Kanisa lingine lachomwa moto Vingunguti

Kanisa lingine lachomwa moto Vingunguti

Status
Not open for further replies.

jigoku

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2011
Posts
2,411
Reaction score
733
Sakata la kuchoma makanisa limeendelea tena baada ya kanisa la Baptist Vingunguti kuchomwa moto usiku wa kuamkia leo majira ya saa nane na robo.

Watu wasuojulikana walionekana kwenye eneo hili la kanisa na kuwasha moto,nyumba jirani kuna binti alitoka kujisadia kwenye choo kilichoko nje,na ndipo alipoona vijana wakitokomea na huku kanisa likiwaka moto,ndipo alipowaamusha wasichana kutoka kwenye familia ya mchungaji Hezron Mwaisemba na kuanza kupiga kelele za kuomba msaada.

Wasamalia wema waliamka na kuanza kuuzima moto kabla haujashika kasi. Kwa mujibu wa mchungaji Hezron amesema vijana hao walikuwa na chupa ya mafuta ya petrol ambayo waliyatumia kuchoma,waokoaji walikuta chupa ya mafuta, kiberiti na kisu kikubwa yaliyopatikana kwenye eneo la tukio, vitu vyote hivyo vimechukuliwa na polisi waluofika kanisani hapo usiku huo.

Kanisa hili liko mtaa wa Mtambani, kitongoji cha Faru kata ya Vingunguti.

Watanzania wapenda amani tutafakari kwa makini nini suluhisho la jambo hili. Nafanya juhudi za ku-upload picha, bado zinagoma.

Source: Mimi mwenyewe niko eneo la tukio.

===========
UPDATE - Oct 21, 2013
Kanisa la Baptist buguruni Dar es salaam limechomwa moto.. Akizungumza kanisanai hapo kwa uchungu mchungaji wa kanisa hilo Ezekiel Mkumbila amesema wamesikitishwa na sana kitendo kilichofanywa na watu wasioulikana.

Mchungaji Mkumbila amesema kanisa limechomwa ndani na kusababisha hasara kubwa sana..Amesema kanisa hilo lilchomwa jumamosi majira ya saa 8 usiku...Kamanda wa polis kanda maalum ya Ilala amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema ameagiza polisi kufanya upelelezi ili kubaini ni nani waliohusika na uchomwaji wa kanisa hilo...

(Wapo radio news)
 
Ni wale waliochiwa juzi,wanaendeleza kazi yao
 
Wakuu naomba maelekezo nini nifanye ili niweze kuwawekea picha na video ya dkk mbili ambayo nimeirekodi.
 
"ukiwa unatafakari kuwasha moto nyumba ya mwenzio kwako kumeshakuwa mkaaa" hawajui adui yao ni nani bado. akili fupi kweli wanachoma kanisa wakidhani kanisa ni jengo la hasha!!!! wajipange upya
 
Mungu wasamehe hawa wafuasi wa shetani.

Hakuna wanachowaza zaidi ya chuki na mauaji
 
kwa nini makanisa tu kila siku?
 
Hii ni Nchi ya wote,inakera sana na nitukio la kishenzi.kama ni kweli.hamna dini ambaye inaruhusu vitendo vya kinyama.
 
Nachukia mno dini ya waabudu SHETANI [SAW]!
Shetani ameshndwa,na atazd kushndwa kwa jina la YESU!
 
Kanisa la Baptist buguruni Dar es salaam limechomwa moto.. Akizungumza kanisanai hapo kwa uchungu mchungaji wa kanisa hilo Ezekiel Mkumbila amesema wamesikitishwa na sana kitendo kilichofanywa na watu wasioulikana. Mchungaji Mkumbila amesema kanisa limechomwa ndani na kusababisha hasara kubwa sana..Amesema kanisa hilo lilchomwa jumamosi majira ya saa 8 usiku...Kamanda wa polis kanda maalum ya Ilala amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema ameagiza polisi kufanya upelelezi ili kubaini ni nani waliohusika na uchomwaji wa kanisa hilo...

(Wapo radio news)
 
Kanisa la Baptist buguruni Dar es salaam limechomwa moto.. Akizungumza kanisanai hapo kwa uchungu mchungaji wa kanisa hilo Ezekiel Mkumbila amesema wamesikitishwa na sana kitendo kilichofanywa na watu wasioulikana. Mchungaji Mkumbila amesema kanisa limechomwa ndani na kusababisha hasara kubwa sana..Amesema kanisa hilo lilchomwa jumamosi majira ya saa 8 usiku...Kamanda wa polis kanda maalum ya Ilala amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo, na kusema ameagiza polisi kufanya upelelezi ili kubaini ni nani waliohusika na uchomwaji wa kanisa hilo...

(Wapo radio news)
Khaa!! hata hivyo kulikuwa na utulivu kwa muda mrefu bila ya haya mambo. wengi tulikuwa hatuna kazi ya kufanya :A S 39:
 
Ni vigumu kuamini tukio hilo hasa kutokana na muda wa tukio kutokea na taarifa kuwa limeungua ndani ru.huenda ni hujuma za ndani ya kanusa
 
Inasikitisha sana.. Haya mambo inabidi serikali iwe makini na strict sana..otherwise tunatengeneza bomu ambalo likilipuka litakuwa na madhara yasiyozuilika.. Hatutaki tena kusikia habari za "watu watasakwa na kuchukuliwa hatua za kisheria" ilihali hatuoni action za kukomesha kabisa hii hali.. Inatakiwa watu wasakwe, wakamatwe na adhabu zao ziwe kali hadi wakasimuliane wenyewe...

Madhara ya vitu kama hivi ni kutokea kwa minong'ono ambayo inaweza kuwa-mislead wananchi juu ya nani kafanya haya yote... Minong'ono hii matokeo yake si mazuri as inaweza jenga chuki baina ya wananchi...

Please serikali; ongezeni ukali kwa hawa wahuni wanaochoma nyumba za ibada..
 
Poleni sana wakristo wenzangu! Vita yetu si ya mwili bali roho

Teh teh teh teh!

Mchome wenyewe! Ili mpate kudai milioni kadhaa insurance halafu mpate sababu ya kufanya ubadhirifu!

Sasa hivi utaskia " NA KULIKUWA NA HELA ZA MICHANGO YA WANAKONDOO NA HELA ZA WAFADHILI MILIONI 120 NAZO PIA ZIMEIBIWA!"

teh teh teh teh teh!

Na hili ni kanisa kama la saba kuchomwa ndani ya miezi sita!

Halafu we mtizame huyo mchungwaji wa hilo kanisa! Baada ya miezi kama minne hivi ataibuka na ki suzuki vitara kipyaa!
Kapakia mwanakondoo mmoja anang'aaa kama taa kwa mkorogo!

Anampeleka kumtoa pepo! Bonga bar!!!

Teh teh teh teh teh!

Cc Tayeb
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom