Kama Wewe ni Mwana-CHADEMA, chama kinakuhitaji kuliko wakati wowote

KalamuTena

JF-Expert Member
Jul 7, 2018
13,189
17,157
Sidhani kuwa kuna wakati wowote ambapo chama kiliwahi kukuhitaji kama ilivyo kwa wakati huu.

Pengine utakuwa na sababu zako maalum zilizokufanya uwe mwanachama wa chama hicho, lakini hata kama sababu mojawapo si kwa sababu ya chama chako kusimamia HAKI, UHURU na DEMOKRASIA, bila shaka wajibu huu (mpya? wa chama chako haukuondolei mapenzi kwa chama hicho.

Katibu Mkuu John Mnyika katika taarifa yake hivi karibuni, alitaja "wajibu" alionao mwanachama wa chama hicho, ikiwa ni pamoja na "kukilinda dhidi ya mahasimu wake.

Nyote sasa, mnaelewa barabara kwamba chama chenu hakitakiwi kuwepo.

Kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA, kuna sababu ipi zaidi ya kukilinda chama chako kisipotee?

Unaweza usiwe tayari kuitikia wito wa viongozi wako katika kushiriki katika baadhi ya mambo yanayoandaliwa na chama ili kuonyesha ulimwengu kwamba chama kina wanachama wanaokijali na wapo tayari kukilinda chama chao, lakini kama mwanachama, kweli utakosa kushiriki hata katika jambo moja tu la kuonyesha ujali wako kwa chama chako?

Kwani CHADEMA inao wanachama wangapi?

Hata milioni moja inatosha kabisa kwa wanachama kiasi hicho kuionyesha dunia kwamba chama chao hakiwezi kuchezewa..., siyo kwa kuvunja sheria, lakini kushiriki ndani ya sheria zilizopo, kumzuia SIRRO kujifanya kwamba yeye ndiye mwenye haki ya kuamua hatma ya nchi hii.

Kama wewe ni mTanzania, hata kama ni mwanachama wa CCM, anayejali hatma ya Tanzania yetu, hata wewe unao wajibu wa kukataa nchi yetu kuvurugwa na hawa viongozi waliokosa mwelekeo.

Hutakubali kukaa kimya na kujifanya yanayotokea wewe hayakuhusu. Wote yanatuhusu. Ni lazima tushiriki kwa njia mbalimbali kuwaonyesha hawa viongozi wetu kwamba wanayofanya sasa yanavuka mipaka, tuyakatae. SIRRO na jeshi lake lenye mitutu hawezi kudharau sauti zetu tukikataa upuuzi anaofanya.

Sisi wengine wote, tunaweza tusiwe na mapenzi yoyote na Chama cha CHADEMA, lakini uTanzania wetu pekee unatosha, tukatae kuvurugwa kwa HAKI ndani ya nchi yetu.

Tushiriki kadri tunavyoweza kuwazuia viongozi wakandamizaji wa haki bila kujali ni nani anayenyimwa haki yake.

Siyo lazima tuwe kwenye mikusanyiko ya CHADEMA, lakini kuna njia nyingi sana za kuwaunga mkono katika juhudi za kukataa uonevu.

Kazi hii itakuwa nyepesi tukishiriki kwa pamoja katika njia mbalimbali za kuunga mkono juhudi hizo. CHADEMA watachambua na kuzieleza njia hizo za wananchi wa makundi mbalimbali wanazoweza kushiriki katika mchango wao wa kuondoa ukandamizaji Tanzania.

Nimetirirka tu, kama kuna makosa, sahihisha.
 
Kama wewe ni mTanzania, hata kama ni mwanachama wa CCM, anayejali hatma ya Tanzania yetu, hata wewe unao wajibu wa kukataa nchi yetu kuvurugwa na hawa viongozi waliokosa mwelekeo...
Asante kwa bandiko elimishi, naunga mkono hoja ila mimi maoni yangu ni kutoa tuu ushauri. Kwa vile IGP Kamanda Sirro emesema Jeshi la Polisi lina ushahidi, nadhani ni busara tungesubiria kuusikia huo ushahidi.

Nashauri pia tujenge utamaduni wa kuheshimu maoni ya wengine hata kama hatukubaliani nayo.

P.
 
Asante kwa bandiko elimishi, naunga mkono hoja ila mimi maoni yangu ni kutoa tuu ushauri. Kwa vile IGP Kamanda Sirro emesema Jeshi la Polisi lina ushahidi, nadhani ni busara tungesubiria kuusikia huo ushahid...
Wewe unapokwenda mahakamani kusikiliza kesi anayotuhumiwa nayo rafiki yako, huwa unakwenda kupinga mashtaka anayotuhumiwa nayo? Hao watakaokwenda kusikiliza hapo mahakamani wametangaza kwenda kupinga maoni ya SIRRO?

