Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Sasa hivi anazikumbuka zile suti zake. Sio mambo aliyoyatenda. Suti zile inatumika wapi?Ndani ya kipindi kifupi alichokaa wizara ya mambo ya ndani Lugola aliwadhalilisha baadhi ya wakuu wa idara hadi wakajiuzulu.
Hivi Lugola unakumbuka ulivyo mdhalilisha yule aliekuwa kamishna wa magereza kisa tu kachelewa dakika chache kwenye kikao,,ukamfukuza kama mbwa baba wa watu akajitahidi kukuomba radhi huku akikupigia saluti lkn kukutaka kumsikiliza ukamuamuru atoke nje huku kamera za wana habari zikimulika tukio lile. Yule kamishna alipotoka pale akaona isiwe tabu mtu mzima kudhalilishwa vile akaamua kuandika barua akajiuzulu.
Kuna maeneo alipokwenda kukagua vikosi vya magereza ama Polisi aliwadhalilisha baadhi kwamba wanampigia saluti vibaya,,yani alikiwa anataka apigiwe saluti tamu inayonoga kuendana na hadhi yake ya uwaziri wa Mambo ya Ndani. Tena kwa kuwauliza kwa kebehi "ndivyo ulivyofundishwa kupiga saluti hivi'? Wakati mawaziri wote waliopita walikuwa wanapigiwa saluti na maaskari hao hao, lkn yeye akaona hawampigii saluti vzr. Leo kiko wapi Lugola ?Ameachia Kitwanga,ameachia Mwigulu na wewe pia umeachia.
Cheo ni dhamana na kunamaisha baada ya cheo,,msiwe mnajisahau mnapo pata cheo,,mana tumemsikia naniliu alivyosema mtu akiua mnyama na yeye atamuua.
Pole sana Lugola mzee wa kutembea na ilani,,,sijui utaendelea kutembea nayo au itakuwa nzito mkononi mwako. Laana za watu ni mbaya sana,,kamishna wa watu alijiuzulu akaacha ajira yake alioitumikia muda mrefu na kwa uadilifu hadi akawa kamishana lkn alilazimika kujiuzulu kupinga udhalilishaji uliomfanyia ,,,mwacheni Mungu aitwe Mungu.