Gwakisa Mwandule
JF-Expert Member
- Jun 20, 2012
- 521
- 185
Acha aje huku sakafuni anafikiri urais ni uleigwanani?
Hashikiki ndani ya hicho chama cha mafisadi, tunamsubiri huku nje tumtie shinikizo la damu kwa matokeo ya ajabu ambayo hajawai kuyafikiria.
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
wewe unadhani huyu akisimama na Dr wa ukweli Mh wilbrod Slaa ataambulia kura ngapi? amini usiamini hata mil 1 hatapata. hao ccm wenyewe siku hizi wana kadi 2, moja ya huko wanachumia tumbo na nyingine ya CHADEMA. wanajua yeyote atakaye gombea na SLAA lazima achezee kichapo.Napata wasiwasi sasa....
Huyu bwana huenda kweli akashinda urasi, maana nilidhania watu wanatambua makosa yake kumbe wanamsherehekea.
Sina la kusema but nimehamini jamaa anaweza kuchukua dola yetu hapo nchini.
Yangu macho....ngoja nisubiri na kuona nini kitajiri.
Hashikiki ndani ya hicho chama cha mafisadi, tunamsubiri huku nje tumtie shinikizo la damu kwa matokeo ya ajabu ambayo hajawai kuyafikiria.
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Acheni kumsulubu mtu bila ushahidi.ufisad wa lowasa ni upi?hebu tajeni kwa ulinganifu na jk na riz,membe na sita
Mkuu BAK, nakushukuru kuanza kuukubali ukweli mchungu!. Kwa vile Tanzania ni nchi ya wala rushwa, inamaa kiongozi bora wa nchi yetu ni yule anayejua kutumia vizuri hii rushwa na bingwa wa matumizi ya fedha anafahamika!. Nawaombeni sana, tuipuuzie kabisa ile kauli ya Baba wa Taifa kuhusu hawa watu wa "kuogopwa kama ukoma". Sasa ndio tuwapende kama mboni za macho yetu!.Fisadi Lowassa nani ataweza kumshika wakati nchi yote inanuka rushwa!? Nchi ingekuwa na utawala bora huyu hata asingethubutu kutamka kama anataka kugombea ubalozi wa nyumba kumi kumi!!! achilia mbali kutaka kuwa Rais.
na Grace Macha, Arusha
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu Edward Lowassa amezidi kuwatimulia vumbi wapinzani wake ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kutokana na wajumbe wanaounga mkono kambi yake kuzidi kupeta katika uchaguzi. Katika uchaguzi wa Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha uliomalizika jana, kambi mbili zinazowaunga mkono Lowassa na Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe katika mbio za urais 2015, zilionekana kutifuana vikali.
Msuguano huo ulianza kujitokeza tangu juzi kwenye uchaguzi wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM) Mkoa huo, ambapo juhudi za Katibu wa Mkoa, Mary Chatanda kutaka kuihujumu kambi ya Lowassa, ziligonga mwamba na kunusurika kipigo.
Chatanda ambaye alikuwa akifanya juhudi za kuhakikisha mshindi anakuwa Dk. Harold Adamson, aliambulia patupu baada ya Robinson Meitinyiku anayedaiwa kuungwa mkono na Lowassa, kushinda kwa kura 247 dhidi ya 188 za mpinzani wake.
Katika mwendelezo huo huo wa msuguano wa kambi hizo mbil, jana Katibu huyo CCM Mkoa wa Arusha, Chatanda, alijikuta akiaibishwa na wajumbe wa mkutano Mkuu wa chama baada ya kujifanya amesahau kumtambulisha Lowassa. Chatanda aliufanya ukumbi mzima kupiga kelele kubwa wakisema bado! bado! Bado Eddo! Eddo! Eddo! Na ndipo kwa aibu kubwa, katibu huyo akameza mate na kumtambulisha Lowassa.
