Kampuni ya Dubai kuendesha Tanzania Airways

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
645
KAMPUNI ya Glasgow International GT LLC ya Dubai imekubali kuwekeza
nchini kwa kuanzisha shirika jipya la ndege linalotarajiwa kuanza
kutoa huduma zake katika kipindi cha miezi sita ijayo kuanzia sasa.

Makubaliano hayo yalifanyika jana jijini hapa baada ya kufanyika
kikao baina na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu na Mwenyekiti wa Bodi ya
Kampuni ya Glasgow International General Trading LLC ya Falme za
Kiarabu, Bahram Taherian.


Mwenyekiti huyo akiwa ameambatana na ujumbe wa Maofisa wa Kampuni
hiyo alieleza nia yake ya kuwekeza nchini kwa kuanzisha Shirika la
Ndege litakaloitwa Tanzania Airways.


Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika kikao hicho, ndege za kampuni hiyo zitakuwa zikifanya safari zake hapa nchini ili
kuongeza ushindani katika huduma hiyo ya usafiri wa anga na baadaye
litafanya safari za nje ya nchi.

Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri Nundu alipozungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kikao hicho, viongozi wa Kampuni hiyo wamekubali kuanzisha shirika jipya la ndege katika kipindi cha miezi
sita ijayo ili kuboresha upatikanaji wa usafiri wa anga.


Nundu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga alisema kuanzishwa kwa
shirika hilo jipya kutakuwa kumefungua ukurasa mpya katika ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga hapa nchini ambapo hata bei ya nauli
itakupungua kutokana na kuongezeka kwa ushindani katika utoaji wa
huduma hiyo.


Alisema katika makubaliano hayo shirika hilo litakuwa na makao yake
hapa nchini pamoja na kufuata sheria zote za nchi ikiwa ni pamoja na
kulipa kodi ambapo Serikali haitakuwa na ubia na shirika hilo

Hizi ni miongoni na hatua zinachokuliwa na Serikali ya awamu ya nne katika kuboresha huduma ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi na utoaji wa huduma hiyo kwa maendeleo ya
Taifa.
 
Hata huyo waziri Nundu sio Creative.

Air Tanzania ingeuza Shares kwa watanzania. Air tanzania wauze shares za 51% kwa watanzania na hivyo management ikakuwa na mix of people. hivyo ubadhirifu hautakuwepo na kutakuwa na efficiency. Pia litakuwa shirika la Watanzania.

Angalia kenya Airways, Serikali ya kenya ina some % na watu wa kenya wana some % na ni heshima kwa kenya.

Hata Uganda Air na Rwandese Airlines.

OOh poor Tanzania, Tanzania is poor because of poor minds of leaders.

OOh Tanzania leaders, selfishness thinking of 10% is killing Tanzania softly.
 
Hata huyo waziri Nundu sio Creative.Air Tanzania ingeuza Shares kwa watanzania. Air tanzania wauze shares za 51% kwa watanzania na hivyo management ikakuwa na mix of people. hivyo ubadhirifu hautakuwepo na kutakuwa na efficiency. Pia litakuwa shirika la Watanzania.Angalia kenya Airways, Serikali ya kenya ina some % na watu wa kenya wana some % na ni heshima kwa kenya.Hata Uganda Air na Rwandese Airlines.OOh poor Tanzania, Tanzania is poor because of poor minds of leaders. OOh Tanzania leaders, selfishness thinking of 10% is killing Tanzania softly.
Siku hizi ni 20%.
 
KAMPUNI ya Glasgow International GT LLC ya Dubai imekubali kuwekeza
nchini kwa kuanzisha shirika jipya la ndege linalotarajiwa kuanza
kutoa huduma zake katika kipindi cha miezi sita ijayo kuanzia sasa.

Makubaliano hayo yalifanyika jana jijini hapa baada ya kufanyika
kikao baina na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu na Mwenyekiti wa Bodi ya
Kampuni ya Glasgow International General Trading LLC ya Falme za
Kiarabu, Bahram Taherian.

Mwenyekiti huyo akiwa ameambatana na ujumbe wa Maofisa wa Kampuni
hiyo alieleza nia yake ya kuwekeza nchini kwa kuanzisha Shirika la
Ndege litakaloitwa Tanzania Airways.

Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika kikao hicho, ndege za kampuni hiyo zitakuwa zikifanya safari zake hapa nchini ili
kuongeza ushindani katika huduma hiyo ya usafiri wa anga na baadaye
litafanya safari za nje ya nchi.

Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri Nundu alipozungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kikao hicho, viongozi wa Kampuni hiyo wamekubali kuanzisha shirika jipya la ndege katika kipindi cha miezi
sita ijayo ili kuboresha upatikanaji wa usafiri wa anga.

Nundu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga alisema kuanzishwa kwa
shirika hilo jipya kutakuwa kumefungua ukurasa mpya katika ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga hapa nchini ambapo hata bei ya nauli
itakupungua kutokana na kuongezeka kwa ushindani katika utoaji wa
huduma hiyo.

