Kampeni chafu zaanza UVCCM

Anatembea taratibu mikono mfukoni.
Uso umejaa soni.
Anatazama chini huku kichwa kimeinamia upande .
Midomo imetengeneza umbo la kutabasamu pia yapiga miluzi ya kujikonga
Miguu yaenda ikipiga maganda makavu ya miwa njiani kwa namna ya kujiliwaza.
Macho yamejaa malengelenge
koo limemkauka.
Na nyimbo zimemwishia.
Amebakia na miluzi

Huyoo
Taratibu ajikongoja kurudi mawiyoni mwake.
 
JK inabidi akae kimya na awaache vijana ( Makalla ) wawajibu viongozi wa dini turned into politicians ! JK is way far ahead in politics with this newly political recruits !

Dude are you serious??? I really hope for the sake of everybody's sanity that you are being sarcastic.
 
Anatembea taratibu mikono mfukoni.
Uso umejaa soni.
Anatazama chini huku kichwa kimeinamia upande .
Midomo imetengeneza umbo la kutabasamu pia yapiga miluzi ya kujikonga
Miguu yaenda ikipiga maganda makavu ya miwa njiani kwa namna ya kujiliwaza.
Macho yamejaa malengelenge
koo limemkauka.
Na nyimbo zimemwishia.
Amebakia na miluzi

Huyoo
Taratibu ajikongoja kurudi mawiyoni mwake.

Hapa umekandamiza kabisaaaaaa Madela mwana wa Madilu
 
uliyosema hapao juu mwewe siyafahamu kiundani, lakini nasema hivi, hao viongozi wa upinzani watadebate na vijana, JK is busy working for the people !

Kweli bwana, JK yuko busy anapanga mikakati ya namna ya kugawana "Sungura" na wanamtandao wenzake!!!
 
uliyosema hapao juu mwewe siyafahamu kiundani, lakini nasema hivi, hao viongozi wa upinzani watadebate na vijana, JK is busy working for the people !
Working for the people? Wakati kasema hata hajui kwanini watu wake ni maskini?
 
alisema hajui matatizo ya watu wake au hajui kwa nini maendeleo hayapatikani ?
 
Jibu la swali la swali hilo alitegemea alipate New York? Nini sasa Dira yake?
 
Hivi kuna mtu alimuuliza huyo MvCCM amejuaje kuwa maandamano ya wapinzani yanayokuja hayana jipya? yakiwa na jipya atasemaje?
 
Wanachama wa uvccm mbeya wameomba rais kikwete kuanza mara moja kukikwamua chama cha mapinduzi uvccm.mapema kbala ya maafa haayajanza kuonekana...wanachama hao walitoa ushauri kufuatia kitendo cha katibu mkuu nchimbi kumvua katibu mkuu wa uvccm mkoa wa tanga bw mwita waitara
walisema hatua ya nchimbi kufanya chama kama familia yake kitaleta maafa ya ajabu uko mbele tuendako..wakiongea na waandishi wa habari wamesema nchimbi ana siasa za chuki hasa kwa wale viongozi walioamuwa kuwa mstari wa mbele kwenye ufisadi...huy jamaa mshenzi sana anatishia kuwalinda mafisadi hata kwa damu akijigamba kabisa ...atakaethubutu atatoka nae...tumemwambia aende tanga akaone mambo...na wanamsubiri kwa hamu kweli....
Wameomba kikwete na cheo chake akinusuru chama mapema na kuthibiti viongozi wa jumuia za ccm ambao wanaendesha siasa za chuki.. Kama utawendelea hivi 2009 kuna shuguli na wameapa kufundishana....
Kwenu ccm kila la kheri...
Tutawasaidia mrekebishane ila msiumize tu wananchi

rgds
mama mia....
 
Date::11/10/2008
Mfanyabiashara atoa Sh400milioni kugharimia mkutano UVCCM

Na Daniel Mjema, Dodoma

MFANYABIASHARA mashuhuri nchini, Tanil Somaiya anayemiliki Kampuni ya Shivacom ametoa Sh400 milioni kugharamia Mkutano wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Vijana (UVCCM) unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.


Mfanyabiashara huyo alikabidhi msaada huo unaohusisha vifaa vyenye thamani ya Sh250 milioni na fedha taslimu Sh150 milioni za posho za wajumbe wanaokadiriwa kuwa 1,000, kwa Mwanyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete katika tafrija fupi iliyofanyika Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma.


Kabla ya kukabidhiwa kwa msaada huo, Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Francis Issack alisema katika kufanikisha mkutano huo wa uchaguzi, Baraza Kuu la UVCCM liliamua kuteua kamati maalumu ya watu wanne ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma William Lukuvi, kutafuta fedha.


Wajumbe wengine wanaounda kamati hiyo ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Lawrence Masha, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Somaiya.




Issack alisema Baraza Kuu la UVCCM liliwaagiza kutafuta vifaa 1,000 kila kimoja ambavyo ni pamoja na fulana, kofia, mabegi, kalamu na madaftari ambavyo vilitengenezwa kwa gharama ya Sh250,000 katika kiwanda kinachomilikiwa na Somaiya mwenyewe.


