Kamwe sitosahau wema huu aliyonifanyia Mungu

Kamwe sitosahau wema huu aliyonifanyia Mungu

Mungu ni mwema ukimtumainia .
Huyo Mungu mbona hajioneshagi, miaka 4000+
Anamtegemea mwanadamu badala ajitetee mwenyewe.

Mungu wenu mliyemtunga nyie siyo mwema.
Mmempa sifa za hovyo mpaka akapoteza mantiki.
 
Wakuu,

Kuna kipindi nilipita matatizo makubwa sana, kiufupi siendi kwa waganga ila nasali siyo ile deep sana, ila kila kitu changu namtizama Mungu, nikipata tatizo nasali.

Sasa bhana ikafikia kipindi matatizo yakanizidia, uji ukazidi unga. Ni Ile point huoni chochote, mbele ni giza mtindo mmoja. Adui zangu wakaanza kuzitingisha champagne wazifungue, aisee ndio nilikuwa naishia hivyo.

Weight imekata, sina hela, mapenzi nayo yakanichanganya, sina kazi, ni story ndefu sana ila sina kipaji cha Umughaka kuelezea Kwa kirefu. Eh, Huku na huku hali ikazidi kuwa mbaya, sali na kusali wapi, yaani adui wakawa wanafungua vinyaya vya champagne waifungue.

Jamani nilipita kwenye moto, nakumbuka kuna siku niliamka usiku nikalia sana mbele za Mungu juu ya matatizo yangu, vile ambavyo Mungu amewapa adui zangu ushindi, nililia lesso ikajaa kamasi na machozi siwezi elezea hali niliyokuwa nayo.

Nikamwambia Mzee Baba Mungu nahitaji mambo mawili tu; 1. Anichukue (yaani nife) au 2. Aniondolee matatizo, hii ni serious kabisa kwani nilikuwa nimezidiwa na matatizo.

Huwezi amini asubuhi nimeamka macho yamenivimba kwa kulia, sina mbele wala nyuma nikapigiwa simu moja tu n the rest is history.

Nilimwona Mungu aisee, jamani Mungu yuko! Adui wakabaki midomo wazi, wanaulizana imekuwaje? Nilivukaje? Kivipi? Kwanini? Mungu ni mwema, alinivusha. Bado nakula ugali, bado ananipa mitihani ila siyo ile iliyotaka kuniangusha.

Kwakweli mimi na nyumba yangu tutamtegemea yeye mpaka ukamilifu wa dahali, Mungu nakushukuru, siwezi kusahau ulivyonifuta Machozi yangu.

Asikiaye na afahamu siyo chai ni kwl tupu, kwa hivyo ukiona kuna la kujifunza chukua, kama ukidiss sawa tu.
Sasa najifunza nini hapa kama matatizo hujayataja, pia baada ya maombi Mungu alifungua milango ipi 🙄 hata mtoto mdogo anaweza simulia kama wewe ulivyosimulia. By the way kama unadhani kwa usimuliaji huu kuna funzo sawa.....
 
Nmetabasamu kusoma hii! Hakika Mungu ni wa ajabu, hajibu kwa wakati ila ANAJIBU kwa maajabu!
 
Ameen!!Hata Mimi namuona Sana Mungu mengi amenifanyia.Yaani namtumikia yeye TU,biblia ndo kila kitu kwangu.Mchana na usiku.Nikipita kwenye magumu huwa namtukuza Mungu kwa Mambo aliyonitendea na maajabu aliyoyafanya ya uumbaji wa dunia.
Hakika Mungu YUPO na anajibu.
MTAJI NI IMANI TU.
 
Nilimwona Mungu aisee, jamani Mungu yuko! Adui wakabaki midomo wazi, wanaulizana imekuwaje? Nilivukaje? Kivipi? Kwanini? Mungu ni mwema, alinivusha. Bado nakula ugali, bado ananipa mitihani ila siyo ile iliyotaka kuniangusha.

Ayubu22:21
 
Wamtumainio Bwana ni Kama Mlima Sayuni.
Kuna ups and down nyingi sana kwenye haya Maisha,Kuna kipindi unajiona wewe tuu ndo ufanikiwi,unawaona wenzako wakishine, Unajiuliza why You(Kwa nini wewe). Ila ukweli katika hao unaowaona wamefanikiwa,wapo ambao kweli wamefanikiwa na Kuna ambao hawajafanikiwa na Wana matatizo zaidi yako,ila wanaweza kujificha na kutoonyesha shida zao Kwa watu.
Kikubwa Muombe Mungu sana,fanya Kwa bidii chochote kile unachokifanya,usihadithie kila mtu matatizo yako,epuka matumizi yasiyo ya lazima na mwisho jiwekee malengo ya mda mfupi na Mrefu,mambo yataenda vizuri tuu.
(Zaburi 23)
 
Wakuu,

Kuna kipindi nilipita matatizo makubwa sana, kiufupi siendi kwa waganga ila nasali siyo ile deep sana, ila kila kitu changu namtizama Mungu, nikipata tatizo nasali.