Hata hivyo, hatua hiyo ilitafsiriwa tofauti na baadhi ya wajumbe ambapo wengine walisema ni tukio la bahati mbaya, lakini wengi wao wakidai kuwa Chatanda alifanya makusudi kutokana na kundi analoliunga mkono kuanguka kwenye uchaguzi wa UVCCM. Katika mkutano huo mkuu wa mkoa uliohudhuriwa na wajumbe 833, nafasi ya Mwenyekiti ilirudi tena kwa Onesmo ole Nangole ambaye anadaiwa kuunga mkono na Lowassa, akiwaacha kwa mbali washindani wake wawili.
Nangole alijizolea kura 604 huku akifuatiwa kwa mbali na Adam Choro wakati Dk. Salash Toure aliyedondoshwa na Lowassa kwenye uchaguzi wa ujumbe wa NEC Taifa kupitia wilayani Monduli akiambulia kura 13. Akitangaza matokeo hayo, msaimamizi mkuu wa uchaguzi huo, Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe, alisema kura zilizopigwa ni 833 ambapo kura halali zilikuwa 830 na tatu ziliharibika.
Mapema akifungua mkutano huo kabla ya uchaguzi, Prof. Maghembe, aliwataka wajumbe kuacha kuzomea au kushangilia wagombea pindi watakapofika mbele yao kujinadi. Alisema lengo la uchaguzi huo ni kupata viongozi watakaojenga chama kwa kuhakikisha wanavunja makundi na kuwaunganisha wanachama wote ili kuvirejesha viti vya udiwani na ubunge walivyovipoteza mkoani humo.
"Msichague viongozi watakaobweteka na kutugawa, hawa hawatufai, tuepuke viongozi wa aina hii, tuchague watakaokisaidia chama," alisema Maghembe.
Naye Lowassa, akizungumza baada ya kuchaguliwa na wajumbe kuwa mwenyekiti wa muda wa mkutano huo, aliwashukuru wote kwa imani waliyompa huku akishangiliwa kwa kishindo. "Wajumbe nimewaelewa na sitawaangusha, nimewaelewa ndugu zangu sitawaangusha, nawashukuru kwa kunishangilia, ila sasa tusishangilie tusije kuharibu utaratibu," alisema Lowassa.
Akijinadi kwa wajumbe hao, Nangole aliwaomba wamchague ili aweze kusimamia dosari zilizopo na kushughulika na watu wote wanaoleta makundi ndani ya chama kwa mgawanyiko kuanzia wilayani mpaka Mkoa.
Naye Dk. Toure, aliwaomba wajumbe hao kuwa akichaguliwa, atamaliza makundi yaliyopo ambayo yamekiathiri chama hicho kwani wanachama wamegawanyika kila ngazi na kuwasihi wawabwage wagombea waliotumia fedha kuomba kura kwenye uchaguzi huo.
Mgawanyiko ndani ya chama ulionekana kuzungumzwa na kila mtu kwani hata Chora, naye aliwaomba wajumbe wamchague ili tatizo hilo alilodai kuwa limewapotezea majimbo.
Hashikiki ndani ya hicho chama cha mafisadi, tunamsubiri huku nje tumtie shinikizo la damu kwa matokeo ya ajabu ambayo hajawai kuyafikiria.
Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
Siasa zetu zinasikitisha
Napata wasiwasi sasa....
Huyu bwana huenda kweli akashinda urasi, maana nilidhania watu wanatambua makosa yake kumbe wanamsherehekea.
Sina la kusema but nimehamini jamaa anaweza kuchukua dola yetu hapo nchini.
Yangu macho....ngoja nisubiri na kuona nini kitajiri.
Waandishi wetu wa habari bado wanasafari ndefu sana,sasa ukisoma habari hiyo unashindwa kuelewa membe anaingiaje arusha kikubwa hapo ni hisia tu na umbea kutoka kwa magamba walioko katika kambi ya EL lakini kikubwa zaidi ushahidi wa mazingira hapo lazima kambi ya mzee iliwatumia ipasavyo waandishi wa habari kwa bei nafuu-safari bado ndefu kwa vyombo vya habari