa na ya kukuumiza zaidi ya hili.
Mimi nakushauri mkuu usikate tamaa na badala yake usali na umuombe Mungu akujalie akujalie mke mwema ambaye alikuandalia tangu kuumbwa kwako.
Usijerogwa kumsomesha mwanamke
Sikurogwa wakuu,nilihisi mimi ni kijana makini na mwenye uelewa nisiyehitaji ubabaishaji kwenye hilo,kumbe hamna kitu,nimejikuta nabakia kuwa kibarua ambaye sikuuelewa mtego wa fundi..
Ama kweli "NO LIFE WITHOUT A WIFE, BUT A WIFE CAN BE A KNIFE TO CUT OFF YOUR LIFE" huyu mwanamke pamoja na kusimamia show zote tangu high school, chuo na kurudi mtaani hana muelekeo, nikatumia unguli wangu mjini kapata kazi T.R.A.
Nikaona ni wakati muafaka home wamjue mambo mengine ya kuwa pamoja milele yaendelee,wakamtambua na sifa tele kuwa najua kuchagua,mwisho wa siku hata posa hatujapeleka anasema alikurupuka nimuache, afanye kwanza kazi, anahisi kuwa single ni vizuri zaidi kwake, atanifikiria baada ya miaka miwili.
Sitaki tena kuoa?
Mchumba hasomeshwi na mume mtarajiwa braza
pole sana ndo ukubwa huo
Well said mkuu,nashukuru kwa kunipa moyo kwa niaba ya wote walionitakia nguvu na ujasiri wa kufanya nione kawaida,game yake ilikuwa ngumu katika familia yao,nikaona sababu atakuwa mwenzi wa maisha na mama wa mbeleni wa wanangu na nguvu ya kumtengeneza kielimu ninayo(pesa)nikaona kiroho safi sio mbaya nim'shape ili asiwe mzigo,na mwisho kaamua kuwa punda na kunilipa mateke,haina shida,lengo la kuandika hapa ni kuwapa alert wahangaikaji wenzangu kuwa haya mambo wengi tunayasikia tu na kuhisi kama ni stori za kumchekesha mfalme,haya mambo ni real wakuu,wanawake hawaaminiki,yaani nimeamini kweli "CURIOSITY KILLED THE CAT"
Mary Nyanzala Sayi wa TRA!!
pole sana kijana mwenzangu njoo kwangu upate pumziko la nafsi i dont need yo pesa wala vitu i only need yo love