Sasa bhana ikafikia kipindi matatizo yakanizidia, uji ukazidi unga. Ni Ile point huoni chochote, mbele ni giza mtindo mmoja. Adui zangu wakaanza kuzitingisha champagne wazifungue, aisee ndio nilikuwa naishia hivyo.

Weight imekata, sina hela, mapenzi nayo yakanichanganya, sina kazi, ni story ndefu sana ila sina kipaji cha Umughaka kuelezea Kwa kirefu. Eh, Huku na huku hali ikazidi kuwa mbaya, sali na kusali wapi, yaani adui wakawa wanafungua vinyaya vya champagne waifungue.

Jamani nilipita kwenye moto, nakumbuka kuna siku niliamka usiku nikalia sana mbele za Mungu juu ya matatizo yangu, vile ambavyo Mungu amewapa adui zangu ushindi, nililia lesso ikajaa kamasi na machozi siwezi elezea hali niliyokuwa nayo.

Nikamwambia Mzee Baba Mungu nahitaji mambo mawili tu; 1. Anichukue (yaani nife) au 2. Aniondolee matatizo, hii ni serious kabisa kwani nilikuwa nimezidiwa na matatizo.

Huwezi amini asubuhi nimeamka macho yamenivimba kwa kulia, sina mbele wala nyuma nikapigiwa simu moja tu n the rest is history.

Nilimwona Mungu aisee, jamani Mungu yuko! Adui wakabaki midomo wazi, wanaulizana imekuwaje? Nilivukaje? Kivipi? Kwanini? Mungu ni mwema, alinivusha. Bado nakula ugali, bado ananipa mitihani ila siyo ile iliyotaka kuniangusha.

Kwakweli mimi na nyumba yangu tutamtegemea yeye mpaka ukamilifu wa dahali, Mungu nakushukuru, siwezi kusahau ulivyonifuta Machozi yangu.

Asikiaye na afahamu siyo chai ni kwl tupu, kwa hivyo ukiona kuna la kujifunza chukua, kama ukidiss sawa tu.
Amen

Ayub anasema hajawai kumwona mwenye haki ameachwaa.
 
Hamna Mungu hapo wala nini, coincidence ya matukio tu hyo..

Ni kawaida ya wanadamu tukizidiwa tunatafuta kisingizio cha kujificha.

Kete ziko kwa maadui, usiwaache tu afu useme Mungu atatenda. Pambana mwenyewe ushinde. Mungu huyo hawezi kukusaidia in reality, wewe ulisaidiwa na aliekupigia simu.
Watu kama wewe mnaosema hakuna Mungu biblia inawaita wapumbavu.
 
Watu kama wewe mnaosema hakuna Mungu biblia inawaita wapumbavu.
Biblia si kitu, ni kakitabu flani tu kaliandikwa na mjinga asiyejua hata jua linaenda wapi usiku.

Nioneshe kama kweli hiyo biblia inatuita wapumbavu..!
 
Hamna Mungu hapo wala nini, coincidence ya matukio tu hyo..

Ni kawaida ya wanadamu tukizidiwa tunatafuta kisingizio cha kujificha.

Kete ziko kwa maadui, usiwaache tu afu useme Mungu atatenda. Pambana mwenyewe ushinde. Mungu huyo hawezi kukusaidia in reality, wewe ulisaidiwa na aliekupigia simu.
...Pole, Mkuu !...
 
Huyo Mungu mbona hajioneshagi, miaka 4000+
Anamtegemea mwanadamu badala ajitetee mwenyewe.

Mungu wenu mliyemtunga nyie siyo mwema.
Mmempa sifa za hovyo mpaka akapoteza mantiki.
...Mkuu Smotor, Kwa Nini unatumia Nguvu nyingi kujaribu kutuaminisha kwamba hakuna Mungu ?

SI utuache TU na Ujinga Wetu wa Kuendelea Kuamini kwamba Kuna Mungu,
na Wewe Uendelee TU na Ujanja wako wa Kuendelea Kuamini kwamba HAKUNA Mungu ?
Tatizo liko Wapi ?
 
Back
Top Bottom