OMUSILANGA
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 384
- 227
Ndiyo Wakuu , heshima kwenu ! Baada ya Kamanda Mawazo kuichakaza CCM Kwimba , wiki hii 2/1/2013 ata ongozana na Makamanda wa M4C kanda ya Ziwa kuwasha moto Igoma Jijini Mwanza. Ikumbukwe kuwa kata ya Igoma imekuwa kwenye sintofahamu kubwa baada ya Diwani wa kata hiyo Ndgu Adam Chagulani kuvuliwa uanachama na kamati kuu kwa tuhuma za kukihujumu chama cha CDM hapa Mwanza. Baada ya kuvuliwa udiwani yeye na Henry Matata walikwenda kupinga uamzi huo Mahakamani. Kwa hiyo mkutano huo ni mwendelezo wa kufikisha dhima pana ya vuguvugu la mabadiliko i.e M4C kwa Wananchi wote . Pia Mkutano huo umelenga kukemea na kulaani hujuma zinazo ratibiwa na kuendeshwa na CCM za kuwanunua vijana Wa Cdm ambao ki msingi wameonekana kuwa ni wachumia tumbo na Wapiga dili tofauti na wao wanavyo jitangaza kwenye vyombo vya Uchwara kwamba wao ni Wazalendo na Wana uchungu na nchi hii. Nape na Mwigulu chini ya ccm wanatakiwa wanunue dawa na vitanda hospitalini, madawati na vitabu, wajenge madarasa, waongeze mishahara ya walimu, madaktari na polisi, watoe mikopo kwa dada zetu wanaojiuza vyuo vikuu kwa sababu ya njaa, wapeleke misaada wa chakula ngorongoro watu wanakufa njaa na wala si kuhangaika na vijana hawa ambao serikali ya ccm imewanyima ajira. MY TAKE :- SISI SOTE NI NDUGU, ADUI YETU NI CCM.