Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK

Kuna siku moja rafiki yangu mmoja alikwenda harusini akiwa amevalia vizuri sana tena alivyokuwa na pamba za uhakika kila mtu alisema kweli jamaa yule kapendeza sana. Halafu kumbe jamaa alikuwa na nafasi fulani kwenye ukoo wa maharusi, kwa hiyo alipata nafasi ya kutoa nasihi zake. Jamaa yule alitoa hotuba nzuri sana yenye maadili mazuri sana kwa maharusi na watu wtote waliokuwapo pale. Mojawapo ya maadili lilihusu maharusi kujiheshimu ili waweze kuheshimiwa na wengine.

Baada ya hotuba ile, jamaa akabugia pombe mpaka akajisadia kwenye nguo pale pale ukumbini na kulala chini akiwa hoi bin-taabani huku uharo wake ukiwa unasambaa hovyo hovyo hadi ikabidi sherehe ya harusi ifungwe.
Kesho yake gumzo lilikuwa jinsi jamaa huyo alivyojisadia kwenye nguo na kuzidiwa na pombe hadi akalala chini ukumbini huku akiwa na kinyesi kwenye nguo zake. Hakuna aliyekumbuka kuwa alikuwa jamaa alikuwa amevalia nguo nzuri na alikuwa ametoa maadili mazuri.

Inawezekana kweli Lowasa aliwahi kufanya mambo mazuri ikiwa ni pamoja na kukemea uuzwaji wa viwanja kiholela pale Dar, na kuhusu matumizi ya maji ya Ziwa Victoria. Hata hivyo, uharo wa rushwa aliolalia kwenye nguo ndio signature identity yake na wala hatutaisahau hata akijisafisha vipi. Kwa sasa hivi tunafahamu kuwa hata vile viwanja alivyokuwa akikemea uuzwaji pale Dar, baadaye vilikuwa uzwa na alipokea rushwa. Kila jambo afanyalo jamaa huyu huwa liko kalikulatedi kumpa ulaji fulani binasfi, siyo kwa maslahi ya taifa. Swala la maji ya Ziwa Victoria lilikuwa kalikulated kumfanya aonekane mchapa kazi ili aweze kuwania ama urais au nafasi kubwa zaidi serikalini.
 
Kichuguu,
Umeelezea vizuri sana. Nimejaribu kutafuta maneno ya kuelezea "uhodari" wa Lowassa katika utendaji kazi wake na ufisadi wake nikashindwa. Kwa hili nakushukuru kutupa wote hapa tuisheni. Hata wale wanaomshangilia Mkapa itabidi wafikirie jinsi alivyojitapikia na kujinyea kirushwa na hivyo ndivyo atakavyokumbukwa. You cannot serve 2 masters at the same time. Ama uamue kujihudumia au kuwahudumia Watanzania.
 
Ni kweli hakupata mpinzani kwa sababu ya kutumia jamaa wa special branch.
 
Katika siku za karibuni kumekuwa na magazeti luluki yaliyoanzishwa na JF ilikuwa ya kwanza kubaini mapema mikakati ya magazeti hayo

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-ya-karamagi-co-dhidi-ya-jakaya-kikwete.html

Lakini pamoja na hayo nikamkumbuka sana ndugu yangu, Ansbert Ngurumo katika makala yake hii ambayo naamini itawapa darasa waandishi na wahariri ambao bado wako usingizini. Mungu atawapa mwanga na kujua waendako.



Makala -Kosa kuu la Kikwete, Lowassa na Rostam
 

- Ngurumo ninamkubali siku zote, huwa hachanganyi maneno Tanzania tunahitaji waandishi watatu tu kama yeye inatosha, nimeona makala moja ya Balile kuhusu Mboma kugombea ubunge, yaani nasikia hata kutapika.

Bravo Ngurumo, maana uandishi wako unakubalika hata na wakulu wengi wa taifa, ninakutobolea siri mkuu karibu wote huwa hawakosi nakala zako kwenye briefcase zao.
 
- Sina uhakika na hilo, lakini arcticle zake huwa ni sindano ya moto kwa viongozi wa vyama vyote vya siasa, na hasa mafisadi.
 
Hatujali chama. kama lengo lake ni kuwapinga mafisadi poa tu.

Article imesimama sana naikubali mkuu wangu.
 
Dah Huku mbagala ni saa karibu sita usiku. mzee ES siku njema mkuu na heri na fanaka za mwaka mpya!

Ufisadi utatukoma toka tuanze miaka hiyo 2005. Tupo pamoja. Halafu mbona wapiganaji wapya ndo wanatokomea?
 

Mkuu FMES inasikitisha. Ila wanasema penye udhia penyeza rupia. Niliambiwa kuwa wana-Apolo walisaidia sana katika mapokezi yale. Michangi mikubwa ya fedha hubadilisha akili za watu.
 

Nakubaliana sana na wewe Mkuu. Kwa kuongezea tu, UVCCM ndio waliopendekeza JMK na EL wachukue form za kugombea URais 1995. Na wao (UVCCM) ndio waliahidi kusaidia ushindi wao. Ikumbukwe pia kwamba, mwaka ule walijitokeza wagombea wengi kuliko wakati wowote wa chaguzi za ndani (CCM) siku za nyuma.