Kwa mujibu wa kaimu katibu huyo, ingawa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa UVCCM Taifa ni 750 lakini wapo waalikwa ambao ni pamoja na Rais Kikwete na wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM ambao pamoja na wajumbe wengine watalipwa posho ya Sh50,000 kwa siku.


Akikabidhi msaada huo, Somaiya alisema ameamua kukisaidia chama hicho kwa kuwa yeye ni mkereketwa na mpenzi wa CCM, kauli ambayo ilipongezwa na Rais Kikwete ambaye alisema kwa kutoa msaada huo, mfanyabiashara huyo atakuwa amejitangaza kibiashara.


Tafrija hiyo fupi ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwemo wajumbe wa NEC waliomaliza kikao chao jana mchana na kupitisha majina ya wanachama wanaogombea nafasi mbalimbali za uongozi UVCCM, Jumuiya ya Wanawake (UWT) na Jumuiya ya Wazazi.



Katika hatua nyingine, wazee wa CCM wa wilaya ya Dodoma mjini wamemuomba Rais Kikwete kuharakisha mpango wake wa kupitisha utaratibu unaotenganisha suala la uongozi na biashara ndani ya Serikali na ndani ya chama cha Mapinduzi.



Akisoma risala kwa niaba ya wazee hao Ikulu ndogo mjini Dodoma jana, Mohamed Makbel alisema bila maadili hakuna nidhamu na kutaka linalowezekana leo lisingoje kesho.


“Pamoja na hayo ili kulinda umoja wetu tunaomba viongozi wetu wa chama na serikali wanapotofautiana watumie vikao husika vya chama,” ilisema sehemu ya risala hiyo.


Pia waliomba kupitiwa kwa sheria ya mwaka 1979 iliyoagiza Dodoma kuwa eneo maalumu la uwekezaji ili sheria hiyo ihuishwe kuwawezesha wawekezaji wengi kuwekeza Dodoma na kuufanya mkoa huo kuwa kitovu cha usambazaji wa bidhaa mbalimbali katika nchi za Afrika Mashariki na Kati.


Walimpongeza Rais Kikwete kwa uamuzi wake wa ujasiri wa kuamua kujenga chuo kikuu cha Dodoma na ujenzi wa uwanja wa kisasa wa ndege wakisema uamuzi huo umeongeza shauku kubwa ya maendeleo ya kiuchumi ya mkoa huo wa Dodoma.


Akiwahutubia wazee hao, Rais Kikwete alisema azima ya serikali ya makao makuu kuhamia Dodoma iko palepale na kwamba amefarijika na hotuba ya wazee hao kwani imeonyesha namna ambavyo bado wako pamoja na serikali yao katika kupigania maendeleo ya wananchi.


Kuhusu suala la kuufanya mkoa wa Dodoma kuwa eneo huru la kibiashara, Rais alisema utekelezaji wa suala hilo ulikwishaanza japo kasi yake haiendi kama ilivyotarajiwa lakini aliahidi kuwa serikali italitazama suala hilo ili shabaha iliyokusudiwa na Serikali iweze kufanikishwa.
 
Hii kali!! Na huyu Somaiya akiwa kwenye issue ya EPA watamkamata kweli?
 
400m. Halafu huyu mtathubutu kumwambia kitu? Mtu akikufadhili kwa kiwango hiki unakuwa huna ubavu wa kusema chochote, hata akisema chochote lazima ukenue meno hata kama inakuuma vipi! haya na tuone. Kina Fisadi Shah wengine hao!
 
Tanil Somaiya anayemiliki Kampuni ya Shivacom ametoa Sh400 milioni kugharamia Mkutano wa Uchaguzi wa Jumuiya ya Vijana (UVCCM) unaotarajiwa kufanyika mwezi ujao.


Mfanyabiashara huyo alikabidhi msaada huo unaohusisha vifaa vyenye thamani ya Sh250 milioni na fedha taslimu Sh150 milioni za posho za wajumbe wanaokadiriwa kuwa 1,000, kwa Mwanyekiti wa CCM Rais Jakaya Kikwete katika tafrija fupi iliyofanyika Makao Makuu ya chama hicho mjini Dodoma.

Huyu anatafuta nini kufutiwa kodi?
Tulisha ambiwa hawalipi kodi hawa jamaa ndo kulipa fadhira nini?
Ameacha kuchangia maendeleo huko vijijini kwa kutoa madawati yeye anafadhili ufisadi.
Anajitengenezea jina..
 
Huyu anatafuta nini kufutiwa kodi?
Tulisha ambiwa hawalipi kodi hawa jamaa ndo kulipa fadhira nini?
Ameacha kuchangia maendeleo huko vijijini kwa kutoa madawati yeye anafadhili ufisadi.
Anajitengenezea jina..

Mkulu,

Unadhani akichangia madawati NEC watamuona?NEC ndio Serikali
 
Mkulu,

Unadhani akichangia madawati NEC watamuona?NEC ndio Serikali

Mkuu nimeamini ukiwa na mihela uwe karibu na viongozi na kutoa toa viposho hata kama 5000 kwa kila mjumbe basi utalindwa balaa.Hata ukitaka kugombea ujumbe wa NEC hutumii nguvu nyingi kama wengine.
 
Chenji ya kwenye rada ndio inarudishwa hiyo, badala ya kulinufaisha Taifa inainufaisha CCM peke yake!
 
Back
Top Bottom