Kanga vazi linalopotea kwa kasi

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,512
Habari wakuu,

Husika na kichwa hapo juu,

Kanga ni vazi lililotumiwa na wanawake wengi kipindi cha miaka ya nyuma. Vazi la kanga lilikuwa likitumiwa na wanawake wakiwa wanaenda mahali kama sokoni. Kukiwa na sherehe ya mbalimbali za wanawake, vazi la kanga lilitumika kama zawadi kwa mwenye sherehe.

Vazi hilo pia lilitumika zaidi kwenye misiba ambapo wanawake hukifunga kanga kiunoni na nyingine hujitanda au kujifunika. Kipindi hicho ukiangalia kabati la mwanamke utakuts kanga zimepangwa vizuri. vazi hilo la kanga lilitumika kuwatega wanaume kimapenzi.

Miaka ya hivi karibuni kanga imepoteza thamani kutokana na kuingia kwa kijora.Kijora/dera ni mavazi yanayopendwa sana na watu wa uswahilini. Hata wanawake wa kiislam wamekuwa wakipendelea mavazi hayo. Kijora/dera hupendwa kuvaliwa sana kwa sasa kwakuwa ni vazi la kujisitiri.

Pia ni vazi la heshima kwa wanawake na kwa sasa vazi hilo linavaliwa na wanawake wengi. Ukienda sherehe nyingi za uswahilini utakuta wamevaa sare zao za vijora/ dera. Hata katika misiba pia mavazi hayo huvaliwa kwa wingi na wanawake.

Kiufupi vazi la kanga linapotea na kijora/dera kimechukua nafasi

1654766077643.png

Picha kutoka maktaba
 
Unakuta msichana yuko mahala bafuni ni hatua mfano maeneo ya ugenini mbali na home au chuo anaenda bafuni amevaa kitaulo kifupi mwili wote uko uchi anapishana njiani na wanaume wala hajali na kujiona yu uchi.

Sijui ndio kujilengesha wanaume wamtongoze ?!
 
Tatizo linaanzia kwa wazazi/walezi ,

Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.

Wazazi/walezi wenyewe wamepinda!

Wenyewe hawavai mavai yenye staha unategemea binti ajifunze tofauti toka Kwa watu anaowaona nyumbani kwao ?!
 
Kwenye misiba siku hizi wanavaa less materials wenye uwezo,

Wengine ndio hivyo vijola.

Kwenye misiba siku hizi watu wanaenda kwanza saluni kisha ndio akae msibani kuomboleza.

Watu hata kulia naona wengine hawalii siku hizi sijui wanaona meckups zitatoka ?!

Yani upendo kama umepungua vile ?!

Sijui ndio kusema siku za mwisho.

Maana unaambiwa siku za mwisho watu watakuwa wenye kupenda pesa sana na upendo wa wengi utapoa!
 
Kwenye misiba siku hizi wanavaa less materials wenye uwezo,

Wengine ndio hivyo vijola.


Kwenye misiba siku hizi watu wanaenda kwanza saluni kisha ndio akae msibani kuomboleza.

Watu hata kulia naona wengine hawalii siku hizi sijui wanaona meckups zitatoka ?!

Yani upendo kama umepungua vile ?!

Sijui ndio kusema siku za mwisho.

Maana unaambiwa siku za mwisho watu watakuwa wenye kupenda pesa sana na upendo wa wengi utapoa!
Kwakweli wewe ni Akilinjema...
Unaongea point tupu...
 
Kwenye misiba siku hizi wanavaa less materials wenye uwezo,

Wengine ndio hivyo vijola.

Kwenye misiba siku hizi watu wanaenda kwanza saluni kisha ndio akae msibani kuomboleza.

Watu hata kulia naona wengine hawalii siku hizi sijui wanaona meckups zitatoka ?!

Yani upendo kama umepungua vile ?!

Sijui ndio kusema siku za mwisho.

Maana unaambiwa siku za mwisho watu watakuwa wenye kupenda pesa sana na upendo wa wengi utapoa!
Mfiwa anapendezakuliko wewe
msindikizaji
Kama hujaelewa vizuri unaweza kudhani ni sherehe
 
Back
Top Bottom