Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Akizungumza jijini Dodoma Machi 24, 2026, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Mhe. Selemani Kakoso, alisema uamuzi huo unaenda sambamba na dhamira ya kuhakikisha miundombinu ya kisasa inaendelea kujengwa na kuboreshwa ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.
Kwa upande wake, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega ameishukuru Kamati hiyo kwa kuidhinisha randama hiyo na kuahidi kuwa Wizara itaendelea kusimamia kwa karibu utekelezaji wa miradi ya kimkakati ili kuhakikisha inakamilika kwa viwango bora na kuleta manufaa kwa wananchi.
Sambamba na hilo, Wizara imepanga kuendeleza ujenzi wa barabara za mzunguko wa ndani wa jiji la Dodoma, ikiwa ni jitihada za kupunguza msongamano wa magari. Miradi hiyo inahusisha barabara za Dodoma–Iringa, Dodoma–Singida, Dodoma–Arusha na Dodoma–Chamwino, ambapo kwa sasa ipo katika hatua za mwisho za kuwapata wakandarasi kwa ajili ya kuanza utekelezaji.