Wanvunja sheria gani wakihudhuria hapo mahakamani kwa amani hadi SIRRO aawatangazie kipigo?
 
mara nyigi nilikuwa najiuliza kwa nini viongozi na wafuasi wa Chadema mara zote ni Wakorofi na huioa lugha za kuitisha mamlaka?
Kumbe Jibu lake ndio hili, kweli waswahili husema mtoto wa nyoka ni nyoka.

Kumbe kiongozi wa Chama alikuwa ananunua na kupanga vitendo vya kigaidi....ndio maaana wafuasi wa chadema ni wakorofi hatari.
Ushauri wangu, viongozi wa Chadema na wafuasi wote badilikeni, acheni vitendo vya uvunjifu wa amani, na kwa sasa IGP katangaza operesheni kubwa ya kuwasaka wale wote wenye lengo la kuvunja sheria.

Ushauri kwa Jeshi la polisi;
kuna haja ya kufuatilia nyendo za viongozi na wafuasi wa Chaema kila kona ya nchi.
 
Sidhani kuwa kuna wakati wowote ambapo chama kiliwahi kukuhitaji kama ilivyo kwa wakati huu.

Pengine utakuwa na sababu zako maalum zilizokufanya uwe mwanachama wa chama hicho, lakini hata kama sababu mojawapo si kwa sababu ya chama chako kusimamia HAKI, UHURU na DEMOKRASIA, bila shaka wajibu huu (mpya? wa chama chako haukuondolei mapenzi kwa chama hicho.

Katibu Mkuu John Mnyika katika taarifa yake hivi karibuni, alitaja "wajibu" alionao mwanachama wa chama hicho, ikiwa ni pamoja na "kukilinda dhidi ya mahasimu wake.

Nyote sasa, mnaelewa barabara kwamba chama chenu hakitakiwi kuwepo.

Kama wewe ni mwanachama wa CHADEMA, kuna sababu ipi zaidi ya kukilinda chama chako kisipotee?

Unaweza usiwe tayari kuitikia wito wa viongozi wako katika kushiriki katika baadhi ya mambo yanayoandaliwa na chama ili kuonyesha ulimwengu kwamba chama kina wanachama wanaokijali na wapo tayari kukilinda chama chao, lakini kama mwanachama, kweli utakosa kushiriki hata katika jambo moja tu la kuonyesha ujali wako kwa chama chako?

Kwani CHADEMA inao wanachama wangapi?

Hata milioni moja inatosha kabisa kwa wanachama kiasi hicho kuionyesha dunia kwamba chama chao hakiwezi kuchezewa..., siyo kwa kuvunja sheria, lakini kushiriki ndani ya sheria zilizopo, kumzuia SIRRO kujifanya kwamba yeye ndiye mwenye haki ya kuamua hatma ya nchi hii.

Kama wewe ni mTanzania, hata kama ni mwanachama wa CCM, anayejali hatma ya Tanzania yetu, hata wewe unao wajibu wa kukataa nchi yetu kuvurugwa na hawa viongozi waliokosa mwelekeo.

Hutakubali kukaa kimya na kujifanya yanayotokea wewe hayakuhusu. Wote yanatuhusu. Ni lazima tushiriki kwa njia mbalimbali kuwaonyesha hawa viongozi wetu kwamba wanayofanya sasa yanavuka mipaka, tuyakatae. SIRRO na jeshi lake lenye mitutu hawezi kudharau sauti zetu tukikataa upuuzi anaofanya.

Sisi wengine wote, tunaweza tusiwe na mapenzi yoyote na Chama cha CHADEMA, lakini uTanzania wetu pekee unatosha, tukatae kuvurugwa kwa HAKI ndani ya nchi yetu.

Tushiriki kadri tunavyoweza kuwazuia viongozi wakandamizaji wa haki bila kujali ni nani anayenyimwa haki yake.

Siyo lazima tuwe kwenye mikusanyiko ya CHADEMA, lakini kuna njia nyingi sana za kuwaunga mkono katika juhudi za kukataa uonevu.

Kazi hii itakuwa nyepesi tukishiriki kwa pamoja katika njia mbalimbali za kuunga mkono juhudi hizo. CHADEMA watachambua na kuzieleza njia hizo za wananchi wa makundi mbalimbali wanazoweza kushiriki katika mchango wao wa kuondoa ukandamizaji Tanzania.

Nimetirirka tu, kama kuna makosa, sahihisha.
Kama Ni Hela Mseme. Tuwape Tunawakubali CHADEMA
 
Mahakamani si sehemu ya MAANDAMANO.....

Mahakamani si sehemu ya MIKUSANYIKO MIKUBWA.....

Wanasheria wanafahamu kiitwacho "VOX POPULI vs DICTATES OF THE LAW.....

Mikusanyiko hiyo inaweza kuathiri majaji wakasukumwa kutoa maamuzi ya KISHINIKIZO.....

#RespectOfTheRuleOfTheLaw
#KaziInaendelea
 
Back
Top Bottom