Kanisa nililosali jana na changamoto zake

Kanisa nililosali jana na changamoto zake

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,579
Reaction score
161,433
Jana nilienda kusali kwenye kanisa moja mitaa ya kati.
Huko mhubiri alikuwa bize kuuponda mchezo wa soka kuwa ni wa kishetani uliotawaliwa na uongo na hila.
Akasema mchezaji anapompiga chenga mwenzake anakuwa amedanganya, maana anakuwa anamdanganya kuwa anaenda kulia wakati anaenda kushoto.
Akaendelea kusema wanapoangushana na kuchezeana faulo wanakuwa wanavunja amani na wanafanya uadui.
Pia akasema wachezaji wanapojiangusha kutafuta penalt wanasema uongo.
Akatoa kali zaidi kwa kusema fifa na kombe vya dunia viliundwa na shetani mwenyewe na akavileta duniani ili kuwapofusha watu.
Watu wawe busy na mpira na kumsahau mungu.
Akawashauri waumini wake waache kabisa kufuatilia michuano ya kombe la dunia inayoendelea afrika ya kusini.
 
Duh! Hii kali ni mara yangu ya kwanza kuisikia. Hakika duniani kuna vituko. Huyo bado ana safari ndefu sana ya kulielewa Neno la Mungu. Maana kwa mwendo huo kila kitu kitakuwa ni dhambi na ushetani. Maisha yataenda mbele kweli?
 
Mhh..Hapo atakuwa anahofia mapato kupungua ktk kipindi hiki cha mwezi mmoja, maana mtu akikesha kuangalia mechi the most likely possibility ni kutokuamka mapema na kwenda kupeleka sadaka kwa 'mpakwa mafuta wa buwana'.

Ama kwa hakika kila kona wamekava wajasiriamali na wachumia tumboni..! lol
 
Jana nilienda kusali kwenye kanisa moja mitaa ya kati.
Huko mhubiri alikuwa bize kuuponda mchezo wa soka kuwa ni wa kishetani uliotawaliwa na uongo na hila.
Akasema mchezaji anapompiga chenga mwenzake anakuwa amedanganya, maana anakuwa anamdanganya kuwa anaenda kulia wakati anaenda kushoto.
Akaendelea kusema wanapoangushana na kuchezeana faulo wanakuwa wanavunja amani na wanafanya uadui.
Pia akasema wachezaji wanapojiangusha kutafuta penalt wanasema uongo.
Akatoa kali zaidi kwa kusema fifa na kombe vya dunia viliundwa na shetani mwenyewe na akavileta duniani ili kuwapofusha watu.
Watu wawe busy na mpira na kumsahau mungu.
Akawashauri waumini wake waache kabisa kufuatilia michuano ya kombe la dunia inayoendelea afrika ya kusini.

Buji unafanya survey kwenye makanisa?? utaingia mahala ambapo NO EXIT... shauri yako, we test zali tu
 
Mshikaji hilo ni kanisa la nabii tito

Mie hivi vyeo vyao tu ndo naishiwa hamu kabisaaaaaaaaa! Kuna mshikaji alikuwa mwalimu wa kwaya tu huku na kule akapelekwa marekani miezi 3 kurudi nasikia anaitwa APOSTLE mweh!
 
Kama hujui kitu ukikaa kimya watu watahisi kuwa hujui, lakini ukifungua mdomo na kuongea, na ukaongea uongo mtupu basi watu watathibitisha hisia zao kuwa wewe hujui!
 
Duh, kama ni hivyo basi Messi ataenda Motoni
 
Kama hujui kitu ukikaa kimya watu watahisi kuwa hujui, lakini ukifungua mdomo na kuongea, na ukaongea uongo mtupu basi watu watathibitisha hisia zao kuwa wewe hujui!

Bonge la quot naiazima hii mara moja!
 
Haya makanisa ndio yanayompa Kiranga na Blueray credit.
 
Bwana ehh, nilikuwa na kiu ya neno la mungu, si ndio nikajikuta najichomeka kusiko faa?

Pole ndugu yangu... siku zote kumbuka "Bora shetani unayemjua kuliko Malaika Usiyemjua"... Unaweza kwenda sehemu kwa nia njema sana lakini ukitoka unashangaa netiweki imepotea kabisa... (wanakutia kinyaa mpaka thelengeti haipandi tena)...:tea:
 
Ndg yangu hukwenda kanisani. Huo ulikuwa ukumbi wa devil worshippers. Nao husema "yesu ni bwana", lakini matendo ni tofauti. Rudi tena uchunguze.
 
Back
Top Bottom