Alisema katika makubaliano hayo shirika hilo litakuwa na makao yake
hapa nchini pamoja na kufuata sheria zote za nchi ikiwa ni pamoja na
kulipa kodi ambapo Serikali haitakuwa na ubia na shirika hilo

Hizi ni miongoni na hatua zinachokuliwa na Serikali ya awamu ya nne katika kuboresha huduma ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi na utoaji wa huduma hiyo kwa maendeleo ya
Taifa.
Waache waanzishe lakini jina libaki air tanzania, tanzania airways ndo nini sasa???????????
 
Magamba kwa nini wasi-give up tu kwene kumiliki shirika la ndege? is it neccessary kuwa na shirika la ndege la umma na kuendelea kufuja ela ya walipa kodi kwene shirika ambalo lilishakufa kitambo sana?
 
Hata huyo waziri Nundu sio Creative.

Air Tanzania ingeuza Shares kwa watanzania. Air tanzania wauze shares za 51% kwa watanzania na hivyo management ikakuwa na mix of people. hivyo ubadhirifu hautakuwepo na kutakuwa na efficiency. Pia litakuwa shirika la Watanzania.

Angalia kenya Airways, Serikali ya kenya ina some % na watu wa kenya wana some % na ni heshima kwa kenya.

Hata Uganda Air na Rwandese Airlines.

OOh poor Tanzania, Tanzania is poor because of poor minds of leaders.

OOh Tanzania leaders, selfishness thinking of 10% is killing Tanzania softly.

the problem we have kama watanzania ni kutangaza mambo tunayoongea kwenye chai au kahawa... we had the chinese here, then we were told tunanunua ndege nyingi tu, now dubai etc. wakati fly 540 never trumpeted anything but they brought ndege...

there is something wrong with our business model and communication tactis, everything is sooo political and utopic that one find it unrealistic

I hope Nundu understands where he is in terms of realism otherwise his name will really mean the nundu rather than Nundu
 
Hata huyo waziri Nundu sio Creative.

Air Tanzania ingeuza Shares kwa watanzania. Air tanzania wauze shares za 51% kwa watanzania na hivyo management ikakuwa na mix of people. hivyo ubadhirifu hautakuwepo na kutakuwa na efficiency. Pia litakuwa shirika la Watanzania.

Angalia kenya Airways, Serikali ya kenya ina some % na watu wa kenya wana some % na ni heshima kwa kenya.

Hata Uganda Air na Rwandese Airlines.

OOh poor Tanzania, Tanzania is poor because of poor minds of leaders.

OOh Tanzania leaders, selfishness thinking of 10% is killing Tanzania softly.
Nyie bwana hivi unadhani shares zinauzwa tu. Yaani air Tanzania wakianza kuuza shares kwa hali ya sasa hakuna atakayenunua. Na atakayenunua naye lazima atakuwa hafaham anachofanya au anahitaji kupimwa akili. Unanunua share kwenye kampuni ambayo ni loss making??? Huu utakuwa wizi wa wazi. ukinunua shares unakuwa mmiliki that means ile loss pale na wewe una mgawo. Shirika lile kwa sasa ni gumu saana kuuzika angalau liwe kwenye break-even. Otherwise madai ya kwamba shirika limeuzwa ni kwamba litauzwa kwa bei ya ajabu. Ndio maana unasikia kila siku Wachina mara wananihii.
Hapa tatizo ni kuoneana aibu katika kufanya maamuzi. Shirika lile lingeachana kwanza na habari ya kuweka mtaji. Wangeanza kufumua ule mfumo. Wanahitaji wafanyakazi wachache saana. Halafu waangalie mali zinazomilika na shirika kwa hali ya sasa ya kibiashara. Waangalie incentives za wafanyakazi na wazibe mianya ya wizi. Walipe madeni yao yote. Kisha wakodi ndege 2-3 tu. Wauze shares kwa Watanzania na mashirika ya kueleweka ya ndege yenye uzoefu ndipo biashara ianze. Na watu wa serikali waache kupanda ndege zao kwa mkopo.
 
Hata huyo waziri Nundu sio Creative.Air Tanzania ingeuza Shares kwa watanzania. Air tanzania wauze shares za 51% kwa watanzania na hivyo management ikakuwa na mix of people. hivyo ubadhirifu hautakuwepo na kutakuwa na efficiency. Pia litakuwa shirika la Watanzania.Angalia kenya Airways, Serikali ya kenya ina some % na watu wa kenya wana some % na ni heshima kwa kenya.Hata Uganda Air na Rwandese Airlines.OOh poor Tanzania, Tanzania is poor because of poor minds of leaders. OOh Tanzania leaders, selfishness thinking of 10% is killing Tanzania softly.
Umenikumbusha shea zangu nilizonunua tz oxygen limited mwaka wa kumi na kitu sijaambulia hata nilu ya kupiga kwenye kibanda changu. Unanitia uchungu maana zile noti za blue nazikumbuka kama nazitoa sasa hivi pale nbc mazengo branch dom mkuu usinikumbushe machungu.
 
Back
Top Bottom