A
Anonymous
Guest
Sisi Wananchi wa Mkoa wa Kigoma, Wilaya ya Buhigwe, Kijiji cha Mwayaya kwa sasa tunaishi kwa hofu na manyanyaso makubwa, tunafanyiwa ukatili mkubwa ambao hauvumiliki na hawa matapeli wanaojiita KAMCHAPE pamoja na Kamati yao ambayo inaongozwa na Viongozi wa Kijiji, Diwani na Wajumbe kadhaa.
Wananchi tunalazimishwa kuaminishwa ushirikina ambao wengine siyo waumini wa hayo mambo, tukikataa tunapigwa, Wazee wananyanyaswa, Watu wananyang'anywa mali zao, mifugo wengine wanavuliwa nguo hadharani, wanadhalilishwa utu wao pale unapokataa kuamini uchawi wao.
Wengine wanatozwa hela hadi shilingi milioni 2, then hao KAMCHAPE na watu wao wanagawana, kibaya zaidi wanapora mifugo na mali za watu waziwazi kwa kivuli kuwa wanaondoa uchawi.
Tumesharipoti kwenye Jeshi la Polisi mara nyingi lakini hakuna msaada ambao tunapata, wanaishia kutuambia kuwa tupambane nao wenyewe.
Swali la kujiuliza hivi na sisi Wananchi tukiamua vita dhidi ya kikundi hicho ambacho wamekuwa kama Panya Road kutokana na kutembea na silaha za jadi ikiwemo mapanga na marungu, kutakalika?
Mwanzoni walianza kuwafikia watu wanaohisi kweli wanahusika na imani hizo, lakini kadiri muda unavyoenda mbele ndivyo wanavyonogewa na kufuata watu wengine ambao hata hawahusiki, ili mradi tu waone ana mazingira ya kuwa na chochote (hela au mali).
Wakifika kwako wanakwambia utoe shilingi 5,000 kisha maelekezo mengine yaendelee, ukikataa wanakushambulia.
Kuna Mwananchi mmoja aligoma kuwapa ushirikiano akapambana nao, wakamkata panga baadaye wanachama hao wa KAMCHAPE wakaenda kuvamia shamba lake wakaharibu mazao, baadaye wakarejea na kuchoma moto nyumba na vibanda vyake.
Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu, Mkuu wa Jeshi la Polisi naomba mfahamu kuwa kinachoendelea huku kinaelekea kuwa vita rasmi kwa kuwa kama Jeshi la Polisi halitachukua hataa mapema kudhibiti Wananchi uvumilivu utatushinda.
Mbunge wetu wa Buhigwe, Felix Eliadory Kavejuru hajachukua hatua kudhibiti hiki kinachoendelea, tena hili ni Jimbo ambalo alikabidhiwa na Dkt. Philip Mpango ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais.
Wananchi tunalazimishwa kuaminishwa ushirikina ambao wengine siyo waumini wa hayo mambo, tukikataa tunapigwa, Wazee wananyanyaswa, Watu wananyang'anywa mali zao, mifugo wengine wanavuliwa nguo hadharani, wanadhalilishwa utu wao pale unapokataa kuamini uchawi wao.
Wengine wanatozwa hela hadi shilingi milioni 2, then hao KAMCHAPE na watu wao wanagawana, kibaya zaidi wanapora mifugo na mali za watu waziwazi kwa kivuli kuwa wanaondoa uchawi.
Tumesharipoti kwenye Jeshi la Polisi mara nyingi lakini hakuna msaada ambao tunapata, wanaishia kutuambia kuwa tupambane nao wenyewe.
Swali la kujiuliza hivi na sisi Wananchi tukiamua vita dhidi ya kikundi hicho ambacho wamekuwa kama Panya Road kutokana na kutembea na silaha za jadi ikiwemo mapanga na marungu, kutakalika?
Mwanzoni walianza kuwafikia watu wanaohisi kweli wanahusika na imani hizo, lakini kadiri muda unavyoenda mbele ndivyo wanavyonogewa na kufuata watu wengine ambao hata hawahusiki, ili mradi tu waone ana mazingira ya kuwa na chochote (hela au mali).
Wakifika kwako wanakwambia utoe shilingi 5,000 kisha maelekezo mengine yaendelee, ukikataa wanakushambulia.
Kuna Mwananchi mmoja aligoma kuwapa ushirikiano akapambana nao, wakamkata panga baadaye wanachama hao wa KAMCHAPE wakaenda kuvamia shamba lake wakaharibu mazao, baadaye wakarejea na kuchoma moto nyumba na vibanda vyake.
Mheshimiwa Rais Samia, Waziri Mkuu, Mkuu wa Jeshi la Polisi naomba mfahamu kuwa kinachoendelea huku kinaelekea kuwa vita rasmi kwa kuwa kama Jeshi la Polisi halitachukua hataa mapema kudhibiti Wananchi uvumilivu utatushinda.
Mbunge wetu wa Buhigwe, Felix Eliadory Kavejuru hajachukua hatua kudhibiti hiki kinachoendelea, tena hili ni Jimbo ambalo alikabidhiwa na Dkt. Philip Mpango ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais.