Chahali tumekusoma ila mimi nina machache kwako:
Inawezekana una ushauri au mawazo mazuri wakati fulanifulani, hata hivyo hoja zako zinakosa tija mara nyingi kwa sababu kadhaa. Labda nikuambie chache kwa ujumla wa kauli zako ziada ya uliyoitoa hapa
Sikiliza Chahali: Wewe ni mtu unayejivunia sana kuwa afisa wa usalama wa taifa utadhani wewe ndio mtanzani apekee uwewahi kufanya hiyo kazi au wewe ndio ulikua mkurugezi mkuu wa TISS au afisa bora kuliko wote. Hakuna kitu unaandika au unasema bila kuingiza ama hisia, kauli, misemo, uzushi, misiamiti, na mbwembwe za mwanausalama. Hivi kama kila daktari, mhandishi, mwalimu, mwanajeshi, mkunga, na wengine kwenye taalama zao watakua wanazitumia katika kujenga hoja au kuonesha umuhim wao au kuelezea mambo ya kijamii, tutaelewana kweli? Unataka kumfanya kila mtu anayekusoma aone usalama wa taifa ndio kazi bora, nyeti, na ya maana kuliko zote hivyo mtu aliyepita huko basi yeye ni mjuaji wa kila kitu, anajua siri nyingi na ni wa kuogopewa. Huu ni uzushi. Una miaka zaidi ya 10 tangu umekimbia hapa nyumbani, siri zote ulizoondoka nazo kwa sasa sio siri tena na zimepitwa na wakati. Wengi uliofanya nao kazi wengine wamebadilika kwa mengi na kustaafu. Labda uliotuacha vijana wadogo tukianza kazi ndio tumebaki na kumbukumbu zako. Ni uzushi uliopita mipaka kila siku kuwaaminisha watu kwamba wewe una siri za nchi, una siri za serikali, unajua CCM inafanya nini, unajua Rais anahusikaje na kitengo, na mengine. Unatumia habari za kuokoteza mitandaoni kujenga taswira isiyo sahihi kabisa juu ya ujuaji wako na unautumia kupotosha. hakuna intellejensia unayoijua kwa sasa zaidi ya kwenye vitabu na maandishi mengine ambayo kila mtu anaweza kujisomea. Huwezi kua nje ya kitengo kwa miaka zaidi ya 10 na bado ukajidai unajua utendaji wake.
Sikiliza Chahali: Unapenda kujifanya wewe ni mjuaji sana wa mbinu na mikakati ya kisiasa. Ila kwa taarifa zako ambazo wewe mwenyewe umezijaza mitandaoni, hujawahi kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi wa CCM wakati unakitumikia na kukisaidia kuiba kura. Hujawahi kusimama jukwaani wala kupigiwa kura. Hujawahi hata kuteuliwa kusaidia kazi za kisiasa. Ila ni ajabu sana unapokua mtaalamu juu wa wataalamu wote kuhusu siasa. Moja ya makala yako ulituambia jinsi ulivyohusika au kujua kama afisa wa TISS kuiba kura za wapinzani kuanzia mwaka 1995.. huo uzoefu sidhani kama CDM na wapinzani wengine wa kweliu wanauhitaji.
Sikiliza Chahali: Wewe ni kigeugeu, huna msimamo, na huna moral values za kuwanyooshea wengine vidole. Kwanza hadi leo hujawahi kutuambia watanzania nini kilikukimbiza Tanzani ukaenda kujificha huko Uingereza. Umebaki kujisifia ni afisa usalama mstaafu na kuitaja Scotland kama utambulisho wako na kama mafanikio yako makubwa. Wewe ulikua unaipinga CCM kwa miaka mingi lakini 2015 ghafla ukageuka kuwa mpiga debe wa CCM hata kuliko wenye chama chao. Hazijapita siku nyingi ukatuandikia kitabu cha kumsifu Magufuli ambacho leo hata wewe mwenyewe unakikimbia na huwezi kuikiongelea.. ulaji ulipokata CCM (ulituambia kwenye Makala uliyomwandikia Kinana) ghafla ukageuka kuwa mpinzani mkubwa wa mtu uliyempigia kampeni. Napata wasiwasi labda hakukupa asante na mshiko kwa kumuandikia kitabu cha kumsifu. Ulikua unabeza na kuwadhalilisha viongozi wa CDM mitandano ghafla ukaanza tena kuwa mtetezi wao. Umeona CDM hakuna ulaji na malipo kama uliyolipwa na CCM wakati wa kampeni sasa umegeuka kuwa KUNGWI wa kuwafundisha siasa na namna ya kupambana na CCM huku ukiwa umejificha nyuma ya kompyuta huko Uingereza. Unatoa wapi huo ujasiri wa kuwasema CDM wakati wenzako wako katika uwanja wa vita wananusa harufu ya damu?
