Tumaini Makene
JF-Expert Member
- Jan 6, 2012
- 2,642
- 6,071
KUFUATIA kifo cha Mbunge Jeremiah Sumari, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeamua mkutano wa kawaida wa Kamati Kuu ya chama uliokuwa ufanyike Zanzibar kuanzia Januari 21, 2012 mpaka Januari 22, 2012, sasa utafanyika Dar es Salaam.
CHADEMA imefikia uamuzi huo ili kuwezesha viongozi wake wakuu wa chama, wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Wilbrod Slaa kuwa karibu ili kujumuika na kuifariji familia ya marehemu pamoja na kushiriki katika kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu Sumari.
Mungu ailaze roho ya Marehemu Jeremia Sumari, mahali pema peponi, Amina.
Imetolewa leo Januari 20, 2012
John Mnyika (Mb),
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi
CHADEMA imefikia uamuzi huo ili kuwezesha viongozi wake wakuu wa chama, wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Dkt. Wilbrod Slaa kuwa karibu ili kujumuika na kuifariji familia ya marehemu pamoja na kushiriki katika kutoa heshima za mwisho kwa Marehemu Sumari.
Mungu ailaze roho ya Marehemu Jeremia Sumari, mahali pema peponi, Amina.
Imetolewa leo Januari 20, 2012
John Mnyika (Mb),
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi