Kanisa Katoliki limesema ukweli kwenye tawala katili na dhalimu mnoo Duniani

Kanisa Katoliki limesema ukweli kwenye tawala katili na dhalimu mnoo Duniani

Life2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,377
Reaction score
4,847
Kanisa katoliki limeundwa kwenye misingi ya Haki, Utii, ukweli na kutetea uhai wa binadamu, wanyama na mazingira.

Kutokana na misimamo yake Kanisa katoliki limejikuta likiwa na maadui wengi waovu nje na ndani ya kanisa.

Hapa ndo tunaweza kutumia ile kauli waliomtesa na kumuua Bwana Yesu walikua ni jamaa zake wa Karibu.

Tanganyika yetu napo wameanza kuibuka akina Yuda Eskarioti, Wayahaudi waliomtesa Yesu, Waasi wa Imani...nk

Kwa Vipande 30 vya fedha wamekubali Kuikana imani yao na kuuza Utu wao kwa watawala wenye kunuka damu, wezi, mafisadi, walevi wa madaraka...nk

Japo wengine ni Mamluki/malofa wakitumika na watawala hao hao kupenyeza agenda zao chafu.

Kanisa limeundwa kwa misingi ya Utii ni ajabu leo wanaibuka waamini waasi wa imani na kutaka kuanza kufundisha Mapadre, Maaskofu, Watawa kusema uwongo, kutetea watawala wenye kunuka damu za watanzania.

Nani asiyejua mauaji yaliyotokea Tarehe 29 nani asiyejua wizi mkubwa wa kura pamoja na uchaguzi feki Tanganyika?

Leo unataka umfundishe askofu kusema kulikua hakuna mauaji, uchaguzi ulikua mzuri na kweli mtawala alishinda kwa asilimia 100 hii dhambi haitubiki hata kidogo.

Mitume, Watakatifu wengi walipoteza maisha yao kwa kusema ukweli na kutotea maovu ndani ya jamii.

Kanisa la kweli linatambulika kwa kusimamia hayo na sio kinyume.

Juu ya Mwamba huu nitalijenga kanisa wala Milango ya kuzimu halitalishinda.

Ora Pro Nobis
 
Fighting with a church is just fighting a loosing battle you can't win.
Alishindwa hitler na wengine je wewe utaweza?
Baadhi ya watu wako ni watu wao je utaweza ?
 
Fighting with a church is just fighting a loosing battle you can't win.
Alishindwa hitler na wengine je wewe utaweza?
Baadhi ya watu wako ni watu wao je utaweza ?
Iogope taasisi ambayo watu wako unaowalipa pesa kiasi kikubwa kabisa na wale wa kiasi kidogo wakifanya uhalifu wowote, uwe mkubwa kiasi gani wanaenda kupiga magoti kwao wakilia na kujisema madhambi yote waliyofanya au uliyowatuma kufanya.
Walatini (warumi) waliobuni sacrament ya kitubio walikuwa mbele ya muda maelfu ya miaka.
Wewe na taasisi yako ambayo mipango (dira) yenu ya maendeleo haizidi miaka 50 hauwezi kuwashinda.
 
Kanisa katoliki limeundwa kwenye misingi ya Haki, Utii, ukweli na kutetea uhai wa binadamu, wanyama na mazingira.

Kutokana na misimamo yake Kanisa katoliki limejikuta likiwa na maadui wengi waovu nje na ndani ya kanisa.

Hapa ndo tunaweza kutumia ile kauli waliomtesa na kumuua Bwana Yesu walikua ni jamaa zake wa Karibu.

Tanganyika yetu napo wameanza kuibuka akina Yuda Eskarioti, Wayahaudi waliomtesa Yesu, Waasi wa Imani...nk

Kwa Vipande 30 vya fedha wamekubali Kuikana imani yao na kuuza Utu wao kwa watawala wenye kunuka damu, wezi, mafisadi, walevi wa madaraka...nk

Japo wengine ni Mamluki/malofa wakitumika na watawala hao hao kupenyeza agenda zao chafu.

Kanisa limeundwa kwa misingi ya Utii ni ajabu leo wanaibuka waamini waasi wa imani na kutaka kuanza kufundisha Mapadre, Maaskofu, Watawa kusema uwongo, kutetea watawala wenye kunuka damu za watanzania.

Nani asiyejua mauaji yaliyotokea Tarehe 29 nani asiyejua wizi mkubwa wa kura pamoja na uchaguzi feki Tanganyika?

Leo unataka umfundishe askofu kusema kulikua hakuna mauaji, uchaguzi ulikua mzuri na kweli mtawala alishinda kwa asilimia 100 hii dhambi haitubiki hata kidogo.

Mitume, Watakatifu wengi walipoteza maisha yao kwa kusema ukweli na kutotea maovu ndani ya jamii.

Kanisa la kweli linatambulika kwa kusimamia hayo na sio kinyume.

Juu ya Mwamba huu nitalijenga kanisa wala Milango ya kuzimu halitalishinda.

Ora Pro Nobis
Kanisa ni Moja Tu wengine ni wakusanya sadaka tu
 
Iogope taasisi ambayo watu wako unaowalipa pesa kiasi kikubwa kabisa na wale wa kiasi kidogo wakifanya uhalifu wowote, uwe mkubwa kiasi gani wanaenda kupiga magoti kwao wakilia na kujisema madhambi yote waliyofanya au uliyowatuma kufanya.
Walatini (warumi) waliobuni sacrament ya kitubio walikuwa mbele ya muda maelfu ya miaka.
Wewe na taasisi yako ambayo mipango (dira) yenu ya maendeleo haizidi miaka 50 hauwezi kuwashinda.
Ni baada ya Utawala wa Rumi kufanya madhambi ya kutisha ya kuua watu wasio na hatia kwa njia ya mateso ya kutisha
.

Katoliki ina historia kubwa ya kujifunza mdhara yatokanayo na uminywaji wa haki
 
Kanisa Katoliki na watakatifu wa Mungu wamedhulumiwa sana tangu enzi za makuhani wakuu huko Jerusalemu, mauaji angamizi wakati wa mfalme Nero, ambapo waumini waliuawa kwa makundi, lakini hawakufaulu, badala yake kanisa la Mungu lilizidi kukua, halafu malofa akina Ludovick baada ya kulipwa vipande 30 vya Yuda Iskariote wanaamini kuwa watalinyong'onyesha Kanisa la Kristo!! Ama kweli shetani akishakuingia unakuwa mwendawazimu, kipofu wa kuona na kutambua. Akina Ludovick, baada ya kuingiwa na shetani, kama ikatokea shetani akawatoka, wanabakia kuhangaika wasijue la kufanya.
 
Back
Top Bottom