Kapata kazi kanitupa


Well said mkuu,nashukuru kwa kunipa moyo kwa niaba ya wote walionitakia nguvu na ujasiri wa kufanya nione kawaida,game yake ilikuwa ngumu katika familia yao,nikaona sababu atakuwa mwenzi wa maisha na mama wa mbeleni wa wanangu na nguvu ya kumtengeneza kielimu ninayo(pesa)nikaona kiroho safi sio mbaya nim'shape ili asiwe mzigo,na mwisho kaamua kuwa punda na kunilipa mateke,haina shida,lengo la kuandika hapa ni kuwapa alert wahangaikaji wenzangu kuwa haya mambo wengi tunayasikia tu na kuhisi kama ni stori za kumchekesha mfalme,haya mambo ni real wakuu,wanawake hawaaminiki,yaani nimeamini kweli "CURIOSITY KILLED THE CAT"
 
Last edited by a moderator:
ngoja Kwanzaa...kakutana na wajanja mjini wacha wachezee ngozi ichuje ndio atarudi kwako kiongozi shukuru ulipiga mzigo fresh na kama ulibahatika kupata na hii kitu 0713 shukuru yaishe tafuta mwingine
 
asomeshe mara ngapi na kamaliza na kazi kapata

Sikurogwa wakuu,nilihisi mimi ni kijana makini na mwenye uelewa nisiyehitaji ubabaishaji kwenye hilo,kumbe hamna kitu,nimejikuta nabakia kuwa kibarua ambaye sikuuelewa mtego wa fundi..
 
Nampongeza huyo binti! Ukimsomesha mtu asiye ndugu yako unatakiwa kujua kuwa ni kama umetoa sadaka na usitegemee malipo au kitu fulani!

Pengine kuna ndugu zako waliitaji huo msaaada ulishindwa kuwasaidia lakini ukamsaidia aliyedhani ni muhimu sana na atathamini mchango wako!

Nafikiri umevuna ulicho panda na hayo ndio mavuno na ni funzo kwako..! Nampongeza huyo binti..
 
Sikurogwa wakuu,nilihisi mimi ni kijana makini na mwenye uelewa nisiyehitaji ubabaishaji kwenye hilo,kumbe hamna kitu,nimejikuta nabakia kuwa kibarua ambaye sikuuelewa mtego wa fundi..

pole sana kijana mwenzangu njoo kwangu upate pumziko la nafsi i dont need yo pesa wala vitu i only need yo love
 

Pole sana brothr bt amin ipo siku atakuja analia
 
Usijali kuoa utaoa mwingine

Huyo inabidi ukae chini uongee na Mungu kwamba maumivu aliyokupatia na hauna kosa lolote kwake basi yampate mara millioni moja na akukumbuke katika kila hatua yake maishani mwake.

Omba Mungu akupe nguvu na umsahau pia na umshukuru kuwa amekuepusha mabaya maishani mwako kwa kukuonyesha sasa hivi huyo mchumaji alivyo.

Hakufai kuwa mke songa mbele utapata uliyepangiwa ma Mungu.

Furahia haukumuweka ndani angekumaliza roho na kuumiza haswa.
 

Ungemtia mimba mapema
kama watoto wawili tu akilu ingemkaa sawa
 
Sometimes maamuz magum yanahitajika temana naye atakuumiza kichwa chako
 
​Ni kwel mchumba hasomeshwi lakini ni zaidi kuwa katika macho yakibinadamu utasema ni mbaya sana ila katika mach yakiroho ni vyema maana ambayo yangekuja ni makubwa zaidi...
 
mshukuru Mungu kwa yote pia jitahidi na umuombe Mungu akusahaulishe huyo mtu. Kilichomtokea huyo mchumba wako ni tamaa tu kwani huko alikoenda atakuwa amepata m/ume mwingine ambaye ana pesa zaidi yako amemdanganya nae bila kufikiria amemkubalia. Ipo sana hiyo kwenye maofisi akija dada mgeni aliye single wale ma-player wanamtokea na kumrubuni kabla hajausoma mchezo anapigwa bomba baadae anapigwa chini na akistuka atajilaumu sana.

Baadae atarudi kwako ila utaamua mwenyewe maana utakuwa ushajua tabia ya mama watoto wako mtarajiwa.

Kuna kanuni za kiume hapa ulizikiuka ambazo ni mbili
1. Kumwamini m/mke na kujitoa jumla as if ni mkeo wa ndoa
2. Kumsomesha mchumba

Hivyo viwili m/ume hutakiwi kuvifanya abadani utakuja kulia kilio kikubwa sana na kulaani wanawake wote wakati kosa niwewe kukiuka hivyo vitu viwili

Tafuta m/mke mwingine ila usimwamini 100% wala usimsomeshe maana ni jukumu la wazazi wake hilo
 
tatizo wadada wengi hawana utu.... wanapenda kujiangalia kwanza wao kabla ya uhusiano uliopo.... Pole mkuu, wewe achana nae, endelea na maisha yako, maana kuna msemo wasema "katika mauhusiano, unaweza ukamfanya mpenzi wako mke/mume bora kwa mwanaume/mwanamke mwengine"... ume play part yako... so u have to move on... usijeshika makali kwa sasa, wakat mpini unakuja, we vumilia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…