santos mtn
JF-Expert Member
- Jul 9, 2015
- 348
- 369
Ni upi ushaur wa kiusalama kwa watu wanaoishi msata
mbona pale makete watu wanahamisha mvua.Where there is a demand there is always a supply
Vile vifo vingi mfululizo vilivyotokana na ajali mwezi wa tatu mwaka jana mpaka leo hakuna mwenye maelezo yaliyonyooka japo kuna watu fulani wanajua kila kitu na kwanini karibia zote zilitokea kanda hii
JE MOTO KUTEMBEA ANGANIUjuzi umetoka huku
dar fisi wanafugwa for international export market, pale pugu kuna mtu anawafugaView attachment 397114usafiri wa namna huu ni wa kiwango cha chini sana kuweza kuukuta kwenye kanda maalum..maendeleo kwenye ulimwengu wa kawaida huenda sambamba na maendeleo kwenye ulimwengu wa kiroho..hivi hapa Dar na maeneo ya jirani unaweza kweli kumkuta mtu anafuga fisi?
Wasalaaam kaka mkubwa. Imenibidi niseme kitu hapa.Soma habari za Osale Otango na wengine utajua nazungumzia nini
Mshana hebu siku moja utuletee uzi unaozungumzia maana ya rangi, hasa nyekundu,nyeusi na nyeupe katika ulimwengu wa ushirikina.Naona waganga wa kienyeji wanazitumia sana.Infact hata makampuni mengi makubwa.Kama ukiwa na muda tuletee pia uhusiano kati ya ushirikina na technologies. Naona tekinolojia zingine siku hizi ni ushirikina mtupu.View attachment 397023kila kinachotokea kwenye ulimwengu wa macho ya kawaida ni replica ya ulimwengu wa roho! (Ushirikina ni mkusanyiko wa juju uchawi ulozi chumaulete kuwanga nk)
Tunapozungumzia kanda maalum ya kitu maana yake ni kwamba eneo hilo lina uhitaji wa ziada wa huduma fulani
..mfano Dar kwa sasa ni kanda maalum ya kipolisi kutokana na matukio ya ujambazi kushamiri! Kariakoo kwa sasa ni kanda maalum ya kodi za mamlaka ya mapato Tanzania kutokana na uhitaji wake!
Eneo lote la pwani ya Dar nenda mpaka bagamoyo msata wami pangani mbwewe mkata mpaka tanga mjini ni kanda maalum ya ushirikina
Hapa ndio kuna vilinge vingi vya ushirikina kuliko sehemu nyingine yoyote Tanzania, hapa ndio kuna wachawi waganga na walozi(kwa ujumla wao washirikina wa kila aina)
Hapa ndo kuna kila aina ya matibabu kuanzia miti shamba tunguli kisomo mpaka uganga/uchawi wa kitabu
Unaweza kwenda mikoani na sehemu tofauti kama gambosh nk lakini ukashindwa kwa hakika kukutana na ushirikina halisi....huu ukanda hukosi
View attachment 397030
Kwanini ukanda huu lakini?
Mazingira na jiografia yanaruhusu, malighafi za baharini na nchi kavu vinapatikana kwa wepesi urahisi na kwa wingi! Taka viungo vya binadamu hupati shida! Taka makombe na mazao bahari mengine ni rahisi mno! Taka variaties ya mizizi miti magome na hata matunda na majani huku sio tatizo kabisa
Lakini kwanini isiwe ndani ya Dar na ni nje ya Dar na maeneo ya karibu au mbali kidogo?
Ushirikina ni mambo ya kiroho zaidi yasiyo na ithibati za kisayansi! Yanahitaji ukimya utulivu upweke usiri uchache wa watu na kitu chochote kilichoendelezwa na binadamu kwenye ulimwengu wa teknolojia..teknolojia na usasa ni sumu kubwa kwenye ushirikina
Unaposhuhudia misafara isiyokoma kwa waheshimiwa sana Unaposhuhudia ajali za kila siku! Unaposhuhudia upotevu wa watu wazima na watoto! Unaposhuhudia mambo ya ajabu ajabu usishangae sana bali jua kwamba uko karibu kabisa na ukanda maalum wa kishirikina View attachment 397053
Na yeye yuko bize na "chuma ulete" yake mkuu.Wapare wako.bize.kusaka pesa mpare huyu yuko bize kuwanga
A recent study from the University of Helsinki has suggested that religious people are more likely to have a poor understanding of the world.
It claims that those with a belief in God are more likely to think that inanimate objects, such as metal and oil can think and feel.
Researchers say that the findings suggest people's lack of understanding about the physical world means they apply their own rules, 'resulting in belief in demons, gods, and other supernatural phenomena'.
Participants were asked how much they agreed with the statement 'there exists an all-powerful, all-knowing, loving God' and if they believed in paranormal phenomena such as ghosts and psychic visions.
They were also tested on a range of other topics, including intuitive physics skills and understanding of basic biology.
