sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
KAMPUNI ya Glasgow International GT LLC ya Dubai imekubali kuwekeza
nchini kwa kuanzisha shirika jipya la ndege linalotarajiwa kuanza
kutoa huduma zake katika kipindi cha miezi sita ijayo kuanzia sasa.

Makubaliano hayo yalifanyika jana jijini hapa baada ya kufanyika
kikao baina na Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu na Mwenyekiti wa Bodi ya
Kampuni ya Glasgow International General Trading LLC ya Falme za
Kiarabu, Bahram Taherian.


Mwenyekiti huyo akiwa ameambatana na ujumbe wa Maofisa wa Kampuni
hiyo alieleza nia yake ya kuwekeza nchini kwa kuanzisha Shirika la
Ndege litakaloitwa Tanzania Airways.


Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika kikao hicho, ndege za kampuni hiyo zitakuwa zikifanya safari zake hapa nchini ili
kuongeza ushindani katika huduma hiyo ya usafiri wa anga na baadaye
litafanya safari za nje ya nchi.

Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri Nundu alipozungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kikao hicho, viongozi wa Kampuni hiyo wamekubali kuanzisha shirika jipya la ndege katika kipindi cha miezi
sita ijayo ili kuboresha upatikanaji wa usafiri wa anga.


Nundu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga alisema kuanzishwa kwa
shirika hilo jipya kutakuwa kumefungua ukurasa mpya katika ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga hapa nchini ambapo hata bei ya nauli
itakupungua kutokana na kuongezeka kwa ushindani katika utoaji wa
huduma hiyo.


Alisema katika makubaliano hayo shirika hilo litakuwa na makao yake
hapa nchini pamoja na kufuata sheria zote za nchi ikiwa ni pamoja na
kulipa kodi ambapo Serikali haitakuwa na ubia na shirika hilo

Hizi ni miongoni na hatua zinachokuliwa na Serikali ya awamu ya nne katika kuboresha huduma ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi na utoaji wa huduma hiyo kwa maendeleo ya
Taifa.
Mwenyekiti huyo akiwa ameambatana na ujumbe wa Maofisa wa Kampuni
hiyo alieleza nia yake ya kuwekeza nchini kwa kuanzisha Shirika la
Ndege litakaloitwa Tanzania Airways.


Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa katika kikao hicho, ndege za kampuni hiyo zitakuwa zikifanya safari zake hapa nchini ili
kuongeza ushindani katika huduma hiyo ya usafiri wa anga na baadaye
litafanya safari za nje ya nchi.

Kwa mujibu wa maelezo ya Waziri Nundu alipozungumza na waandishi wa
habari mara baada ya kikao hicho, viongozi wa Kampuni hiyo wamekubali kuanzisha shirika jipya la ndege katika kipindi cha miezi
sita ijayo ili kuboresha upatikanaji wa usafiri wa anga.


Nundu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Tanga alisema kuanzishwa kwa
shirika hilo jipya kutakuwa kumefungua ukurasa mpya katika ukuaji wa sekta ya usafiri wa anga hapa nchini ambapo hata bei ya nauli
itakupungua kutokana na kuongezeka kwa ushindani katika utoaji wa
huduma hiyo.


Alisema katika makubaliano hayo shirika hilo litakuwa na makao yake
hapa nchini pamoja na kufuata sheria zote za nchi ikiwa ni pamoja na
kulipa kodi ambapo Serikali haitakuwa na ubia na shirika hilo

Hizi ni miongoni na hatua zinachokuliwa na Serikali ya awamu ya nne katika kuboresha huduma ya usafiri wa anga ili kuongeza ufanisi na utoaji wa huduma hiyo kwa maendeleo ya
Taifa.