Wasiwasi wangu mkubwa kuhusiana na EL ni ubinafsi wake. Kuna issue moja ambayo hadi leo siielewi, inashangaza na inauma sana. Nayo ni ubomoaji wa jengo kubwa (apartments) karibu na nyumba yake aliyopangisha kwa ubalozi wa SA. Jengo lile lilibomolewa kwa kisingizio kuwa lilikosa hati zilizohitajika kulijenga (building permits). Na hata hati hizo zilipotolewa na wahusika, zilikataliwa na baadhi wa watendaji wa Municipal ya Kinondoni walichukuliwa hatua kutokana na kutoa hati hizo. Inasemekana Jengo lilibomolewa kwasababu kuwepo kwake kulizuia hewa nzuri kufikia nyumba yake (Ubalozi wa SA). Naamini kuwa kama jengo lile lingekuwa la mtu mwingine, lisingebomolewa. Na hata kama halikuwa na uhalali wa kuwepo, ingekuwa busara zaidi kutoza "fine" kubwa kwa wamiliki ili iwe fundisho, kuliko kuacha masalia yake yasiyopendeza kabisa.
 
Phillemon Mikael mkuu, kuna kitu kimoja umekisema katika mchango wako ambacho nadhani wanajanvi hawakichukulii seriously ingawa ni muhimu sana kwa utawala wa Jakaya; nacho ni role ya SANGOMA katika maamuzi. Ni kweli usiopingika kuwa waganga wa kienyeji wanainfluence sana na maamuzi ya muungwana kwahiyo kama alivyosema Mikael siyo ripoti ya Mwakyembe peke yake iliyomfanya Jakaya amtose Lowassa bali ni ushauri wa waganga wake wa kienyeji kuwa huyu bwana alikuwa anampiku mwaka 2010. Hata wakati wa mchakato pale DODOMA mwaka 2005 Jakaya alikuwaanatembea na SANGOMA wake kwenye Cruiser lake.; wengine anaimport toka West Africa!! sasa kwa imani potofu namna hiyo uongozi utaleta maendeleo au maaalbino wataachwa kuchinjwa kweli??
 
...............duh!!!!!!!!!!!!....................JUJUMAN ndani ya IKULU?????
 

Ndio maana muungwana huwa anapagawa wakati mwingine ggggrrrrrrrrrrrrrrrrrrhhhh! Kweli Nyerere aliona mengi, aliweza kutueleza machache tu. Mengine tutasoma wenyewe kwa nyakati. Nilifikiri Muungwana kaacha masangomaism!
Mkuu Bulesi,
Hivi hayo Masangoma hayapokei 'rushwa' tuyape hoja zetu za mafisadi na mustakabali wa taifa?
 

Nimesoma, hakuna hoja hapa!

Bye bye thread
 
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/22374-sauti-huru-anguko-la-mengi-kama-maxell-3.html

Mod na hii ya Sauti Huru ingewekwa humu kwani ina uhusiano mkubwa kwa kuwa nalo ni miongoni mwa magazeti yaliyoanzishwa mahsusi kuwatetea watu ambao jamii imeamini na serikali imeamini na kuwachukulia hatua. Hii ni hatari, lazima tukatae kulishwa sumu hii mbaya na tena bila hoja. Kuna gazeti moja limethubutu hata kusema kwamba VITA YA UFISADI NI VITA KATI YA WACHAGA NA WAHAYA na bado Mkuchika na jamaa zake wa Maelezo hawajachukua hatua kwa habari/makala inayolenga kuchochea mgawanyiko wa kikabila. HII NI HATARI KUBWA NA SIJUI hao UWT wanafanya kazi gani.

Lakini habari ya Sauti Huru sijui kama ni habari ama makala
 
Nimesoma kwa mshangao sifa anazotupiwa Lowasa,kabla ya kumpamba mtu kwa sifa ni bora uangalie uadilifu wake kwanza Mh: huyu hana tofauti na Mkapa kwa waliyowatendea wananchi wa Tanzania si watu wa kusifiwa hawa. Mkapa ni mung'unye ameharibikia ukubwani ameanza wizi ktk hatua za mwisho za kipindi cha pili cha uraisi wake. Lowasa nimebahatika kumjua kidogo ktk miaka ya mwanzoni mwa 80 nilipokuwa Arusha wakati huo nchi inanuka hamna bidhaa,chakula ,nguo nk naye alikuwa katibu wa CCM mkoa by then alishaharibika kwa ulafi. alipopewa uwaziri ndipo alipofungulia mbwa akasema mtanikoma, kiasi hayati mwl Nyerere akamwambia hafai kuwa raisi mtoto mdogo mwenye tamaa ya mali, bahati mbaya na huyo mtoto mkubwa alietupa ndio akawa MZINGA MBOVU unalipuka ovyo kwa tamaa na ufisadi. kwakifupi hawa jamaa ni magabacholi tu hawastahili sifayeyote. wamejivua heshima ya kusifiwa kitambo.
 

- Mkuu Jujuman, saafi sana maneno mazito sana haya.
 

Hakuna JARS zozote hizo ni imani potofu na zimepitwa na wakati harafu ni stori za vijiweni,kwanza humu duniani hakuna sangoma lolote sangoma ni wewe mwenyewe ama rafiki yako.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…