Hakika ninawaeleza,hali ya CCM hivi sasa ni tete,waasisi wa kudondoka kwa CCM ni Viongozi wa CCM wenyewe!!Natarajia kura nyingi za CCM kwa UKAWA.Waliotoka CCM ni wengi mno,waliojitambulisha hadharani ni wachache wengi wanaugulia moyoni ni maelfu kwa maelfu!!
Nimezaliwa miaka ya 70 na nimeishi vijijini ndani kabisa katika mikoa zaidi ya nane (Njombe,Arusha,Kagera,Morogoro ,Iringa,Rukwa,Mbeya,Pwani na Tanga) mijini pamoja na nje ya nchi.Kati ya mataifa yaliyokuwa na rasilimali ambazo asilimia 90 ya watu wa Nchi hiyo hawanufaiki nazo ni Tanzania.Tuna kila ina ya madini.tuna gesi na makaa ya mawe,tuna mbuga na misitu.ardhi safi na vyanzo vya maji,bahari,milima na mabonde yenye rutuba.Wananchi wa Tanzania ni "maskini wa kutupwa" kuna watu kesho yao ni kitendawili kigumu na wengine wapo hata jiji maarufu la Dar es Salaam. Maisha yamekuwa maigizo. Takwimu zinaonesha ujinga umeongezeka kwa asilimia za kutisha,vijana wengi hawajui kusoma wala kuandika.Wanaendelea na masomo ya Vyuo Vikuu ni wale wenye uwezo wa fedha na mali.Wengi wameshindwa kuendelea kwa sababu hawana uwezo ni mikopo ina utata mwingi..Mpaka leo tunavyoandika magonjwa ambayo yametokomea duniani Tanzania ndio mahala pake.Jiji la Dar limekumbwa na ugonjwa wa aibu wa kipindupindu na wengi wameaga dunia kwa sababu ya uchafu.Mahospitalini wagonjwa wamelala mzungu wa nne kwa magonjwa mbalimbali na wakina mama wakijifungulia mitaroni ama vichochoroni!!!..Upande wa pili,watoto wa vigogo wanasoma nje ya nchi ama katika shule ambazo ada ya mwaka ni Milioni 80.Matibabu yao ya mafua na kikohozi ni ulaya na Marekani.Mavazi yao yamedizainiwa na Madizaina maarufu duniani.Mapumziko yao ni Vegas ama London.Benki zao ni Uswisi na Visiwa vya Uingereza. Vyakula vyao vinaagizwa kutoka Italy na Singapore,Usafiri wao ni ndege za kukodi na magari ya kifahari.Barabara za vumbi hawazijui asilani...Kuing'angania CCM ni miongoni wa matatizo yetu Watanzania.Wakati umefika ni LAZIMA IONDOKE ili kama itakuwa na Jipya IJITAFAKARI….