The results showed that religious people tend to base their actions on instinct, rather than analytical thinking.
So, which part do you believe in?
Mpeni heshima yake
Mheshimiwa Mshana Jr,
Elimu anayoitoa ni nadra kutolewa hadharani.
Kwa karne nyingi mifumo ya elimu rasmi na isiyo rasmi ilikuwa inatoa elimu ya upande mmoja
Elimu ya nadharia na vitendo ya Falsafa za jamii, ilikuwa inatolewa bila masharti.
Elimu ya kiroho ya upande wa Mungu Yehova, ilikuwa inatolewa hadharani kila mwenye kuihitaji aliipata bure kwenye nyumba za ibada.
Elimu ya kiroho upande wa Shetani ilikuwepo lakini ilikuwa inatolewa kwa Siri, ikiambatana na Masharti mazito, mikataba, viapo, nadhiri, maagano ya damu , kafara, kwa usiri, kificho, vitisho,woga,nk.
Unasikia tu mtu fulani kalogwa, fulani ni Mchawi, Anaagua, ana majini, mizimu.nk
Watu wanasafiri kwa ungo, Fisi, na mambo mengi, ambayo yanafundishwa kwa vificho ndo maana jumuiya hizo zinajiita Secret Societies.
Mshana Jr,
ameshaweka wazi kuwa yeye kwa shari au heri alibahatika kusoma huko South Afrika, na nchi nyingine nyingi hivyo kuwa mhitimu wa kiwango cha juu kabisa wa elimu ya imani za kiroho mbadala.
Mimi naielewa elimu hiyo inaitwa. "Science Beyond Material"
Mtu anasoma kuanzia chekechea hadi PHD.
Ndugu yetu Mshana Jr, yeye ana PHD zaidi ya moja ya maswala ya Elimu ya kiroho mbadala.
Elimu ya kiroho ya imani ya Kikristo pia anayo na ni Mlutheri mzuri tu.
Ndugu yetu huyo anajitahidi kutuelimisha kuhusu nini kilichopo kwenye elimu hiyo ya kiroho yaani mambo ya uchawi, Satanism, mizimu, Secret Societies nk, kwa lengo la kuwafahamu wenzetu huko ni nini wanakifanya na kwa malengo gani.
Hii ni baada ya kuokoka na kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wake.
Angalieni,
Wachawi na walozi kamwe hawatoi siri za falme zao.
Hili ni jambo la kwanza lamsingi katika imani
yao hiyo, na wanaapa.
Mshana Jr, anatupa elimu bure ya kutuwezesha kumtambua adui Shetani, nini anaamini, nini anafanya nini malengo yake na zaidi ni wapi anawanasa watu wa Mungu,
Mfano, somo la ndugu
Mshana Jr lililosema
"SHETANI. adui, rafiki asiye na kinyongo"
Lilitufundisha matumaini ya shetani kupata wafuasi na uvumilivu wake.
Mtu anakua na matatizo, anakimbilia kumwomba Mungu ambariki.
Akibarikiwa na kupata mali anakuwa mwovu kuliko mwanzo. hapo Shetani anamdaka ki ulaini kabisa.
Wengine wakipata mali wanaanza kuhalibu mwili wao kwa ulevi, uzinzi nk.
Ndo maana mkiomba baraka, Mungu anawanyima kwasababu mnaomba ili kutimiza tamaa za miili yenu na sio kwa kumtukuza Mungu. Ni bora mbakie kuwa maskini mnakuwa na nidhamu kwa Mungu wenu, kuliko kutajirika na kumkufuru.
Mungu anafahamu mioyo yetu ndo maana anatupa mali kutokana na mafanikio yetu ya kiroho kuweza kuhimili vishawishi vya utajiri wa mali.
Hivyo basi
Sisi tunao endelea kutafakari Falme za Mwanga na Giza tunaendelea kuelimika kwa masomo mbadala ya Ndugu yetu Mshana Jr
Ni mtu aliye jitolea kutupa elimu hiyo bure kabisa.
Narudia tena Mshana Jr ni mtu aliyejielimisha kwa viwango vya PHD.
Ni mtu anayestahili kuheshimika na jamii kwa mchango wake wa mawazo,
Si mchawi wala mlozi na ameokoka.
Taarifa hii ni yangu mimi baada ya kuchunguza kwa makini mawazo yake, sijawahi kumhoji wala kumwona wala hajawahi kuniambia jambo lolote
Ni tafakari yangu tu kwake jinsi nilivyo msoma, maana hata mimi ni msomi wa PHD.
Hivyo tunafahamiana kimawazo tu. yaani kwa kusoma maandiko unaweza kujua kiwango cha elimu ya Mwandishi.
Ndugu Mshana Jr. endelea kuelimisha jamii, tunahitaji kuelewa kwa mapana Elimu mbadala ya kiroho uliyobobea kwayo.
Samahani ndugu Mshana Jr, kwa kukuelezea bila ridhaa yako.
Che mittoga.