Sikiliza Chahali: Tuchukulie kwamba una nia njema ya kuisaidia CDM au wapinzani wengine ambao wewe hutaki kujiunga nao. Ila umewahi kuona wapi askari walio kwenye kikosi cha mapambano wanaanza kudharauliana na kukebehiana hadharani na mbele ya adui wanayepambana naye? kwa nini usiwe unawasida CDM na wapinzani wengine kimkakati kwa kutumia huo utalaamu wako unajigamba nao? Kama unajua CDM haina kitengo cha intellejensia na wewe ni mwana intelejensia kwa nini usijiunge na kuwaonesha una msaada? unataka kila unachofanya dunia nzima ijue na kisiposikilizwa ghafla unageuka kuwa mkosaji. Ni mtu ambaye hajui ugumu wa siasa za Tanzania chini ya JPM pekee kama wewe anayeweza kuwa jasiri anayeweza kuwa na ujasiri wa kutumia muda mwingi kuwakosao na kupambana na watu kama CDM na wenzao wachache kama kina Zitto na Mtatito ambayo wameyaweka maisha yao rehani kuwasemea watanzania wasioweza kujieleza. Wewe uliyejificha nyuma ya kompyuta au simu yako, kikubwa ungewasaidia nyuma ya pazia kwa taarifa na mikakati kama unayo na sio kuwabwekea hadharani kila mara na kwamba hawashauriki.
Sikiliza Chahali: Inawekana kukaa huko ulikojificha kumekupa mwanga wa mambo kadha wa kadha kwa sababu zilizo wazi. Ila ni uzushi kutaka kuwaaminisha watanzania wewe unajua kila kitu. ninapopita kwenye miaandishi yako mitandaoni wewe ni mtaalamu wa kila kitu. unafundisha watu kila kitu kuanzia IT, mitandano, usalama, busara, maadili, biashara, uandishi, siasa, jinsi ya kufanikiwa, nk. Halafu ukiulizwa hata maswali ya kawaida kabisa ya ufafanuzi unakua mkali sana na kuanza kuporomosha matusi na kushambulia watu. Kwa umri wako na utaalamu unaojigamba unao havifanani kabisa na matusi unayotukana watu mitandaoni.
Sikiliza Chahali: Nikushauri kua inapokuja kwenye siasa za hapa Tanzania chini ya uongozi wa kikatili na kiimla uliopo, kama nawe hufurahishwi nayo huko nyuma ya kompyuta uliko jitahidi tu kutoa maoni na kukemea kama wengi wafanyavyo. Ila huna kabisa uwezo na mamlaka ya kimaadili na ujuzi wa kuwafunisha CDM au ACT au CUF namna ya kufanya siasa za kuimarisha vyama vyao, kuzuia watu kuhama, na namna ya kukabiliana na serikali inayoendeshwa na mitazamo katili. Kama vipi njoo ujiunge kwenye chama hata cha Dovutwa ili nawe ufanye harakati za kupambana na CCM uone inavyofanana. Maumivu tunayoyapata hapa nyumbani yanatuondolea kabisa uvumilivu wa kumsikiliza mtu yoyote anayetumia nguvu kuwakosoa wanaopambana kwa ajili yetu, tusio na vyama, wenye vyama, na hata walio ndani ya CCM na wamenyamaza kwa uvumilivu wakiogopa kupigwa wao na shangazi zao. Waache CDM na vyama vingine vyenye nia ya dhati ya kupammba na ukatili unaondelea wafanye waanachoweza.
Sikiliza Chahali: ninapomalizia nikushauri wewe na mtanzania mwingine yoyote aliye ndani ya nchi au huko nje kokkote nyuma ya TV au kompyuta ambaye anachukia yanayoendelea nyumbani, tafadhali watieni moyo sana wanaopambana kwa ajili yetu. Wawe ni ACT, CDM, CUF, NCCR, au watu mmoja mmoja wenye ujasiri wa kusema au wanaotumia mitandao kuandika kinyume na ukatili na ungozi mbovu unaota mizizi kila kona, watiwe moyo na wasidiewe nila kujali madhaifu yao yasiiyo na madhara kwetu. Askari asiyejua kushika silaha au kulenga shabaha asaidiwe au kufundishwa namana ya kufanya lakini isiwe kumzoea kwamba hajui kupigana au ni dhaifu.
Ni mimi afisa mwenzako (ila sijakimbia wala kusatafu)
Mutumishi wa umma